< Hosea 3 >

1 Bwana akaniambia, “Nenda tena, mpendeni mwanamke, aliyependwa na mumewe; lakini ni mzinzi. Mpende kama mimi, Bwana, ninavyowapenda watu wa Israeli, ingawa wanaigeukia miungu mingine na kupenda mikate ya zabibu.”
And YHWH says to me: “Again, go, love a woman, loved of a friend, and an adulteress, like the loved of YHWH, the sons of Israel, and they are turning to other gods, and are lovers of grape-cakes.”
2 Kwa hiyo nimemnunulia mwenyewe kwa vipande kumi na tano vya fedha na homeri na letheki ya shayiri.
And I buy her for myself for fifteen pieces of silver, and a homer and a lethech of barley;
3 Nilimwambia, “Lazima uishi pamoja nami siku nyingi. Huwezi kuwa kahaba au kuwa na mtu mwingine yeyote. Kwa njia hiyo hiyo, nitakuwa pamoja nanyi.”
and I say to her, “You remain many days for Me, you do not go whoring, nor become anyone’s; and I also [am] for you.”
4 Kwa maana wana wa Israeli wataishi kwa siku nyingi bila mfalme, mtu mkuu, dhabihu, nguzo ya mawe, efodi au sanamu za nyumbani.
For the sons of Israel remain without a king for many days, and there is no prince, and there is no sacrifice, and there is no standing pillar, and there is no ephod and teraphim.
5 Baadaye watu wa Israeli watarudi na kumtafuta Bwana Mungu wao na Daudi mfalme wao. Na katika siku za mwisho, watakuja wakitetemeka mbele za Bwana na wema wake.
Afterward the sons of Israel have turned back, and sought their God YHWH, and David their king, and have hurried to YHWH, and to His goodness, in the latter end of the days.

< Hosea 3 >