< Hosea 4 >

1 Sikilizeni neno la Bwana, enyi watu wa Israeli. Bwana ana mashtaka dhidi ya wenyeji wa nchi, kwa sababu hakuna ukweli au uaminifu wa agano, hakuna ujuzi wa Mungu katika nchi.
“Hear a word of YHWH, sons of Israel, For a strife [is] to YHWH with inhabitants of the land, For there is no truth, nor kindness, Nor knowledge of God in the land;
2 Kuna laana, uongo, mauaji, wizi na uzinzi. Watu wamevunja mipaka yote, na damu inakuja baada ya damu.
Swearing, and lying, and murdering, And stealing, and committing adultery—have increased, And blood has touched against blood.
3 Kwa hiyo nchi inakauka, na kila mtu aliyeishi ndani yake anaangamia; wanyama katika mashamba na ndege angani, hata samaki katika bahari, wanaondolewa.
Therefore the land mourns, And every dweller is weak in it, With the beast of the field, And with the bird of the heavens, And the fishes of the sea—they are removed.
4 Lakini usiruhusu mtu yeyote kuleta mashtaka; msiruhusu mtu yeyote ahukumu mtu mwingine. Kwa maana ninyi ndio makuhani, ninaowashtaki.
Only, let no one strive, nor reprove a man, And your people [are] as those striving with a priest.
5 Ninyi makuhani mtajikwaa wakati wa mchana; manabii pia watajikwaa pamoja nanyi usiku, nami nitamwangamiza mama yako.
And you have stumbled in the day, And a prophet has also stumbled with you in the night, And I have cut off your mother.
6 Watu wangu wanaharibiwa kwa sababu ya ukosefu wa maarifa. Kwa sababu makuhani wamekataa maarifa, nami nitawakataa msiwe makuhani kwangu. Kwa sababu umesahau sheria yangu, ingawa mimi ni Mungu wako, nami pia nitasahau watoto wako.
My people have been cut off for lack of knowledge, Because you have rejected knowledge, I reject you from being priest to Me, And you forget the Law of your God—I forget your sons, I also!
7 Makuhani wengi waliongezeka, zaidi walifanya dhambi dhidi yangu. Walibadilisha heshima zao kwa aibu.
According to their abundance so they sinned against Me, I change their glory into shame.
8 Wanajilisha dhambi ya watu wangu; wao ni wenye tamaa zaidi ya uovu wao.
The sin of My people they eat, And to their iniquity lift up their soul.
9 Itakuwa sawa kwa watu kama kwa makuhani: nitawaadhibu wote kwa matendo yao; Nitawalipa kwa matendo yao.
And it has been, like people, like priest, And I have charged on it its ways, And its habitual doings I return to it.
10 Watakula lakini hawatashiba; watafanya uzinzi lakini hawataongezeka, kwa sababu wamekwenda mbali na Bwana.
And they have eaten, and are not satisfied, They have gone whoring, and do not increase, For they have left off taking heed to YHWH.
11 Wanapenda uasherati, divai, na divai mpya, ambayo imechukua uelewa wao.
Whoredom, and wine, and new wine, take the heart,
12 Watu wangu hutaka shauri kwa sanamu zao za mbao, na fimbo zao za kutembelea huwapa unabii. Kwa maana mawazo ya uasherati yamewadanganya, na wamefanya kama makahaba badala ya kuwa mwaminifu kwa Mungu wao.
My people at its staff asks and its rod declares to it, For a spirit of whoredoms has caused to err, And they go whoring from under their God.
13 Wanatoa sadaka juu ya milima na kuteketeza uvumba kwenye milima, chini ya mialoni, milibua na miela, kwa sababu kivuli ni nzuri. Basi binti zenu hufanya uasherati, na binti zenu wanazini.
On tops of the mountains they sacrifice, And on the hills they make incense, Under oak, and poplar, and terebinth, For good [is] its shade.
14 Mimi siwaadhibu binti zako wakati wanachagua kutenda uasherati, wala binti zako wakati wazini. Kwa maana wanaume pia wanajitoa kwa makahaba, na hutoa dhabihu ili waweze kufanya vitendo vya uasherati na makahaba. Hivyo watu wasiofahamu wataangamizwa.
Therefore your daughters commit whoredom, And your spouses commit adultery, I do not see after your daughters when they commit whoredom, And after your spouses when they commit adultery, For they with the harlots are separated, And with the whores they sacrifice, A people that does not understand kicks.
15 Ingawa wewe, Israeli, umefanya uzinzi, lakini Yuda asiwe na hatia. Ninyi msiende Gilgali; msiende hadi Beth Aven. Wala msiape, “Aishivyo Bwana.”
Though you [are] a harlot, O Israel, Do not let Judah become guilty, And do not come to Gilgal, nor go up to Beth-Aven, Nor swear, YHWH lives.
16 Kwa maana Israeli amefanya ukaidi, kama ndama mkaidi. Je! Bwana anaweza kuwaleta kwenye malisho kama kondoo mahali penye nafasi?
For Israel has turned aside as a stubborn heifer, Now YHWH feeds them as a lamb in a large place.
17 Efraimu alijiunga na sanamu; mwache peke yake.
Ephraim is joined to idols, leave him alone.
18 Hata wakati kileo chao kimeondoka wakaendelea kufanya uzinzi; watawala wake hupenda sana aibu yao.
Sour [is] their drink, They have gone whoring diligently, Her protectors have thoroughly loved shame.
19 Upepo utamfunga kwa mabawa yake; nao wataona aibu kwa sababu ya dhabihu zao.
Wind has distressed her with its wings, And they are ashamed of their sacrifices!”

< Hosea 4 >