< Isaya 10 >
1 Ole wao watimizao sheria zisizo za haki na waandikao sheria zisizo na haki.
Woe to those who make unfair laws, and who, when writing, write injustice:
2 Wanawanyima wahitaji haki yao, wanawaibia watu wangu walio masikini haki zao, wajane mateka wao, na kuwafanya waliofiwa na baba zao mawindo yao!
in order to oppress the poor in judgment, and to do violence to the case of the humble of my people, in order that widows may be their prey, and that they might plunder the orphan.
3 Hutafanya nini siku ya hukumu pale siku ya uaribifu itakapokuja kutoka mbali, utakimbilia msaada kwa nani? na utauacha utajiri wako wapi?
What will you do on the day of visitation and calamity which is approaching from afar? To whom will you flee for assistance? And where will you leave behind your own glory,
4 Hakuna kitakachobaki, utaota miongoni mwa wafungwa au kuanguka miongoni mwa wauwaji. Katika mambo yote haya, hasira yake haijapungua; badala yake mkono wake ameunjoosha hata sasa.
so that you may not be bowed down under the chains, and fall with the slain? Concerning all this, his fury was not turned away; instead, his hand was still extended.
5 Ole kwa watu wa Asiria klabu ya asira yangu, fimbo ya asira yangu!
Woe to Assur! He is the rod and the staff of my fury, and my indignation is in their hands.
6 Nimemtuma juu ya taifa lenye kiburi na juu ya watu waliobeba uwingi wa hasira. Ninaamuru chukua nyara, chukua mawindo, na kuwakanyaga wao kama matope mitaani.
I will send him to a deceitful nation, and I will order him against the people of my fury, so that he may take away the plunder, and tear apart the prey, and place it to be trampled like the mud of the streets.
7 Lakini hichi sicho alichomaanisha, wala sivyo afikiriavyo. Maana katika moyo wake ni kuharibu na kuondoa mataifa.
But he will not consider it to be so, and his heart will not suppose it to be this way. Instead, his heart will be set to crush and to exterminate more than a few nations.
8 Maana amesema, '' wakuu wote sio wafalme?
For he will say:
9 Je? kalno si kama Karkemish? Je Hamathi si kama Arpadi? Je Samaria si kama Demeski?
“Are not my princes like many kings? Is not Calno like Carchemish, and Hamath like Arpad? Is not Samaria like Damascus?
10 Kama mikono yangu imeshinda falme za ibada ya sanamu, ikiwa sanamu zao za kuchonga ni bora kuliko sanamu za Yerusalemu
In the same manner as my hand reached the kingdoms of the idol, so also will it reach their false images, those of Jerusalem and of Samaria.
11 na Kama nilivyofanya kule Samaria na sanamu zake zisizo na maana, je sitaweza kufanya hivyo Yerusalemu na sanamu zake?''
Should I not do to Jerusalem and her false images, just as I have done to Samaria and her idols?”
12 Pindi ambapo Bwana alipoimaliza kazi kwenye mlima Sayuni na juu ya Yerusalemu, nitayaadhibu maneno ya moyo wenye kiburi ya mfalme wa Asiria na majivuno yake.
And this shall be: when the Lord will have completed each of his works on Mount Zion and in Jerusalem, I will act against the fruit of the exalted heart of king Assur, and against the glory of the haughtiness of his eyes.
13 Kwa maana amesema, ''Kwa nguvu zangu na kwa hekima yangu niliyoifanya. na Nimeelewa, na nimeondoa mipaka ya watu. nimewaibia akiba yao, ni kama nilioileta chini kwa wenyeji wake.
For he has said: “I have acted with the strength of my own hand, and I have understood with my own wisdom, and I have removed the limits of the people, and I have plundered their leaders, and, like one with power, I have pulled down those residing on high.
14 Na mkono wangu umezitoa mali za mataifa kama vile mtu ayakusanyavyo mayai, kama nilivyokusanya dunia yote. Hakuna atakayeperusha mabawa yake au kufungua midomo yake au kulia.''
And my hand has reached to the strength of the people, as to a nest. And, just as the eggs which have been left behind are gathered, so have I gathered the entire earth. And there was no one who moved a wing, or opened a mouth, or uttered a snarl.”
15 Je shoka lijisifu lenyewe juu ya mtu anayelitumia? Je litajisifia lenyewe zaidi ya yule anaelitumia kukatia? Au fimbo imuinuae yeye ambaye si mti.
Should the axe glorify itself over him who wields it? Or can the saw exalt itself over him who pulls it? How can a rod lift itself up against him who wields it, or a staff exalt itself, though it is only wood?
16 Hivyo basi Yahwe wa majeshi atatuma wadhaifu miongoni mwa wasomi wa kijeshi; na chini ya utukufu na kuteketea kama kuteketea kwa moto.
Because of this, the sovereign Lord, the Lord of hosts, will send leanness among his fat ones. And under the influence of his glory, a burning ardor will rage, like a consuming fire.
17 Mwanga wa Isreli utakuwa moto, na Mtakatifu wake atakuwa ni moto unaoteketeza na kula mbigiri siku moja.
And the light of Israel will be like a fire, and the Holy One of Israel will be like a flame. And his thorns and briers will be set ablaze and devoured, in one day.
18 Yahwe atauteketeza utukufu wa msitu wake na shamba lake linalostawi, vyote nafsi na mwili; itakuwa kama vile mgonjwa apotezae maisha yake.
And the glory of his forest and of his beautiful hill will be consumed, from the soul even to the flesh. And he will flee away in terror.
19 Mabaka ya miti ya misitu itakuwa michache sana, ambayo mtoto anaweza kuyahesabu.
And what remains of the trees of his forest will be so few, and so easily numbered, that even a child could write them down.
20 Siku hiyo, mabaki ya Israeli, familia ya Yakobo ambayo imekimbia, hawatategemea kushindwa, lakini watamtegemea Yahwe, Mtakatifu wa Israeli.
And this shall be in that day: those not added to the remnant of Israel, and those who escape of the house of Jacob, will not lean upon him who strikes them. Instead, they will lean upon the Lord, the Holy One of Israel, in truth.
21 Mabaki ya Yakobo yatarudi kwa Mungu mwenye nguvu.
The remnant of Jacob, again I say the remnant, will be converted to the mighty God.
22 Kwa kupitia watu wako, Israeli ni kama mchanga kama pwani ya bahari, Mabaki yao tu ndio yatakayorudi. Uaribifu wa amri, na mahitaji ya wingi wa haki.
For though your people, O Israel, will be like the sand of the sea, yet only a remnant of them will be converted. The consummation, having been shortened, will be inundated with justice.
23 Maana Bwana wa majeshi, anakaribia kuleta uharibifu utachukua nafasi kubwa kitika nchi.
For the Lord, the God of hosts, will accomplish an abbreviation and a consummation, in the midst of all the earth.
24 Hivyo basi Bwana Yahwe wa majeshi anasema, ''watu wangu mhishio Sayuni, msiwaogope watu wa Asiria. Atawangamiza nyie kwa fimbo na atawanyua wafanyakazi juu yenu, kama ilivyotokea kwa Wamisri.
For this reason, the Lord, the God of hosts, says this: “My people, who inhabit Zion: do not be afraid of Assur. He will strike you with his rod, and he will lift up his staff over you, on the way of Egypt.
25 Msimuogope, kwa mda mfupi hasira yangu itakwisha juu yenu, na hasira yangu italeta uharibifu.''
But after a little while and a brief time, my indignation will be consumed, and my fury will turn to their wickedness.”
26 Hivyo Yahwe wa majeshi atapiga mjeledi juu yenu kama vile alivyoishinda Midiani karibu na mwamba Orebu. Na atanyanyua fimbo yake juu ya bahari kama alivyofanya kule Misri.
And the Lord of hosts will raise up a scourge over him, like the scourge of Midian at the rock of Oreb, and he will raise up his rod over the sea, and he will lift it up against the way of Egypt.
27 Siku hiyo mzigo wake utanyanyuliwa kwenye mabeba yako na nira katika shingo yako, nayo nira itaharibiwa kwa sababu ya unene.
And this shall be in that day: his burden will be taken away from your shoulder, and his yoke will be taken away from your neck, and the yoke will decay at the appearance of the oil.
28 Adui amekuja Aiathi na amepitia Migroni; katika Michmashi ameyahifadhi mahitaji yake.
He will approach Aiath; he will cross into Migron; he will entrust his vessels to Michmash.
29 Wamevuka juu ya njia na wamepunzika huko Geba. Rama inatetemeka na Gibea ya Sauli imekimbia.
They have passed through in haste; Geba is our seat; Ramah was stupefied; Gibeah of Saul fled.
30 Lia kwa sauti, ewe binti wa Galimu! sikiliza, Laishashi! Maskini Anathothi!
Neigh with your voice, daughter of Gallim; pay attention, Laishah, impoverished woman of Anathoth.
31 Madmena ni mkimbizi na mkazi wa Gebuni wamejikusanya wanakimbia kutafuta msada.
Madmenah has moved away; be strengthened, you inhabitants of Gebim.
32 Siku hizi za leo atasimulia huko Nobi na atatingisha mlima wa binti Sayuni, mlima wa Yerusalemu.
It is still daylight, so stand at Nob. He will shake his hand against the mountain of the daughter of Zion, the hill of Jerusalem.
33 Tazama, Bwana Yahwe wa majeshi atapunguza matawi kwa nguvu za kutisha; miti mirefu itakatwa chini, wanaojivuna wataangushwa.
Behold, the sovereign Lord of hosts will crush the little bottle of wine with terror, and the exalted in stature will be cut down, and the lofty will be brought low.
34 Atang'oa vichaka vya msitu kwa shoka, Lebanoni na utukufu wake utaanguka.
And the dense forest will be overturned with iron. And Lebanon, with its exalted ones, will fall.