< Hosea 11 >
1 “Wakati Israeli alikuwa kijana nilimpenda, na nikamwita mtoto wangu kutoka Misri.
If [was] a youth Israel and I loved him and from Egypt I summoned son my.
2 Kwa kadiri waliyoitwa, ndivyo walivyoondoka kwangu. Wakawafanyia dhabihu Baali, wakatafuta uvumba kwa sanamu.
They summoned them so they went from before them to the Baals they sacrificed and to the idols they made smoke!
3 Lakini mimi ndio niliyemfundisha Efraimu kutembea. Ndiye niliyewainua kwa silaha zao, lakini hawakujua kwamba niliwajali.
And I I taught to walk Ephraim he took them on arms his and not they knew that I had healed them.
4 Niliwaongoza kwa kamba za ubinadamu, na mafungo ya upendo. Mimi nilikuwa kama mtu aliyepunguza jozi juu ya taya zao, na nikainama na kuwalisha.
With cords of humankind I drew them with ropes of love and I was to them like [those who] lift a yoke on jaws their and I incline to him I feed [him].
5 Je, hawatarudi nchi ya Misri? Je, Ashuru haitatawala juu yao kwa sababu wanakataa kurudi kwangu?
Not he will return to [the] land of Egypt and Assyria it [will be] king his for they have refused to repent.
6 Upanga utaanguka juu ya miji yao na kuharibu makomeo ya milango yao; itawaangamiza kwa sababu ya mipango yao wenyewe.
And it will whirl a sword in cities his and it will put an end to bars his and it will devour [them] from schemes their.
7 Watu wangu wameamua kuniacha. Ingawa wanaita kwa Aliye Juu, hakuna mtu atawasaidia.
And people my [is] hung up to apostasy my and to a height they call on him together not he will exalt [them].
8 Ninawezaje kukuacha, Efraimu? Ninawezaje kukupeleka, Israeli? Ninawezaje kukufanya kama Adma? Ninawezaje kukufanya kama Seboimu? Moyo wangu umebadilika ndani yangu; huruma zangu zote zimeongezeka.
How? will I give up you O Ephraim will I deliver up? you O Israel how? will I make you like Admah will I make? you like Zeboiim it has been changed on me heart my together they have grown warm compassions my.
9 Sitafanya hasira yangu kali; Mimi sitawaangamiza Efraimu tena. Kwa maana mimi ni Mungu, wala si mtu; Mimi ni Mtakatifu kati yenu, nami sitakuja katika ghadhabu.
Not I will carry out [the] burning of anger my not I will repeat to destroy Ephraim for [am] God I and not a human in midst your [the] holy [one] and not I will come in rage.
10 Watanifuata, Bwana. Nitanguruma kama simba. Nami nitaomboleza, na watu watakuja wakitetemeka kutoka magharibi.
After Yahweh they will walk like a lion he will roar if he he will roar and they may tremble children from [the] west.
11 Watakuja wakitetemeka kama ndege kutoka Misri, kama njiwa kutoka nchi ya Ashuru. Nitawafanya wapate kuishi katika nyumba zao.” Hii ndiyo tamko la Bwana.
They will tremble like a bird from Egypt and like a dove from [the] land of Assyria and I will cause to dwell them at houses their [the] utterance of Yahweh.
12 Efraimu ananizunguka kwa maneno ya uongo, na nyumba ya Israeli kwa udanganyifu. Lakini Yuda bado anaendelea nami, Mungu, na ni mwaminifu kwangu, Mtakatifu.
They have surrounded me with lying Ephraim and with deceit [the] house of Israel and Judah still it has roamed with God and with [the] holy [one] faithful.