< Isaya 10 >

1 Ole wao watimizao sheria zisizo za haki na waandikao sheria zisizo na haki.
Woe vnto them that decree wicked decrees, and write grieuous things,
2 Wanawanyima wahitaji haki yao, wanawaibia watu wangu walio masikini haki zao, wajane mateka wao, na kuwafanya waliofiwa na baba zao mawindo yao!
To keepe backe ye poore from iudgement, and to take away the iudgement of the poore of my people, that widowes may be their pray, and that they may spoyle the fatherlesse.
3 Hutafanya nini siku ya hukumu pale siku ya uaribifu itakapokuja kutoka mbali, utakimbilia msaada kwa nani? na utauacha utajiri wako wapi?
What will ye doe nowe in the day of visitation, and of destruction, which shall come from farre? to whom will ye flee for helpe? and where will ye leaue your glorie?
4 Hakuna kitakachobaki, utaota miongoni mwa wafungwa au kuanguka miongoni mwa wauwaji. Katika mambo yote haya, hasira yake haijapungua; badala yake mkono wake ameunjoosha hata sasa.
Without me euery one shall fall among them that are bound, and they shall fall downe among the slayne: yet for all this his wrath is not turned away, but his hand is stretched out still.
5 Ole kwa watu wa Asiria klabu ya asira yangu, fimbo ya asira yangu!
O Asshur, the rodde of my wrath: and the staffe in their hands is mine indignation.
6 Nimemtuma juu ya taifa lenye kiburi na juu ya watu waliobeba uwingi wa hasira. Ninaamuru chukua nyara, chukua mawindo, na kuwakanyaga wao kama matope mitaani.
I will sende him to a dissembling nation, and I will giue him a charge against the people of my wrath to take the spoyle and to take the pray, and to treade them vnder feete like the mire in the streete.
7 Lakini hichi sicho alichomaanisha, wala sivyo afikiriavyo. Maana katika moyo wake ni kuharibu na kuondoa mataifa.
But he thinketh not so, neither doeth his heart esteeme it so: but he imagineth to destroy and to cut off not a fewe nations.
8 Maana amesema, '' wakuu wote sio wafalme?
For he sayeth, Are not my princes altogether Kings?
9 Je? kalno si kama Karkemish? Je Hamathi si kama Arpadi? Je Samaria si kama Demeski?
Is not Calno as Carchemish? Is not Hamath like Arpad? Is not Samaria as Damascus?
10 Kama mikono yangu imeshinda falme za ibada ya sanamu, ikiwa sanamu zao za kuchonga ni bora kuliko sanamu za Yerusalemu
Like as mine hand hath founde the kingdomes of the idoles, seeing their idoles were aboue Ierusalem, and aboue Samaria:
11 na Kama nilivyofanya kule Samaria na sanamu zake zisizo na maana, je sitaweza kufanya hivyo Yerusalemu na sanamu zake?''
Shall not I, as I haue done to Samaria, and to the idoles thereof, so doe to Ierusalem and to the idoles thereof?
12 Pindi ambapo Bwana alipoimaliza kazi kwenye mlima Sayuni na juu ya Yerusalemu, nitayaadhibu maneno ya moyo wenye kiburi ya mfalme wa Asiria na majivuno yake.
But when the Lord hath accomplished all his worke vpon mount Zion and Ierusalem, I will visite the fruite of the proude heart of the King of Asshur, and his glorious and proud lookes,
13 Kwa maana amesema, ''Kwa nguvu zangu na kwa hekima yangu niliyoifanya. na Nimeelewa, na nimeondoa mipaka ya watu. nimewaibia akiba yao, ni kama nilioileta chini kwa wenyeji wake.
Because he said, By ye power of mine owne hand haue I done it, and by my wisdome, because I am wise: therefore I haue remooued the borders of the people, and haue spoyled their treasures, and haue pulled downe the inhabitants like a valiant man.
14 Na mkono wangu umezitoa mali za mataifa kama vile mtu ayakusanyavyo mayai, kama nilivyokusanya dunia yote. Hakuna atakayeperusha mabawa yake au kufungua midomo yake au kulia.''
And mine hand hath found as a nest the riches of the people, and as one gathereth egges that are left, so haue I gathered all the earth: and there was none to mooue the wing or to open the mouth, or to whisper.
15 Je shoka lijisifu lenyewe juu ya mtu anayelitumia? Je litajisifia lenyewe zaidi ya yule anaelitumia kukatia? Au fimbo imuinuae yeye ambaye si mti.
Shall the axe boast it selfe against him that heweth therewith? or shall the sawe exalt it selfe against him that moueth it? as if the rod shoulde lift vp it selfe against him that taketh it vp, or the staffe should exalt it selfe, as it were no wood.
16 Hivyo basi Yahwe wa majeshi atatuma wadhaifu miongoni mwa wasomi wa kijeshi; na chini ya utukufu na kuteketea kama kuteketea kwa moto.
Therefore shall the Lord God of hostes send amog his fat men, leannes, and vnder his glorie he shall kindle a burning, like the burning of fire.
17 Mwanga wa Isreli utakuwa moto, na Mtakatifu wake atakuwa ni moto unaoteketeza na kula mbigiri siku moja.
And the light of Israel shalbe as a fire, and the Holy one thereof as a flame, and it shall burne, and deuoure his thornes and his briers in one day:
18 Yahwe atauteketeza utukufu wa msitu wake na shamba lake linalostawi, vyote nafsi na mwili; itakuwa kama vile mgonjwa apotezae maisha yake.
And shall consume the glory of his forest, and of his fruitfull fieldes both soule and flesh: and he shalbe as ye fainting of a standard bearer.
19 Mabaka ya miti ya misitu itakuwa michache sana, ambayo mtoto anaweza kuyahesabu.
And the rest of the trees of his forest shalbe fewe, that a childe may tell them.
20 Siku hiyo, mabaki ya Israeli, familia ya Yakobo ambayo imekimbia, hawatategemea kushindwa, lakini watamtegemea Yahwe, Mtakatifu wa Israeli.
And at that day shall the remnant of Israel, and such as are escaped of the house of Iaakob, stay no more vpon him that smote them, but shall stay vpon ye Lord, ye Holy one of Israel in trueth.
21 Mabaki ya Yakobo yatarudi kwa Mungu mwenye nguvu.
The remnant shall returne, euen the remnant of Iaakob vnto the mightie God.
22 Kwa kupitia watu wako, Israeli ni kama mchanga kama pwani ya bahari, Mabaki yao tu ndio yatakayorudi. Uaribifu wa amri, na mahitaji ya wingi wa haki.
For though thy people, O Israel, be as the sand of the sea, yet shall the remnant of them returne. The consumption decreed shall ouerflow with righteousnesse.
23 Maana Bwana wa majeshi, anakaribia kuleta uharibifu utachukua nafasi kubwa kitika nchi.
For the Lord God of hostes shall make the consumption, euen determined, in the middes of all the land.
24 Hivyo basi Bwana Yahwe wa majeshi anasema, ''watu wangu mhishio Sayuni, msiwaogope watu wa Asiria. Atawangamiza nyie kwa fimbo na atawanyua wafanyakazi juu yenu, kama ilivyotokea kwa Wamisri.
Therefore thus saith ye Lord God of hostes, O my people, that dwellest in Zion, be not afraid of Asshur: he shall smite thee with a rod, and shall lift vp his staffe against thee after the maner of Egypt:
25 Msimuogope, kwa mda mfupi hasira yangu itakwisha juu yenu, na hasira yangu italeta uharibifu.''
But yet a very litle time, and the wrath shall be consumed, and mine anger in their destruction.
26 Hivyo Yahwe wa majeshi atapiga mjeledi juu yenu kama vile alivyoishinda Midiani karibu na mwamba Orebu. Na atanyanyua fimbo yake juu ya bahari kama alivyofanya kule Misri.
And ye Lord of hostes shall raise vp a scourge for him, according to the plague of Midian in the rocke Oreb: and as his staffe was vpon the Sea, so he will lift it vp after the maner of Egypt.
27 Siku hiyo mzigo wake utanyanyuliwa kwenye mabeba yako na nira katika shingo yako, nayo nira itaharibiwa kwa sababu ya unene.
And at that day shall his burden be taken away from off thy shoulder, and his yoke from off thy necke: and the yoke shalbe destroied because of the anoynting.
28 Adui amekuja Aiathi na amepitia Migroni; katika Michmashi ameyahifadhi mahitaji yake.
He is come to Aiath: he is passed into Migron: at Michmash shall he lay vp his armour.
29 Wamevuka juu ya njia na wamepunzika huko Geba. Rama inatetemeka na Gibea ya Sauli imekimbia.
They haue gone ouer the foorde: they lodged in the lodging at Geba: Ramah is afraide: Gibeah of Saul is fled away.
30 Lia kwa sauti, ewe binti wa Galimu! sikiliza, Laishashi! Maskini Anathothi!
Lift vp thy voyce, O daughter Gallim, cause Laish to heare, O poore Anathoth.
31 Madmena ni mkimbizi na mkazi wa Gebuni wamejikusanya wanakimbia kutafuta msada.
Madmenah is remoued: the inhabitants of Gebim haue gathered themselues together.
32 Siku hizi za leo atasimulia huko Nobi na atatingisha mlima wa binti Sayuni, mlima wa Yerusalemu.
Yet there is a time that he will stay at Nob: he shall lift vp his hand towarde the mount of the daughter Zion, the hill of Ierusalem.
33 Tazama, Bwana Yahwe wa majeshi atapunguza matawi kwa nguvu za kutisha; miti mirefu itakatwa chini, wanaojivuna wataangushwa.
Beholde, the Lord God of hostes shall cut off the bough with feare, and they of high stature shalbe cut off, and the hie shalbe humbled.
34 Atang'oa vichaka vya msitu kwa shoka, Lebanoni na utukufu wake utaanguka.
And he shall cut away the thicke places of the forest with yron, and Lebanon shall haue a mightie fall.

< Isaya 10 >