< Wahebrania 1 >
1 Nyakati zilizopita Mungu alizungumza na mababu zetu kupitia manabii mara nyingi na kwa njia nyingi.
God, having spoken to the fathers through the prophets in many parts and in various ways, in the past,
2 Lakini katika siku hizi tulizonazo, Mungu ameongea nasi kupitia Mwana, ambaye alimweka kuwa mrithi wa vitu vyote, na ambaye kupitia yeye pia aliumba ulimwengu. (aiōn )
has at the end of these days spoken to us by Son, whom He appointed heir of all things, through whom also He made the ages; (aiōn )
3 Mwanawe ni nuru ya utukufu wake, tabia pekee ya asili yake, na anayeendeleza vitu vyote kwa neno la nguvu zake. Baada ya kukamilisha utakaso wa dhambi, aliketi chini mkono wa kulia wa enzi huko juu.
who being the projection of His glory and the very image of His essence, and sustaining all things by the expression of His[S] own power, when He had by Himself provided purification for our sins He sat down on the highest Majesty's right,
4 Amekuwa bora kuliko malaika, kama vile jina alilolirithi lilivyo bora zaidi kuliko jina lao.
having become so much superior to the angels as He has inherited a more excellent name than they have.
5 Kwa maana ni kwa malaika gani aliwahi kusema, “Wewe ni mwanangu, leo nimekuwa baba yako?” Na tena, “Nitakuwa baba kwake, naye atakuwa mwana kwangu?”
For to which of the angels did He[F] ever say, “You are my Son, today I begot you,” and again, “I will be ‘Father’ to Him, and He will be ‘Son’ to me?”
6 Tena, wakati Mungu alipomleta mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, husema, “Malaika wote wa Mungu lazima wamwabudu.”
Again, when He introduces the Firstborn into the inhabited earth He says, “Let all God's angels worship Him[S].”
7 Kuhusu malaika asema, “Yeye ambaye hufanya malaika zake kuwa roho, na watumishi wake kuwa ndimi za moto.”
Further, about the angels He[F] says, “Who makes His angels winds, His servants flames of fire”;
8 Lakini kuhusu Mwana husema, “Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele. Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya haki. (aiōn )
while to the Son He says: “Your throne, O God, is forever and ever; ‘Scepter of Uprightness’ is the scepter of Your kingdom. (aiōn )
9 Umependa haki na kuchukia uvunjaji wa sheria, kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekupaka mafuta ya furaha kuliko wenzako.”
You have loved righteousness and hated lawlessness, therefore God, Your God, has anointed You with the oil of exultation beyond Your companions.”
10 Hapo mwanzo, Bwana, uliweka msingi wa dunia. Mbingu ni kazi za mikono yako.
Also: “You, Lord, in the beginning, laid the foundation of the earth, and the heavens are works of Your hands;
11 Zitatoweka, lakini wewe utaendelea. Zote zitachakaa kama vazi.
they will perish but You continue on —they will all grow old like a garment;
12 Utazikunjakunja kama koti, nazo zitabadilika kama vazi. Lakini wewe ni yuleyule, na miaka yako haitakoma.”
You will roll them up like a cloak and they will be changed, while You stay the same and Your years will never end.”
13 Lakini ni kwa malaika yupi Mungu alisema wakati wowote, “Keti mkono wangu wa kulia mpaka nitakapowafanya adui zako kuwa kiti cha miguu yako”?
On the other hand, to which of the angels did He ever say, “Sit on my right until I place your enemies as a stool under your feet”?
14 Je, malaika wote siyo roho zilizotumwa kuwahudumia na kuwatunza wale watakaourithi wokovu?
Are they not all ministering spirits being sent to serve those who are going to inherit salvation?