< Hosea 8 >

1 “Weka tarumbeta katika midomo yako! Tai anakuja juu ya nyumba ya Bwana kwa sababu watu wamevunja agano langu na waliasi dhidi ya sheria yangu.
To mouth your a horn like eagle over [the] house of Yahweh because they have transgressed covenant my and on law my they have rebelled.
2 Wananililia,'Mungu wangu, sisi katika Israeli tunakujua.'
To me they cry out O God my we know you Israel.
3 Lakini Israeli amekataa mema, na adui atamfuata.
It has rejected Israel good an enemy he will pursue him.
4 Wameweka wafalme, lakini sio kwa shauri langu. Wamewafanya wakuu, lakini sikuwa na habari. Kwa fedha zao na dhahabu wamejifanyia sanamu wenyewe, ili wakatiliwe mbali.”
They they have made kings and not from me they have installed leaders and not I knew silver their and gold their they have made for themselves idols so that it may be cut off.
5 “Ndama yako imekataliwa, Samaria. Hasira yangu inawaka juu ya watu hawa. Kwa muda gani watakuwa na hatia?
He has rejected calf your O Samaria it has burned anger my on them until when? not will they be able innocence.
6 Kwa maana sanamu hii ilitoka Israeli; fundi aliifanya; si Mungu! Ndama ya Samaria itavunjwa vipande vipande.
For [are] from Israel and it a craftsman he made it and not [is] God it for fragments it will become [the] calf of Samaria.
7 Kwa maana watu hupanda upepo na kuvuna kimbunga. Mbegu zilizosimama hazina vichwa; haitoi unga. Ikiwa itakomaa, wageni watakula.
For a wind they sow and a storm-wind they will reap standing grain not [belongs] to it growth not it will produce flour perhaps it will produce strangers they will swallow it.
8 Israeli imemezwa; sasa wanalala kati ya mataifa kama kitu kisicho na maana.
It will be swallowed Israel now they are among the nations like a vessel [which] there not [is] pleasure in it.
9 Kwa maana walikwenda Ashuru kama punda wa mwitu pekee. Efraimu ameajiri wapenzi kwa ajili yake mwenyewe.
For they they have gone up Assyria a wild donkey isolated to itself Ephraim they have hired (lovers *L(abh)*)
10 Hata ingawa wameajiri wapenzi kati ya mataifa, sasa nitawakusanya pamoja. Wao wataanza kupotea kwa sababu ya unyanyasaji wa mfalme wa wakuu.
also for they will hire among the nations now I will gather them and they have begun a few from [the] burden of a king princes.
11 Kwa maana Efraimu imeongeza madhabahu kwa sadaka za dhambi, lakini zimekuwa madhabahu kwa kufanya dhambi.
For he has multiplied Ephraim altars for sinning they have become to him altars for sinning.
12 Niliweza kuandika sheria yangu kwao mara elfu kumi, lakini wangeiona kama kitu cha ajabu kwao.
(I wrote *Q(k)*) for him ([the] numerous things of *Q(K)*) law my like a strange [thing] they are regarded.
13 Kwa ajili ya dhabihu za sadaka zangu, hutoa nyama na kuila, lakini mimi, Bwana, siwakubali. Sasa nitafikiri juu ya uovu wao na kuadhibu dhambi zao. Watarudi Misri.
[the] sacrifices of Gifts my they sacrifice flesh and they ate [it] Yahweh not he is pleased with them now he will remember iniquity their so he may punish sins their they Egypt they will return.
14 Israeli amenisahau mimi, Muumba wake, na amejenga majumba. Yuda ameimarisha miji mingi, lakini nitatuma moto juu ya miji yake; itaharibu ngome zake.
And he has forgotten Israel maker his and he has built palaces and Judah he has multiplied cities fortified and I will send fire on cities his and it will consume fortresses his.

< Hosea 8 >