< Hosea 5 >
1 Sikilizeni haya, makuhani! kuweni makini, nyumba ya Israeli! Sikilizeni, nyumba ya mfalme! Kwa maana hukumu itakuja juu yenu nyote. Mmekuwa mtego huko Mizpa na wavu uliosambazwa juu ya Tabori.
Entendez-le, sacrificateurs, écoute-le, maison d'Israël! et maison du roi, sois-y attentive! car pour vous il s'agit du jugement; car vous fûtes un filet à Mitspa, et une toile tendue sur le Thabor.
2 Waasi husimama sana katika mauaji, lakini nitawaadhibu wote.
Ils accumulent les sacrifices coupables; mais moi [j'accumulerai] les châtiments sur eux tous.
3 Najua Efraimu, na Israeli hajajificha kwangu. Efraimu, sasa umekuwa kama kahaba; Israeli ni unajisi.
Je connais Éphraïm, et Israël ne m'est point caché; car maintenant tu te prostitues, Éphraïm, et Israël se souille.
4 Matendo yao hayawataruhusu kumgeukia Mungu, maana mawazo ya uzinzi yako ndani yao, na hawatamjua Bwana.
Ils ne font point leur œuvre de revenir à leur Dieu, car l'esprit d'impudicité est en eux, et de l'Éternel ils n'ont nulle connaissance.
5 Kiburi cha Israeli kinawashuhudia; Kwa hiyo Israeli na Efraimu watajikwaa kwa hatia zao; na Yuda pia wataanguka pamoja nao.
Ainsi l'orgueil d'Israël s'exprime sur son visage, et Israël et Éphraïm tomberont par l'effet de leur péché; avec eux tombera aussi Juda.
6 Watakwenda pamoja na kondoo zao na ng'ombe zao kumtafuta Bwana, lakini hawatamuona, kwa kuwa amejiondoa kutoka kwao.
Avec leurs brebis et leurs taureaux ils viendront chercher l'Éternel et ne le trouveront pas; Il se dérobe à eux.
7 Walikuwa wasio waaminifu kwa Bwana, kwa kuwa wamezaa watoto haramu. Sasa sherehe mpya za mwezi zitawaangamiza na mashamba yao.
A l'Éternel ils furent infidèles; car ils donnèrent naissance à des enfants bâtards; maintenant il ne faudra qu'une nouvelle lune pour les dévorer, eux et leurs possessions.
8 Piga tarumbeta huko Gibea, na tarumbeta huko Rama. Sauti ya kilio cha vita huko Beth Aveni 'Tutakufuata, Benyamini!'
Sonnez de la trompette en Guibha, et du clairon à Rama! pousse des cris, Bethaven! on est à ta poursuite, Benjamin!
9 Efraimu itakuwa ukiwa siku ya adhabu. Miongoni mwa makabila ya Israeli nimetangaza habari itakayotokea.
Éphraïm sera un désert au jour du châtiment; parmi les tribus d'Israël j'annonce une chose certaine.
10 Viongozi wa Yuda ni kama wale wanaondoao jiwe la mipaka. Nami nitamwaga ghadhabu yangu juu yao kama maji.
Les princes de Juda sont comme ceux qui déplacent les bornes; sur eux je verserai comme les eaux ma colère.
11 Efraimu ameangamizwa; ameangamizwa kwa hukumu, kwa sababu ametembea kwa hiari kufuata sanamu.
Éphraïm est accablé, écrasé par le jugement, car il se plaît à suivre la voie qu'il se trace.
12 Kwa hiyo nitakuwa kama nondo kwa Efraimu, na kama uozo kwa nyumba ya Yuda.
Et je suis comme une teigne pour Éphraïm, comme une carie pour la maison de Juda.
13 Efraimu alipoona ugonjwa wake, Yuda akaona jeraha lake; Efraimu akaenda Ashuru; Yuda akatuma wajumbe kwa mfalme mkuu. Lakini hakuweza kuwaponya watu au kuponya jeraha lako.
Et Éphraïm voit sa maladie, et Juda sa blessure, et Éphraïm se rend auprès d'Assur, et députe vers un roi qui le venge; mais il ne pourra vous guérir, ni enlever votre plaie.
14 Kwa hiyo nitakuwa kama simba kwa Efraimu, na kama simba kwa nyumba ya Yuda. Mimi, naam mimi, nitapotea na kwenda mbali; Nitawachukua, na hakutakuwa na mtu wa kuwaokoa.
Car je suis comme un lion pour Éphraïm, et comme un jeune lion pour la maison de Juda; moi, moi je déchire, puis je m'en vais, j'emporte, et personne qui sauve.
15 Nitakwenda na kurudi mahali pangu, mpaka watambue hatia yao na kutafuta uso wangu, hata wakanitafute kwa bidii katika dhiki yao.
Je m'en vais et retourne à ma demeure, jusqu'à ce qu'ils se reconnaissent et cherchent ma face; dans leur angoisse ils voudront me trouver.