< Wahebrania 8 >

1 Sasa jambo ambalo tunasema ni hili: tunaye kuhani mkuu aliyekaa chini katika mkono wa kulia wa kiti cha enzi Mbinguni.
To sum up what I have been saying: — Such is the High Priest that we have, one who ‘has taken his seat at the right hand’ of the throne of God’s Majesty in Heaven,
2 Yeye ni mtumishi katika mahali patakatifu, hema la kweli ambalo Bwana ameliweka, siyo mtu yeyote wa kufa.
where he ministers in the Sanctuary, in that true Tabernacle set up by the Lord and not by man.
3 Kwa maana kila kuhani mkuu huwekwa kutoa zawadi na dhabihu; kwa hiyo ni muhimu kuwa na kitu cha kutoa.
Every High Priest is appointed for the purpose of offering gifts and sacrifices to God; it follows, therefore, that this High Priest must have some offering to make.
4 Sasa kama Kristo alikuwa juu ya nchi, yeye asingekuwa kuhani zaidi ya hapo. Kwa kuwa walikuwa tayari wale waliotoa vipawa kulingana na sheria.
If he were, however, still upon earth, he would not even be a priest, since there are already priests who offer the gifts as the Law directs.
5 Walihudumu kitu ambacho kilikuwa nakala na kivuli cha vitu vya mbinguni, sawa kama Musa alipoonywa na Mungu wakati alipotaka kujenga hema. “Ona,” Mungu akasema, “kwamba tengeneza kila kitu kulingana na muundo ulioonyeshwa juu ya mlima”.
(These priests, it is true, are engaged in a service which is only a copy and shadow of the heavenly realities, as is shown by the directions given to Moses when he was about to construct the Tabernacle. ‘Look to it,’ are the words, ‘that thou make every part in accordance with the pattern shown thee on the mountain.’)
6 Lakini sasa Kristo amepokea huduma bora zaidi kwa sababu yeye pia ni mpatanishi wa agano zuri, ambalo limekwisha kuimarishwa kwa ahadi nzuri.
But Jesus, as we see, has obtained a ministry as far excelling theirs, as the Covenant of which he is the intermediary, based, as it is, on better promises, excels the former Covenant.
7 Hivyo kama agano la kwanza lisingekuwa na makosa, ndipo hakungekuwa na haja kutafuta agano la pili.
If that first Covenant had been faultless, there would have been no occasion for a second.
8 Kwa kuwa wakati Mungu alipogundua makosa kwa watu alisema, “Tazama, siku zinakuja, 'asema Bwana, 'wakati nitakapotengeneza agano jipya pamoja na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda.
But, finding fault with the people, God says — ‘“Behold, a time is coming,” says the Lord, “When I will ratify a new Covenant with the People of Israel and with the People of Judah —
9 Halitakuwa kama agano nililofanya pamoja na baba zao siku ambayo niliwachukua kwa mkono kuwaongoza kutoka nchi ya Misri. Kwa kuwa hawakuendelea katika agano langu, nami sikuwajali tena,' asema Bwana.
Not such a Covenant as I made with their ancestors On the day when I took them by the hand to lead them out of the land of Egypt. For they did not abide by their Covenant with me, And therefore I disregarded them,” says the Lord.
10 Kwa kuwa hili ndilo agano nitafanya kwa nyumba ya Israeli baada ya siku hizo,' asema Bwana. 'nitaweka sheria zangu mawazoni mwao, na nitaziandika mioyoni mwao. Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
“This is the Covenant that I will make with the People of Israel After those days,” says the Lord. “I will impress my laws on their minds, And will inscribe them on their hearts; And I will be their God, And they shall be my People.
11 Hawatafundishana kila mmoja na jirani yake, na kila mmoja na ndugu, yake, akisema, “Mjue Bwana,” hivyo wote watanijua mimi, kutoka mdogo hadi mkubwa wao.
There shall be no need for every man to instruct his fellow-citizen, Or for a man to say to his Brother ‘Learn to know the Lord’; For every one will know me, From the lowest to the highest.
12 Hivyo nitaonyesha rehema kwa matendo yao yasiyo ya haki, na sizitazikumbuka dhambi zao tena.”
For I will be merciful to their wrong-doings, And I will no longer remember their sins.”’
13 Kwa kusema “Mpya,” amelifanya agano la kwanza kuwa kuukuu. Na hilo ambalo amelitangaza kuwa kuukuu liko tayari kutoweka.
By speaking of a ‘new’ Covenant, God at once renders the former Covenant obsolete; and whatever becomes obsolete and loses its force is virtually annulled.

< Wahebrania 8 >