< Hosea 6 >
1 “Njoo, turudi kwa Bwana. Kwa maana ametuvunja vipande vipande, lakini atatuponya; ametujeruhi, lakini atatufunga majeraha yetu.
“Come on! Let's go back to the Lord. He has torn us to pieces, but now he will heal us. He has struck us down, but now he will bind up our wounds.
2 Baada ya siku mbili atatufufua; siku ya tatu atatuinua, na tutaishi mbele yake.
In two days he will heal us; after three days he will raise us up so we can live in his presence.
3 Nasi tumjue Bwana; tukaendelee kumjua Bwana. Kuja kwake ni hakika kama asubuhi; atakuja kwetu kama mvua, kama mvua ya vuli ambayo huinyeshea ardhi.”
Let's get to know the Lord, really strive to know him, and he will appear to us as surely as the sun will rise; he will come to us as certainly as the spring rains fall on the earth.”
4 Efuraimu, nikufanyie nini? Yuda, nikufanyie nini? Uaminifu wako ni kama wingu la asubuhi, kama umande unaoondoka mapema.
Ephraim, what shall I do with you? Judah, what shall I do with you? Your love disappears like mist at dawn; it vanishes like dew in the morning.
5 Kwa hiyo nimewavunja vipande vipande kwa vinywa vya manabii, nimewaua kwa maneno ya kinywa changu. Maagizo yako ni kama nuru inayoangaza.
So I cut you down through the prophets; I killed you with my words. My judgment shines out like a light.
6 Kwa maana natamani uaminifu wala si dhabihu, na kumjua Mungu kuliko sadaka za kuteketezwa.
I want your true love, not your sacrifices; I want you to know me, not your burnt offerings.
7 Kama Adamu wamevunja agano; hawakuwa waaminifu kwangu.
But you, just like Adam, broke our agreement, there you were unfaithful to me.
8 Gileadi ni jiji la wahalifu wenye miguu ya damu.
Gilead is a city of evil people where footprints are tracked in blood.
9 Kama makundi ya wanyang'anyi wanaomngojea mtu, hivyo makuhani hujiunga pamoja kufanya mauaji kwa njia ya Shekemu; wamefanya uhalifu wa aibu.
Priests are like a gang of bandits, lying in wait to ambush travelers on the road. They commit murder in Shechem, carrying out wicked crimes.
10 Katika nyumba ya Israeli nimeona jambo baya; Uzinzi wa Efraimu ukopale, na Israeli ametiwa unajisi.
I have seen in the house of Israel something totally disgusting: Ephraim engages in prostitution and Israel is sexually corrupt.
11 Kwa maana wewe, Yuda, mavuno yameteuliwa, nitakaporudisha urithi wa watu wangu.
And as for you, Judah, your harvest-time has been set! When I restore the fortunes of my people,