< Hosea 5 >

1 Sikilizeni haya, makuhani! kuweni makini, nyumba ya Israeli! Sikilizeni, nyumba ya mfalme! Kwa maana hukumu itakuja juu yenu nyote. Mmekuwa mtego huko Mizpa na wavu uliosambazwa juu ya Tabori.
Hear these things, you priests; and attend, O house of Israel; and listen, O house of the king; for the controversy is with you, because you have been a snare in Scopia, and as a net spread on Itabyrium,
2 Waasi husimama sana katika mauaji, lakini nitawaadhibu wote.
which they that hunt the prey have fixed: but I will correct you.
3 Najua Efraimu, na Israeli hajajificha kwangu. Efraimu, sasa umekuwa kama kahaba; Israeli ni unajisi.
I know Ephraim, and Israel is not far from me: for now Ephraim has gone grievously a-whoring, Israel is defiled.
4 Matendo yao hayawataruhusu kumgeukia Mungu, maana mawazo ya uzinzi yako ndani yao, na hawatamjua Bwana.
They have not framed their counsels to return to their God, for the spirit of fornication is in them, and they have not known the Lord.
5 Kiburi cha Israeli kinawashuhudia; Kwa hiyo Israeli na Efraimu watajikwaa kwa hatia zao; na Yuda pia wataanguka pamoja nao.
And the pride of Israel shall be brought low before his face; and Israel and Ephraim shall fall in their iniquities; and Judas also shall fall with them.
6 Watakwenda pamoja na kondoo zao na ng'ombe zao kumtafuta Bwana, lakini hawatamuona, kwa kuwa amejiondoa kutoka kwao.
They shall go with sheep and calves diligently to seek the Lord; but they shall not find him, for he has withdrawn himself from them.
7 Walikuwa wasio waaminifu kwa Bwana, kwa kuwa wamezaa watoto haramu. Sasa sherehe mpya za mwezi zitawaangamiza na mashamba yao.
For they have forsaken the Lord; for strange children have been born to them: now shall the cankerworm devour them and their heritages.
8 Piga tarumbeta huko Gibea, na tarumbeta huko Rama. Sauti ya kilio cha vita huko Beth Aveni 'Tutakufuata, Benyamini!'
Blow you the trumpet on the hills, sound aloud on the heights: proclaim in the house of On, Benjamin is amazed.
9 Efraimu itakuwa ukiwa siku ya adhabu. Miongoni mwa makabila ya Israeli nimetangaza habari itakayotokea.
Ephraim has come to nothing in the days of reproof: in the tribes of Israel I have shown faithful [dealings].
10 Viongozi wa Yuda ni kama wale wanaondoao jiwe la mipaka. Nami nitamwaga ghadhabu yangu juu yao kama maji.
The princes of Juda became as they that removed the bounds: I will pour out upon them my fury as water.
11 Efraimu ameangamizwa; ameangamizwa kwa hukumu, kwa sababu ametembea kwa hiari kufuata sanamu.
Ephraim altogether prevailed against his adversary, he trod judgment under foot, for he began to go after vanities.
12 Kwa hiyo nitakuwa kama nondo kwa Efraimu, na kama uozo kwa nyumba ya Yuda.
Therefore I [will be] as consternation to Ephraim, and as a goad to the house of Juda.
13 Efraimu alipoona ugonjwa wake, Yuda akaona jeraha lake; Efraimu akaenda Ashuru; Yuda akatuma wajumbe kwa mfalme mkuu. Lakini hakuweza kuwaponya watu au kuponya jeraha lako.
And Ephraim saw his disease, and Judas his pain; then Ephraim went to the Assyrians, and sent ambassadors to king Jarim: but he could not heal you, and your pain shall in nowise cease from you.
14 Kwa hiyo nitakuwa kama simba kwa Efraimu, na kama simba kwa nyumba ya Yuda. Mimi, naam mimi, nitapotea na kwenda mbali; Nitawachukua, na hakutakuwa na mtu wa kuwaokoa.
Therefore I am as a panther to Ephraim, and as a lion to the house of Juda: and I will tear, and go away; and I will take, and there shall be none to deliver.
15 Nitakwenda na kurudi mahali pangu, mpaka watambue hatia yao na kutafuta uso wangu, hata wakanitafute kwa bidii katika dhiki yao.
I will go and return to my place, until they are brought to nothing, and [then] shall they seek my face.

< Hosea 5 >