< Isaya 25 >

1 Yahwe wewe ni Mungu wangu; nitakutukuza wewe, nitalisifu jina lako; maana umetenda matendo ya ajabu, mambo uliyoyapanga toka zamaini, kwa uaminifu na ukamilifu.
O Jehovah, thou art my God; I will exalt thee; I will praise thy name, For thou hast done wonderful things; Thine ancient purposes are faithfulness and truth.
2 Maana umeufanya mji kuwa chungu, ngome ya mji, uharibifu na ngome ya wageni kuwa si mji.
Thou hast made the city a heap; The fortified city a ruin. The palace of the barbarians is to be no more a city! It shall never be built again.
3 Hivyo basi watu wenye nguvu watakutukuza wewe; na mji waishio watu wasio na ukatili watakuogopa wewe.
Therefore shall mighty kingdoms praise thee; The cities of the terrible nations shall honor thee;
4 Maana umekuwa katika eneo salama kwa aliye masikni, makazi kwa mhitaji ambaye yuko kwenye dhiki- makazi kwa aliyeko kwenye dhoruba na kivuli kwa aliyeko kwenye jua. Pale punzi ya watu wakatili imekuwa kama dhoruba dhidi ya ukuta,
For thou hast been a defence to the poor; A defence to the needy in his distress; A refuge from the storm, a shadow from the heat, When the rage of tyrants was like a storm against a wall.
5 na jua kwenye aridhi kavu, na watazuia kelele za wageni, kama vile jua linavyozuiliwa na kivuli cha mawingu, hivyo basi nyimbo wasio na makosa zimejibiwa.
As heat in a dry land is made to vanish, So thou puttest down the tumult of the barbarians; As heat is allayed by a thick cloud, So the triumph of the tyrants is brought low.
6 Katika mlima huu Yahwe wa majeshi atafanya kwa watu sikukuu ya ya vitu vilivyonona, na mvinyo uliochaguliwa, zabuni ya nyama na sikuku juu ya sira.
Then in this mountain shall Jehovah of hosts prepare for all nations A feast of fat things, and wines kept on the lees; Of fat things full of marrow, of wines kept on the lees well refined.
7 Na katika mlima huu atauharibu mfuniko uliowekwa juu watu wote, na mtandao wa kusuka juu ya mataifa.
He will destroy in this mountain the covering that was cast over all people, And the veil that was spread over all nations.
8 Atameza kifo daima, na Bwana Yahwe atayafuta machozi katika nyuso zetu; na aibu ya watu wake itatupwa mbali kutoka duniani kote, maana Yahwe amesema hivyo.
He will destroy death forever; The Lord Jehovah will wipe away the tears from all faces, And the reproach of his people will he take away from the whole earth; For Jehovah hath said it.
9 Yatazungumzwa katika siku hiyo, ''Huyu ni Mungu wetu; na tunayemngoja, na atatuokoa. Huyu ni Yahwe; tuliyemngoja, tutafurahia na kushangilia wokovu wake.''
In that day shall men say, “Behold, this is our God; We waited for him, and he hath saved us; This is Jehovah, for whom we waited; Let us rejoice and exult in his salvation.”
10 Maana katika mlima huu mkono wa Bwana utashuka; na Moabu itakanyagwakangwa chini kwenye eneo lake, na hata majani yatakanyagwakanyagwa chini katika shimo lililojaa mbolea.
For the hand of Jehovah shall rest upon this mountain, And Moab shall be trodden down in his place, As straw is trodden down in a dung-pool.
11 Wataitawnya mikono yao katikati yao, kama vile mpiga mbizi atawanyavyo mikono yake wakati akipiga mbizi. Lakini Bwana atashusha kiburi chao chini japo kuwa na ujuzi katika mikono yao.
And he shall stretch out his hands in the midst of it, As the swimmer stretcheth out his hands to swim, But God shall put down his pride, Together with the devices of his hands.
12 Na ataiangusha chini kwenye aridhi kuta za ngome, kwenye mavumbi.
And the high bulwarks of thy walls will he lay low; He will bring them down to the ground; he will lay them in the dust.

< Isaya 25 >