< Hosea 7 >

1 Wakati wowote ninapotaka kuponya Israeli, dhambi ya Efraimu inafunuliwa, pamoja na matendo maovu ya Samaria, kwa sababu wanafanya udanganyifu; mwizi huingia, na kundi la wanyang'anyi hushambulia mitaani.
“When I give healing to Israel, Then the iniquity of Ephraim is revealed, And the wickedness of Samaria, For they have worked falsehood, And a thief comes in, A troop has stripped off in the street,
2 Hawatambui mioyoni mwao kwamba ninakumbuka matendo yao mabaya. Sasa matendo yao huwazunguka; yapo mbele ya uso wangu.
And they do not say to their heart, [That] I have remembered all their evil, Now their doings have surrounded them, They have been before My face.
3 Kwa sababu ya uovu wao wamemfanya mfalme awe na furaha, na maofisa wao kwa uongo wao.
With their wickedness they make a king glad, And with their lies—princes.
4 Wote ni wazinzi, kama tanuru iliyochomwa na mwokaji, ambaye huacha kuuchochea moto tangu kukanda unga mpaka kuwa chachu.
All of them [are] adulterers, Like a burning oven of a baker, He ceases from stirring up after kneading the dough, until its leavening.
5 Siku ya mfalme wetu, viongozi walijifanya wagonjwa na ukali wa divai. Alinyoosha mkono wake kwa wale waliokuwa wakidhihaki.
A day of our king! Princes have defiled themselves [with] the poison of wine, He has drawn out his hand with scorners.
6 kwa mioyo kama tanuri, wao hupanga mipango yao ya udanganyifu. Hasira zao hulala usiku wote; asubuhi huwaka juu kama moto.
For they have drawn near, Their heart [is] as an oven In their lying in wait—their baker sleeps all night, Morning! He is burning as a flaming fire.
7 Wote wamepata moto kama tanuru, na huwaangamiza wale wanaowatawala. Wafalme wao wote wameanguka; hakuna hata mmoja wao ananiita.
All of them are warm as an oven, And they have devoured their judges, All their kings have fallen, There is none calling to Me among them.
8 Efraimu anajichanganya mwenyewe kati ya watu. Efraimu ni mkate ambayo haujawahi kugeuzwa.
Ephraim! He mixes himself among peoples, Ephraim has been an unturned cake.
9 Wageni wamekula nguvu zake, lakini hajui. Nywele za mvi hunyunyiza juu yake, lakini hajui.
Strangers have devoured his power, And he has not known, Also old age has sprinkled [itself] on him, And he has not known.
10 Kiburi cha Israeli kinawashuhudia; hata hivyo, hawajarudi kwa Bwana, Mungu wao, wala hawakumtafuta licha ya hayo yote.
And the excellence of Israel has been humbled to his face, And they have not turned back to their God YHWH, Nor have they sought Him for all this.
11 Efraimu ni kama njiwa, baradhuli na asiye na busara, humwita kwenda Misri, kisha huruka kwenda Ashuru.
And Ephraim is as a simple dove without heart, Egypt they called on—[to] Asshur they have gone.
12 Wakienda, nitasambaza wavu wangu juu yao, nami nitawaangusha kama ndege wa angani. Nitawaadhibu katika kusonga kwao pamoja.
When they go I spread over them My net, As the bird of the heavens I bring them down, I discipline them as their congregation has heard.
13 Ole wao! Kwa maana wamepotea kutoka kwangu. Uharibifu unawajia! Wao wameasi dhidi yangu! Napenda kuwaokoa, lakini waliongea uongo dhidi yangu.
Woe to them, for they wandered from Me, Destruction to them, for they transgressed against Me, And I ransom them, and they have spoken lies against Me,
14 Wala hawakunililia kwa moyo wao wote, lakini wanaomboleza kwenye vitanda vyao. Wanakusanyika kwa ajili ya nafaka na divai mpya, nao wananiasi mimi.
And have not cried to Me with their heart, but howl on their beds; They assemble themselves for grain and new wine, They turn aside against Me.
15 Ingawa niliwafundisha na kuimarisha mikono yao, sasa wanapanga mabaya dhidi yangu.
And I instructed—I strengthened their arms, And concerning Me they think evil!
16 Wanarudi, lakini harudi kwangu, Niliye Juu. Wao ni kama upinde usiotumainika. Maofisa wao wataanguka kwa upanga kwa sababu ya udhalimu wa vinywa. Hii itakuwa ni aibu yao katika nchi ya Misri.
They turn back—not to the Most High, They have been as a deceitful bow, Their princes fall by sword, From the insolence of their tongue, This [is] their derision in the land of Egypt!”

< Hosea 7 >