< Isaya 12 >

1 Siku hiyo utasema, ''Nitakushukuru wewe, Yahwe. Japo ulikuwa na hasira na mimi, laana yako imeondoka mbali, na umenifariji mimi,
And in that day you shall say, O LORD, I will praise you: though you were angry with me, your anger is turned away, and you comforted me.
2 Ona Bwana ni wokovu wangu; nitamwamini na sitakuwa na hofu, kwa Yahwe, ndio, Yahwe ni nguvu yangu na wimbo wangu. Amekuwa wokovu wangu.''
Behold, God is my salvation; I will trust, and not be afraid: for the LORD JEHOVAH is my strength and my song; he also is become my salvation.
3 Kwa furaha utachota maji kwenye kisima cha wokovu.
Therefore with joy shall all of you draw water out of the wells of salvation.
4 Siku hiyo utasema, ''Mshukuru Yahwe na ita jina lake; tangaza matendo yake miongoni mwa watu, tangaza jina lake limeinuliwa.
And in that day shall all of you say, Praise the LORD, call upon his name, declare his doings among the people, make mention that his name is exalted.
5 Mwiimbie Yahwe, maana ametenda matendo yaliotukuka; acha hili lijulikane dunia nzima.
Sing unto the LORD; for he has done excellent things: this is known in all the earth.
6 Lia kwa nguvu na piga kelele kwa furaha, enyi wakazi wa Sayuni, maana katikati yenu ni mtakatifu wa Israeli.
Cry out and shout, you inhabitant of Zion: for great is the Holy One of Israel in the midst of you.

< Isaya 12 >