< Hosea 9 >

1 Usifurahi, Israeli, kwa furaha kama watu wengine. Kwa maana haukuwa mwaminifu, umemuacha Mungu wako. Unapenda kulipa mshahara kwa kahaba kwenye sakafu zote za nafaka.
Israel, don't rejoice! Don't celebrate like other nations! For you have practiced prostitution; you have loved a prostitute's wages on every threshing floor of grain.
2 Lakini sakafu na divai hazitawalisha; divai mpya itampungukia.
Your threshing floors and winepresses will not feed you; the land will fail to produce your new wine.
3 Hawawezi kuendelea kuishi katika nchi ya Bwana; badala yake, Efraimu atarudi Misri, na siku moja watakula chakula kichafu katika Ashuru.
You will not stay in the Lord's land, instead Ephraim will return to Egypt, and will eat unclean food in Assyria.
4 Hawatamtolea Bwana sadaka za divai, wala hawatamfurahisha. Dhabihu zao zitakuwa kwao kama chakula cha matanga wote wanaolila watakuwa wamejisikia. Maana chakula chao kitakuwa chao pekee; hautakuingia nyumbani mwa Bwana.
You won't pour out any drink offerings to the Lord. None of your sacrifices will please him. Your sacrifices will be like food eaten by a person in mourning—all who eat will be unclean. You will eat this food yourselves, but it will not enter the house of the Lord.
5 Utafanya nini siku ya sikukuu iliyowekwa rasmi, siku ya sikukuu ya Yahweh?
What are you going to do on the days of your appointed religious feasts, on the days of the festivals of the Lord?
6 Kwa maana, angalia, wamekimbia uharibifu, Misri itawakusanya, na Nofu itawazika. Maana hazina zao za pesa za fedha zitakuwa nao, na miiba itajaza hema zao.
Look, they have left because of the destruction: Egypt with gather them, and Memphis will bury them. They gain a “valued possession” for their silver. Weeds will possess them, and thorns will grow over their tents.
7 Siku za adhabu zinakuja; siku za kulipiza kisasi zinakuja. Waisraeli wote wajue mambo haya. Nabii ni mpumbavu, na mtu aliyevuviwa ni mwendawazimu, kwa sababu ya uovu wako mkubwa na uadui mkubwa.
The time of punishment has come; the day of retribution has arrived. Let Israel know! You say the prophet is a fool, the man of the Spirit is mad, because your sin and hostility is so great.
8 Nabii ndiye mlinzi wa Mungu wangu juu ya Efraimu. Lakini mtego wa ndege ni juu ya njia zake zote, na uadui umo katika nyumba ya Mungu wake.
The watchman over Ephraim is with my God, and a prophet is a birdcatcher's snare on all his ways. Hatred is in the house of his God
9 Wamejiharibu wenyewe kama siku za Gibea. Mungu atawakumbusha uovu wao, naye atawaadhibu dhambi zao.
for they have corrupted themselves so deeply, as in the time of Gibeah. He will remember their sin; he will punish their wickedness.
10 Bwana asema, “Nilipoikuta Israeli, ilikuwa kama kutafuta zabibu jangwani. Kama matunda ya kwanza ya msimu kwenye mtini, nimewaona baba zenu. Lakini wakaenda Baal Peori, nao wakajitoa kwenye sanamu ya aibu. Walikuwa chukizo kama sanamu waliyoipenda.
When I found Israel, it was like finding grapes in the desert. When I saw your forefathers it was like seeing early fruit on the fig tree. But when they came to Baal Peor, they gave themselves over to that shameful idol, becoming as filthy as the filthy thing they loved.
11 Na kwa ajili ya Efraimu, utukufu wao utatoka kama ndege. Hakutakuwa na kuzaa, hakuna mimba, wala achukuaye mimba.
Ephraim! Like a bird that flies away so shall your glory—no births, no pregnancies, no conceptions.
12 Ingawa wameleta watoto, nitawachukua ili asibaki hata mmoja. Ole wao nikiwaacha!
Even if they bring up children, I will make sure they do not survive. What a disaster for you when I turn away from you!
13 Nimeiona Efraimu, kama vile Tiro, alipandwa katika mlima, lakini Efraimu atatoa watoto wake kwa mtu atakayewaua.
Ephraim! Just as I saw Tyre planted in a meadow, so too Ephraim will lead out his children to the murderer.
14 Wape, Bwana-utawapa nini? Wape tumbo lenye kuharibu mimba na matiti ambayo haitoi maziwa.
Give them—well, Lord, what should you give them? Give them wombs that miscarry and dry breasts.
15 'Kwa sababu ya uovu wao wote huko Gilgali, ndivyo nilipowachukia. Kwa sababu ya matendo yao ya dhambi, nitawafukuza nje ya nyumba yangu. Sitawapenda tena; maofisa wao wote ni waasi.
All of their evil began at Gilgal, and that's where I began to hate them. I will drive them out of my house because of their wickedness. I will love them no longer; all their leaders are rebels.
16 Efraimu ni mgonjwa, na mizizi yao imekauka; hawazai matunda. Hata ikiwa wana watoto, nitawaua watoto wao wapendwa.
Ephraim, you are blighted, dried up from the roots. You shall bear no fruit. Even if you have children, I will slaughter your beloved offspring.
17 Mungu wangu atawakataa kwa sababu hawakumtii. Watakuwa watu wa kutangatanga kati ya mataifa.
My God will reject you because you have not listened to him, and you will become homeless wanderers among the nations.

< Hosea 9 >