< Isaya 17 >
1 Tamko kuhusu Damaskasi.
[the] oracle of Damascus there! Damascus [is] about to be removed from a city and it will be a ruin of a ruin.
2 Miji ya Aroera itaharibiwa. Patakuwa na nafasi kwa ajili ya kutunzia mifugo, na hakuna hatakayeizuia.
[will be] abandoned [the] cities of Aroer for flocks they will be and they will lie down and there not [will be one who] terrifies.
3 Miji ilioachwa itatoweka kutoka Efraimu, ufalme katuka Damskasi, na walobaki Aramu-watakuwa kama utukufu wa watu wa Israeli-Hili ni tamko la Yahwe wa majeshi.
And it will cease fortress from Ephraim and kingship from Damascus and [the] remnant of Aram like [the] glory of [the] people of Israel they will be [the] utterance of Yahweh of hosts.
4 Itakuwa siku hiyo utukufu wa Yakobo utapungua, utakuwa mwembamba na kunona kwa mwili wake utapungua.
And it will be in the day that it will become low [the] glory of Jacob and [the] fatness of flesh its it will be made lean.
5 Itakuwa kama mvuna ikusanyavyo mavuno, na mkono wake huvuna maganda ya mazao. Itakuwa kama mtu atoae maganda ya mavuno katika bonde la Refaimu.
And it will be like [the] gathering of a harvest of standing grain and arm his ears of grain someone will reap and it will be like [one who] gathers ears of grain in [the] valley of Rephaim.
6 Masalia yataachwa, hata hivyo, mti wa mzabibu utatingishwa: Mizeituni miwili au mitatu iliyo juu sana matawi yake yako juu, manne au matano katka tawi la juu katika mti unaozaa-hili ni tamko la Yahwe, Mungu wa Israeli.
And it will be left in it gleanings like [the] beating of an olive tree two three olives at [the] top of [the] tree-top four five on branches its fruit-bearing [the] utterance of Yahweh [the] God of Israel.
7 Siku hiyo watu watawangalia Muumba wake, na macho yatamuangalia Mtakatifu wa Israeli.
In the day that he will look person on maker his and eyes his to [the] holy [one] of Israel they will see.
8 Hawatangalia madhabahu, kazi za mikono yao, wala hataangalia kile kinachofanywa na vidole vyao, nguzo za Ashera na picha ya jua.
And not he will look to the altars [the] work of hands his and [that] which they have made fingers his not he will see and the Asherah poles and the incense altars.
9 Siku hiyo miji yenye nguvu itakuwa kama msitu uliotelekezwa na juu ya kilele cha mlima, na palipo achwa kwa sababu ya wana wa Israeli patakuwa ukiwa.
In the day that they will be - [the] cities of refuge his like [the] forsaken [place] of the forest and the tree-top which they abandoned because of [the] people of Israel and it will be a desolation.
10 Maana mmemsahau Mungu wa wakovu wenu, na umeudharau mwamba wa nguvu zako. Hivyo basi umeotesha miti mizuri, na mizabibu mizuri iliyotoka ugenini,
For you have forgotten [the] God of salvation your and [the] rock of refuge your not you have remembered there-fore you plant plantations of pleasantness and [the] vine branch of a stranger you sow it.
11 Siku hiyo uliootesha na fensi na kulima. Mbegu zako zitaota mapema na kukua, lakini mavuno yatashindikana siku hiyo itakuwa huzuni na kukata tamaa.
On [the] day of planting your you cause to grow and in the morning seed your you cause to sprout a heap a harvest in a day of [being] sick and pain incurable.
12 Ole! Watu wenye ghasia, Kishindo chake ni kama mngurumo wa bahari, na kasi ya mataifa, wananguruma kama ngurumo ya maji mengi!
Woe to! [the] tumult of peoples many as roar [the] seas they roar! and [the] uproar of nations like [the] uproar of waters mighty they are in an uproar!
13 Mataifa yataunguruma kama maji mengi yaendao kasi, lakini Mungu atawakemea.
Nations like [the] uproar of waters many they are in an uproar! and he will rebuke it and it will flee from a distance and it will be chased like chaff of mountains before a wind and like whirling dust before a storm-wind.
14 Watakimbia mbali sana na watafukuzwa kama pumba kwenye mlima mbele ya upepo, kama mavumbi yazungukayo kwenye dhoruba. Wakati wa usiku, ona, hofu! Na kabla ya alfajiri watakwenda; hili ndilo eneo la wale waliotupora, na wale wanaotunyang'anya mali zetu.
To a time of evening and there! sudden terror before morning there not [is] it this [will be] [the] portion of [those who] plunder us and [the] lot of [those who] despoil us.