< Hosea 1 >

1 Hili ni neno la Bwana lililofika kwa Hosea mwana wa Beeri siku za Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda, na katika siku za Yeroboamu mwana wa Yoashi, mfalme wa Israeli.
This is the word of Yahweh that came to Hosea son of Beeri in the days of Uzziah, Jotham, Ahaz and Hezekiah, kings of Judah, and in the days of Jeroboam son of Joash, king of Israel.
2 Wakati Bwana alipozungumza kwanza kupitia Hosea, akamwambia, “Nenda ukajitwalie mke ambaye ni kahaba. Atakuwa na watoto ambao ni matokeo ya ukahaba wake. Kwa maana nchi inafanya uzinzi mkubwa kwa kumwacha Bwana.”
When Yahweh spoke at first through Hosea, he said to him, “Go, take for yourself a wife who is a prostitute. She will have children who are the result of her prostitution. For the land is committing great prostitution by forsaking Yahweh.”
3 Basi Hosea akaenda akamwoa Gomeri binti Diblaimu, naye akachukua mimba, akazaa mtoti mwanamume.
So Hosea went and married Gomer daughter of Diblaim, and she conceived and bore him a son.
4 Bwana akamwambia Hosea, Mwite jina lake Yezreeli. Kwa maana kwa muda mfupi nitaiadhibu nyumba ya Yehu kwa sababu ya kumwaga damu huko Yezreeli; nami nitamaliza ufalme wa nyumba ya Israeli.
Yahweh said to Hosea, “Call his name Jezreel. For in a little while I will punish the house of Jehu for the bloodshed at Jezreel, and I will put an end to the kingdom of the house of Israel.
5 Itatokea siku ile nitakapovunja upinde wa Israeli katika bonde la Yezreeli.
It will happen on the day that I break the bow of Israel in the Valley of Jezreel.”
6 Gomeri akachukua mimba tena akamzaa binti. Ndipo Bwana akamwambia Hosea, “Mwite jina lake Lo Ruhama; kwa maana sitawahurumia tena nyumba ya Israeli, nisije nikawasamehe kwa njia yoyote.
Gomer conceived again and bore a daughter. Then Yahweh said to Hosea, “Call her name Lo-Ruhamah, for I will no longer have mercy on the house of Israel, that I should forgive them at all.
7 Hata hivyo nitawahurumia nyumba ya Yuda, nami nitawaokoa mwenyewe, Bwana, Mungu wao. Sitawaokoa kwa upinde, upanga, vita, farasi, au wapanda farasi. '
Yet I will have mercy on the house of Judah, and I will save them by myself, Yahweh their God. I will not save them by bow, sword, battle, horses, or horsemen.”
8 Baada ya Gomeri kumwachisha Lo Ruhama, alipata mimba na kuzaa mtoto mwingine mwanamume.
Now after Gomer had weaned Lo-Ruhamah, she conceived and bore another son.
9 Ndipo Bwana akasema, “Mwite jina la Lo Ami; kwa kuwa ninyi si watu wangu, wala mimi si Mungu wenu.”
Then Yahweh said, “Call his name Lo-Ammi, for you are not my people, and I am not your God.
10 Hata hivyo idadi ya watu wa Israeli itakuwa kama mchanga wa bahari, ambayo haiwezi kupimwa au kuhesabiwa. Itakuwa pale ambapo waliambiwa, “Ninyi si watu wangu,” wataambiwa, “Ninyi ni watu wa Mungu aliye hai.”
Yet the number of the people of Israel will be like the sand of the seashore, which cannot be measured or counted. It will be that where it was said to them, 'You are not my people,' it will be said to them, 'You are people of the living God.'
11 Watu wa Yuda na watu wa Israeli watakusanyika pamoja. Wao wataweka kiongozi mmoja wao wenyewe, na watatoka kutoka nchi, kwa maana itakuwa siku ya Yezreeli kuu.
The people of Judah and the people of Israel will be gathered together. They will appoint one leader for themselves, and they will go up from the land, for great will be the day of Jezreel.

< Hosea 1 >