< Hosea 10 >

1 Israeli ni mzabibu mzuri ambao huzaa matunda yake. kwa kadiri matunda yake yanavyoongezeka vivyo hivyo anajenga madhabahu nyingi. Kwa kuwa nchi yake ilizalishwa zaidi, aliboresha nguzo zake.
Israel is a luxuriant vine that produces his fruit. As his fruit increased, the more altars he built. As his land produced more, he improved his pillars.
2 Moyo wao ni udanganyifu; sasa wanapaswa kubeba hatia yao. Bwana ataharibu madhabahu zao; ataharibu nguzo zao.
Their heart is deceitful; now they must bear their guilt. Yahweh will demolish their altars; he will destroy their pillars.
3 Kwa maana watasema, “Hatuna mfalme, kwa maana hatukumcha Bwana. Na mfalme-angeweza kutufanyia nini?”
For then they will say, “We have no king, for we did not fear Yahweh, and a king—what could he do for us?”
4 Wanasema maneno tupu na kufanya maagano kwa kuapa uongo. Kwa hivyo haki inakuja kama magugu yenye sumu katika mito ya shamba.
They speak empty words and make covenants by swearing falsely. So justice springs up like poisonous weeds in the furrows of a field.
5 Wakazi wa Samaria wataogopa kwa sababu ya ndama za Beth Aveni. Watu wake waliomboleza juu yao, kama walivyofanya wale makuhani wa sanamu ambao walikuwa wamefurahi juu yao na utukufu wao, lakini hawako tena.
The inhabitants of Samaria will be afraid because of the calves of Beth Aven. Its people mourned over them, as did those idolatrous priests who had rejoiced over them and their splendor, but they are no longer there.
6 Wao watachukuliwa kwenda Ashuru kama sadaka kwa mfalme mkuu. Efraimu atakuwa na aibu, na Israeli atakuwa na aibu kwa sanamu yake.
They will be carried to Assyria as a present for the great king. Ephraim will be disgraced, and Israel will be ashamed of its idol.
7 Mfalme wa Samaria ataangamizwa, kama chipu cha kuni juu ya uso wa maji.
Samaria's king will be destroyed, like a chip of wood on the surface of the water.
8 Sehemu za juu za uovu zitaharibiwa. Hii ndiyo dhambi ya Israeli! Miti na vichaka vitakua juu ya madhabahu zao. Watu wataiambia milima, “Tufunike sisi!” na kwa vilima, “Tuangukieni!”
The high places of wickedness will be destroyed. This is the sin of Israel! Thorns and thistles will grow over their altars. The people will say to the mountains, “Cover us!” and to the hills, “Fall on us!”
9 Ee Israeli, umetenda dhambi tangu siku za Gibea; huko umebaki. Je, vita vitawapata wana wa uovu huko Gibea?
“Israel, you have sinned since the days of Gibeah; there you have remained. Will not war overtake the sons of wrong in Gibeah?
10 Nitakapotaka, nitawaadhibu. Mataifa wataungana pamoja nao na kuwaweka katika vifungo kwa uovu wao mara mbili.
When I desire it, I will discipline them. The nations will gather together against them and put them in bonds for their double iniquity.
11 Efraimu ni ndama mwenye mafunzo ambayo anapenda kupura nafaka, hivyo nitaweka jozi juu ya shingo yake nzuri. Efraimu nitauweka jozi; Yuda ataimea; Yakobo atauvuta pigo kwa nafsi yake.
Ephraim is a trained heifer that loves to thresh the grain, so I will put a yoke on her fair neck. I will put a yoke on Ephraim; Judah will plow; Jacob will pull the harrow by himself.
12 Jifanyieni haki, vuneni matunda ya uaminifu wa agano. Chimbueni ardhi yenu isiyopandwa, kwa maana ni wakati wa kumtafuta Bwana, mpaka atakapokuja na kuinua haki juu yenu.
Sow righteousness for yourselves, and reap the fruit of covenant faithfulness. Break up your unplowed ground, for it is time to seek Yahweh, until he comes and rains righteousness on you.
13 Mmelima uovu; mmevuna udhalimu. Mmekula matunda ya udanganyifu kwa sababu uliamini katika mipango yako na katika askari wako wengi.
You have plowed wickedness; you reaped injustice. You have eaten the fruit of deception because you trusted in your plans and in your many soldiers.
14 Kwa hiyo mlipuko wa vita utafufuka kati ya watu wako, na miji yako yote yenye ngome itaharibiwa. Itakuwa kama Shalmani aliharibu Beth Arbeli siku ya vita, wakati mama alivunjika vipande vipande na watoto wake.
So a tumult of war will rise among your people, and all your fortified cities will be destroyed. It will be as Shalman destroyed Beth Arbel on a day of battle, when mothers were dashed to pieces with their children.
15 Kwa hiyo itakuwa kwako, Betheli, kwa sababu ya uovu wako mkubwa. Wakati wa mchana mfalme wa Israeli atakatwa kabisa.
So it will happen to you, Bethel, because of your great wickedness. At daybreak the king of Israel will be completely cut off.”

< Hosea 10 >