< Hosea 13 >
1 Efraimu alipozungumza, kulikuwa na tetemeko. Alijikuza katika Israeli, lakini akawa na hatia kwa sababu ya ibada ya Baali, naye akafa.
When Ephraim spoke, there was trembling, he exalted himself in Israel; but when he became guilty through Baal, he died.
2 Sasa wanafanya dhambi zaidi na zaidi. Wanatengeneza sanamu za chuma kutoka kwenye fedha zao, sanamu kwa kadiri ya ufanisi wao, zote ni kazi ya mafundi. Watu wanasema juu yao, 'Watu hawa watoao dhabihu na kumbusu ndama.'
And now they sin more and more, and have made them molten images of their silver, according to their own understanding, even idols, all of them the work of the craftsmen; of them they say: 'They that sacrifice men kiss calves.'
3 Kwa hiyo watakuwa kama mawingu ya asubuhi, kama umande unaoondoka mapema, kama makapi yanayotokana na upepo kutoka kwenye sakafu, na kama moshi utokao kwenye bomba.
Therefore they shall be as the morning cloud, and as the dew that early passeth away, as the chaff that is driven with the wind out of the threshing-floor, and as the smoke out of the window.
4 Lakini mimi ndimi Bwana, Mungu weko, tangu nchi ya Misri. Hutamjua Mungu mwingine bali mimi; wala zaidi yangu, hakuna mkombozi mwingine.
Yet I am the LORD thy God from the land of Egypt; and thou knowest no God but Me, and beside Me there is no saviour.
5 Nilikujua jangwani, katika nchi yenye kame.
I did know thee in the wilderness, in the land of great drought.
6 Wakati ulipokuwa na malisho, ulishiba; na wakati uliposhiba, moyo wako ukainuliwa. Kwa sababu hiyo umenisahau.
When they were fed, they became full, they were filled, and their heart was exalted; therefore have they forgotten Me.
7 Nitakuwa kama simba; kama chui nitaangalia kando ya njia.
Therefore am I become unto them as a lion; as a leopard will I watch by the way;
8 Nitawaangamiza kama dubu aliyenyang'anywa watoto wake. Nami nitararua vifua vyao, na huko nitawaangamiza kama simba, kama vile mnyama wa mwitu atakayerarua vipande vipande.
I will meet them as a bear that is bereaved of her whelps, and will rend the enclosure of their heart; and there will I devour them like a lioness; the wild beast shall tear them.
9 Nitawaangamiza, Israeli; nani atakayekusaidia?
It is thy destruction, O Israel, that thou art against Me, against thy help.
10 Mfalme wako yuko wapi, ili akuokoe katika miji yako yote? Wako wapi wakuu, ambao kwao umeniambia hivi, 'Nipe mfalme na wakuu'?
Ho, now, thy king, that he may save thee in all thy cities! and thy judges, of whom thou saidst: 'Give me a king and princes!'
11 Nimekupa mfalme kwa hasira yangu, nikamchukua kwa ghadhabu yangu.
I give thee a king in Mine anger, and take him away in My wrath.
12 Uovu wa Efraimu umehifadhiwa; hatia yake imehifadhiwa.
The iniquity of Ephraim is bound up; his sin is laid up in store.
13 Atakuwa na uchungu wa kujifungua, lakini ni mwana mjinga, kwa maana wakati wa kuzaliwa, hatatoka tumboni.
The throes of a travailing woman shall come upon him; he is an unwise son; for it is time he should not tarry in the place of the breaking forth of children.
14 Je, nitawaokoa na mkono wa kaburi? Je, nitawaokoa na kifo? Ewe Mauti yako wapi mapigo yako? Ewe kaburi kuko wapi kuharibu kwako? Huruma itafichwa na macho yangu. (Sheol )
Shall I ransom them from the power of the nether-world? Shall I redeem them from death? Ho, thy plagues, O death! Ho, thy destruction, O nether-world! Repentance be hid from Mine eyes! (Sheol )
15 Ingawa Efraimu anafanikiwa kati ya ndugu zake, upepo wa mashariki utakuja; upepo wa Bwana utapiga kutoka jangwani. Kijito cha maji cha Efraimu kitauka, na kisima chake hakitakuwa na maji. Adui yake atapora ghala lake la kila kitu cha thamani.
For though he be fruitful among the reed-plants, an east wind shall come, the wind of the LORD coming up from the wilderness, and his spring shall become dry, and his fountain shall be dried up; he shall spoil the treasure of all precious vessels.
16 Samaria itakuwa na hatia, kwa sababu amemuasi dhidi ya Mungu wake. Wataanguka kwa upanga; watoto wao wadogo watavunjwa, na wanawake wao wajawazito watatambuliwa wazi.
Samaria shall bear her guilt, for she hath rebelled against her God; they shall fall by the sword; their infants shall be dashed in pieces, and their women with child shall be ripped up.