< Hosea 1 >

1 Hili ni neno la Bwana lililofika kwa Hosea mwana wa Beeri siku za Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda, na katika siku za Yeroboamu mwana wa Yoashi, mfalme wa Israeli.
Parole de Yahvé adressée à Osée, fils de Beéri, aux jours d'Ozias, de Jotham, d'Achaz et d'Ézéchias, rois de Juda, et aux jours de Jéroboam, fils de Joas, roi d'Israël.
2 Wakati Bwana alipozungumza kwanza kupitia Hosea, akamwambia, “Nenda ukajitwalie mke ambaye ni kahaba. Atakuwa na watoto ambao ni matokeo ya ukahaba wake. Kwa maana nchi inafanya uzinzi mkubwa kwa kumwacha Bwana.”
Lorsque Yahvé parla d'abord par Osée, il dit à Osée: « Va, prends pour toi une femme de prostitution et des enfants d'infidélité; car le pays commet un grand adultère, en abandonnant Yahvé. »
3 Basi Hosea akaenda akamwoa Gomeri binti Diblaimu, naye akachukua mimba, akazaa mtoti mwanamume.
Et il alla prendre Gomer, fille de Diblaïm; et elle conçut, et lui donna un fils.
4 Bwana akamwambia Hosea, Mwite jina lake Yezreeli. Kwa maana kwa muda mfupi nitaiadhibu nyumba ya Yehu kwa sababu ya kumwaga damu huko Yezreeli; nami nitamaliza ufalme wa nyumba ya Israeli.
Yahvé lui dit: « Appelle-le du nom de Jizreel, pour un peu de temps encore, et je vengerai le sang de Jizreel sur la maison de Jéhu, et je ferai cesser le règne de la maison d'Israël.
5 Itatokea siku ile nitakapovunja upinde wa Israeli katika bonde la Yezreeli.
Il arrivera en ce jour-là que je briserai l'arc d'Israël dans la vallée de Jizreel. »
6 Gomeri akachukua mimba tena akamzaa binti. Ndipo Bwana akamwambia Hosea, “Mwite jina lake Lo Ruhama; kwa maana sitawahurumia tena nyumba ya Israeli, nisije nikawasamehe kwa njia yoyote.
Elle conçut de nouveau, et enfanta une fille. Et il lui dit: « Appelle-la du nom de Lo-Ruhamah, car je n'aurai plus pitié de la maison d'Israël, et je ne leur pardonnerai plus d'aucune manière.
7 Hata hivyo nitawahurumia nyumba ya Yuda, nami nitawaokoa mwenyewe, Bwana, Mungu wao. Sitawaokoa kwa upinde, upanga, vita, farasi, au wapanda farasi. '
Mais j'aurai pitié de la maison de Juda, et je les sauverai par Yahvé, leur Dieu, et je ne les sauverai ni par l'arc, ni par l'épée, ni par la bataille, ni par les chevaux, ni par les cavaliers. »
8 Baada ya Gomeri kumwachisha Lo Ruhama, alipata mimba na kuzaa mtoto mwingine mwanamume.
Or, lorsqu'elle eut sevré Lo-Ruhamah, elle conçut et enfanta un fils.
9 Ndipo Bwana akasema, “Mwite jina la Lo Ami; kwa kuwa ninyi si watu wangu, wala mimi si Mungu wenu.”
Il dit: « Appelle-le Lo-Ammi, car vous n'êtes pas mon peuple, et je ne serai pas le vôtre.
10 Hata hivyo idadi ya watu wa Israeli itakuwa kama mchanga wa bahari, ambayo haiwezi kupimwa au kuhesabiwa. Itakuwa pale ambapo waliambiwa, “Ninyi si watu wangu,” wataambiwa, “Ninyi ni watu wa Mungu aliye hai.”
Mais le nombre des enfants d'Israël sera comme le sable de la mer, qui ne peut être ni mesuré ni compté; et là où on leur a dit: « Vous n'êtes pas mon peuple », on les appellera « fils du Dieu vivant ».
11 Watu wa Yuda na watu wa Israeli watakusanyika pamoja. Wao wataweka kiongozi mmoja wao wenyewe, na watatoka kutoka nchi, kwa maana itakuwa siku ya Yezreeli kuu.
Les enfants de Juda et les enfants d'Israël s'assembleront, ils se donneront une tête, et ils monteront du pays; car grand sera le jour de Jizreel.

< Hosea 1 >