< Isaya 20 >
1 Katika mwaka ambao Tartani alipofika kwa Ashdodi, alipotumwa na Sarjoni mfalme wa Asiria, nae akapigana na Ashdodd na akachukua.
In the year in which Tharthan entered into Ashdod, when Sargon, the king of the Assyrians, had sent him, and when he had fought against Ashdod and had captured it,
2 Mda huo Yahwe alizungumza na Isaya mwana wa Amozi, ''Nenda ukaondoe nguo za magunia katika kiuno chako, na ondoeni viatu vyenu kwenye miguu.'' Alifanya hivyo, tembeeni uchi na miguu wazi.
in that same time, the Lord spoke by the hand of Isaiah, the son of Amoz, saying: “Go forth, and remove the sackcloth from your waist, and take your shoes from your feet.” And he did so, going out naked and barefoot.
3 Yahwe asema, ''Kama ilivyokuwa kwa mtumishi wangu Isaya alivyotembea uchi na pasipo kuvaa viatu kwa miaka mitatu, ni ishara na dalili kuhusu Misri na kuhusu Ethiopia—
And the Lord said: Just as my servant Isaiah has walked naked and barefoot, as a sign and as a portent of three years over Egypt and over Ethiopia,
4 katika njia hii mfalme wa Asiria atawaongoza mateka wa Misri, na walioko uhamishoni Ethiopia, watoto kwa wazee, waliouchi na wasio na viatu, na ambao hawajajisitiri kuiweka Misri katika aibu.
so also will the king of the Assyrians force the captivity of Egypt, and the transmigration of Ethiopia: young and old, naked and barefoot, with their buttocks uncovered, to the shame of Egypt.
5 Watafadhaika na kuona aibu, kwa sababu ya Ethiopia ni matumaini yao na Misri ni utukufu wao.
And they will be afraid and confounded over Ethiopia, their hope, and Egypt, their glory.
6 Wenyeji wa pwani hiiwatasema siku hiyo, 'Kweli, hichi ndicho chanzo chetu cha matumaini, tulipokimbilia kuhitaji msaada kutoka kwa mfalme wa Asiria, je ni kwa jisi gani tunaweza kupona?''
And in that day, the inhabitants of a certain island will say: “Behold, this was our hope, we fled to them for help, to free us from the face of the king of the Assyrians. And now, how will we be able to escape?”