< Hosea 5 >
1 Sikilizeni haya, makuhani! kuweni makini, nyumba ya Israeli! Sikilizeni, nyumba ya mfalme! Kwa maana hukumu itakuja juu yenu nyote. Mmekuwa mtego huko Mizpa na wavu uliosambazwa juu ya Tabori.
Hear ye this, O priests, and hearken, O ye house of Israel, and give ear, O house of the king: for there is a judgment against you, because you have been a snare to them whom you should have watched over, and a net spread upon Thabor.
2 Waasi husimama sana katika mauaji, lakini nitawaadhibu wote.
And you have turned aside victims into the depth: and I am, the teacher of them all.
3 Najua Efraimu, na Israeli hajajificha kwangu. Efraimu, sasa umekuwa kama kahaba; Israeli ni unajisi.
I know Ephraim, and Israel is not hid from me: for now Ephraim hath committed fornication, Israel is defiled.
4 Matendo yao hayawataruhusu kumgeukia Mungu, maana mawazo ya uzinzi yako ndani yao, na hawatamjua Bwana.
They will not set their thoughts to return to their God: for the spirit of fornication is in the midst of them, and they have not known the Lord.
5 Kiburi cha Israeli kinawashuhudia; Kwa hiyo Israeli na Efraimu watajikwaa kwa hatia zao; na Yuda pia wataanguka pamoja nao.
And the pride of Israel shall answer in his face: and Israel and Ephraim shall fall in their iniquity, Juda also shall fall with them.
6 Watakwenda pamoja na kondoo zao na ng'ombe zao kumtafuta Bwana, lakini hawatamuona, kwa kuwa amejiondoa kutoka kwao.
With their flocks, and with their herds, they shall go to seek the Lord, and shall not find him: he is withdrawn from them.
7 Walikuwa wasio waaminifu kwa Bwana, kwa kuwa wamezaa watoto haramu. Sasa sherehe mpya za mwezi zitawaangamiza na mashamba yao.
They have transgressed against the Lord, for they have begotten children that are strangers: now shall a month devour them with their portions.
8 Piga tarumbeta huko Gibea, na tarumbeta huko Rama. Sauti ya kilio cha vita huko Beth Aveni 'Tutakufuata, Benyamini!'
Blow ye the cornet in Gabaa, the trumpet in Rama: howl ye in Bethaven, behind thy back, O Benjamin.
9 Efraimu itakuwa ukiwa siku ya adhabu. Miongoni mwa makabila ya Israeli nimetangaza habari itakayotokea.
Ephraim shall be in desolation in the day of rebuke: among the tribes of Israel I have shewn that which shall surely be.
10 Viongozi wa Yuda ni kama wale wanaondoao jiwe la mipaka. Nami nitamwaga ghadhabu yangu juu yao kama maji.
The princes of Juda are become as they that take up the bound: I will pour out my wrath upon them like water.
11 Efraimu ameangamizwa; ameangamizwa kwa hukumu, kwa sababu ametembea kwa hiari kufuata sanamu.
Ephraim is under oppression, and broken in judgment: because he began to go after filthiness.
12 Kwa hiyo nitakuwa kama nondo kwa Efraimu, na kama uozo kwa nyumba ya Yuda.
And I will be like a moth to Ephraim: and like rottenness to the house of Juda.
13 Efraimu alipoona ugonjwa wake, Yuda akaona jeraha lake; Efraimu akaenda Ashuru; Yuda akatuma wajumbe kwa mfalme mkuu. Lakini hakuweza kuwaponya watu au kuponya jeraha lako.
And Ephraim saw his sickness, and Juda his band: and Ephraim went to the Assyrian, and sent to the avenging king: and he shall not be able to heal you, neither shall he be able to take off the band from you.
14 Kwa hiyo nitakuwa kama simba kwa Efraimu, na kama simba kwa nyumba ya Yuda. Mimi, naam mimi, nitapotea na kwenda mbali; Nitawachukua, na hakutakuwa na mtu wa kuwaokoa.
For I will be like a lioness to Ephraim, and like a lion’s whelp to the house of Juda: I, I will catch, and go: I will take away, and there is none that can rescue.
15 Nitakwenda na kurudi mahali pangu, mpaka watambue hatia yao na kutafuta uso wangu, hata wakanitafute kwa bidii katika dhiki yao.
I will go and return to my place: until you are consumed, and seek my face.