< Hosea 7 >
1 Wakati wowote ninapotaka kuponya Israeli, dhambi ya Efraimu inafunuliwa, pamoja na matendo maovu ya Samaria, kwa sababu wanafanya udanganyifu; mwizi huingia, na kundi la wanyang'anyi hushambulia mitaani.
Whanne Y wolde heele Israel, the wickidnesse of Effraym was schewid, and the malice of Samarie was schewid, for thei wrouyten a leesyng. And a niyt theef entride, and robbid; a dai theef was withoutforth.
2 Hawatambui mioyoni mwao kwamba ninakumbuka matendo yao mabaya. Sasa matendo yao huwazunguka; yapo mbele ya uso wangu.
And lest thei seien in her hertis, that Y haue mynde on al the malice of hem, now her fyndyngis han cumpassid hem, tho ben maad bifor my face.
3 Kwa sababu ya uovu wao wamemfanya mfalme awe na furaha, na maofisa wao kwa uongo wao.
In her malice thei gladiden the kyng, and in her leesyngys `thei gladiden the princes.
4 Wote ni wazinzi, kama tanuru iliyochomwa na mwokaji, ambaye huacha kuuchochea moto tangu kukanda unga mpaka kuwa chachu.
Alle that doen auoutrie, ben as an ouene maad hoot of a bakere. The citee restide a litil fro the medlyng of sour douy, til al was maad sour `of sour douy.
5 Siku ya mfalme wetu, viongozi walijifanya wagonjwa na ukali wa divai. Alinyoosha mkono wake kwa wale waliokuwa wakidhihaki.
The dai of oure kyng; the princis bigunnen to be wood of wyn; he stretchide forth his hoond with scorneris.
6 kwa mioyo kama tanuri, wao hupanga mipango yao ya udanganyifu. Hasira zao hulala usiku wote; asubuhi huwaka juu kama moto.
For thei applieden her herte as an ouene, whanne he settide tresoun to hem. Al the niyt he slepte bakynge hem, in the morewtid he was maad hoot, as the fier of flawme.
7 Wote wamepata moto kama tanuru, na huwaangamiza wale wanaowatawala. Wafalme wao wote wameanguka; hakuna hata mmoja wao ananiita.
Alle weren maad hoot as an ouene, and thei deuouriden her iugis. Alle the kyngis of hem fellen doun, and noon is among hem that crieth to me.
8 Efraimu anajichanganya mwenyewe kati ya watu. Efraimu ni mkate ambayo haujawahi kugeuzwa.
Effraym hym silf was medlid among puplis; Effraym was maad a loof bakun vndur aischis, which is not turned ayen.
9 Wageni wamekula nguvu zake, lakini hajui. Nywele za mvi hunyunyiza juu yake, lakini hajui.
Aliens eeten the strengthe of hym, and he knew not; but also hoor heeris weren sched out in hym, and he knew not.
10 Kiburi cha Israeli kinawashuhudia; hata hivyo, hawajarudi kwa Bwana, Mungu wao, wala hawakumtafuta licha ya hayo yote.
And the pride of Israel schal be maad low in the face therof; thei turneden not ayen to her Lord God, and thei souyten not hym in alle these thingis.
11 Efraimu ni kama njiwa, baradhuli na asiye na busara, humwita kwenda Misri, kisha huruka kwenda Ashuru.
And Effraym was maad as a culuer disseyued, not hauynge herte. Thei clepiden Egipt to help, thei yeden to Assiriens.
12 Wakienda, nitasambaza wavu wangu juu yao, nami nitawaangusha kama ndege wa angani. Nitawaadhibu katika kusonga kwao pamoja.
And whanne thei ben goen forth, Y schal sprede abrood on hem my net, Y schal drawe hem doun as a brid of the eir. Y schal beete hem, bi the heryng of the cumpany of hem.
13 Ole wao! Kwa maana wamepotea kutoka kwangu. Uharibifu unawajia! Wao wameasi dhidi yangu! Napenda kuwaokoa, lakini waliongea uongo dhidi yangu.
Wo to hem, for thei yeden awei fro me; thei schulen be distried, for thei trespassiden ayens me. And Y ayenbouyte hem, and thei spaken leesyngis ayenus me.
14 Wala hawakunililia kwa moyo wao wote, lakini wanaomboleza kwenye vitanda vyao. Wanakusanyika kwa ajili ya nafaka na divai mpya, nao wananiasi mimi.
And thei crieden not to me in her herte, but yelliden in her beddis. Thei chewiden code on wheete, and wyn, and thei yeden awei fro me.
15 Ingawa niliwafundisha na kuimarisha mikono yao, sasa wanapanga mabaya dhidi yangu.
And Y tauyte, and coumfortide the armes of hem, and thei thouyten malice ayens me.
16 Wanarudi, lakini harudi kwangu, Niliye Juu. Wao ni kama upinde usiotumainika. Maofisa wao wataanguka kwa upanga kwa sababu ya udhalimu wa vinywa. Hii itakuwa ni aibu yao katika nchi ya Misri.
Thei turneden ayen, that thei schulden be with out yok; thei ben maad as a gileful bowe. The princis of hem schulen falle doun bi swerd, for the woodnesse of her tunge; this is the scornyng of hem in the lond of Egipt.