< Wahebrania 5 >
1 Kwani kila kuhani mkuu, aliyechaguliwa kutoka miongoni mwa watu, amechaguliwa kusimama badala yao katika vitu vinavyohusiana na Mungu, ili aweze kutoa kwa pamoja zawadi na dhabihu kwa ajili ya dhambi.
For every high priest, being taken from among people, is appointed for people in things pertaining to God, that he may offer both gifts and sacrifices for sins.
2 Anaweza kujishughulisha kwa upole na wajinga na wabishi kwa kuwa yeye mwenyewe pia amezungukwa na udhaifu.
The high priest can deal gently with those who are ignorant and going astray, because he himself is also surrounded with weakness.
3 Kwa sababu ya hili, ana wajibu wa kutoa sadaka kwa ajili ya dhambi zake kama afanyavyo kwa dhambi za watu.
Because of this, he must offer sacrifices for sins for the people, as well as for himself.
4 Na hakuna mtu achukuaye heshima hii kwa ajili yake mwenyewe, lakini badala yake, lazima aitwe na Mungu, kama alivyokuwa Haruni.
Nobody takes this honor on himself, but he is called by God, just like Aaron was.
5 Hata Kristo hakujipa heshimu mwenyewe kwa kujifanya mwenyewe kuwa kuhani mkuu. Badala yake, Mungu alisema kwake, “Wewe ni mwanangu, leo nimekuwa Baba yako.”
So also Messiah did not glorify himself to be made a high priest, but it was he who said to him, "You are my Son. Today I have become your Father."
6 Ni kama asemavyo pia sehemu nyingine, “Wewe ni kuhani milele baada ya mfumo wa Melkizedeki.” (aiōn )
As he says also in another place, "You are a priest forever, after the order of Melchizedek." (aiōn )
7 Wakati wa kipindi chake katika mwili, aliomba na kuombea, alimwomba Mungu kwa machozi, kwa yeye awezaye kumwokoa kutoka kwenye kifo. Kwa sababu ya unyenyekevu wake kwa Mungu, alisikiwa.
In the days of his flesh, he offered up prayers and petitions with loud cries and tears to him who was able to save him from death, and he was heard because of his reverence.
8 Ijapokuwa alikua mwana, alijifunza kutii kwa mambo yaliyomtesa.
Although he was a Son, he learned obedience by the things which he suffered.
9 Alikamilishwa na kwa njia hii alifanyika kwa kila mtu amwaminiye kuwa sababu ya wokovu wa milele, (aiōnios )
Having been made perfect, he became to all of those who obey him the author of everlasting salvation, (aiōnios )
10 kwa kutengwa na Mungu kama kuhani Mkuu baada ya zamu ya Melkizedeki.
named by God a high priest after the order of Melchizedek.
11 Tuna mengi ya kusema kuhusu Yesu, lakini ni vigumu kuwaelezea kwa kuwa ninyi ni wavivu wa kusikia.
About him we have many words to say, and hard to interpret, seeing you have become dull of hearing.
12 Ijapokuwa kwa kipindi hiki mlipaswa kuwa walimu, bado kuna umuhimu wa mtu kuwafundisha mafundisho ya awali ya kanuni za neno la Mungu. Mnahitaji maziwa na si chakula kigumu.
For when by reason of the time you ought to be teachers, you again need to have someone teach you the rudiments of the first principles of the oracles of God. You have come to need milk, not solid food.
13 Kwa kuwa yeyote anywaye maziwa tu hana uzoefu katika ujumbe wa haki, kwa kuwa bado ni mtoto.
For everyone who lives on milk is not experienced in the word of righteousness, for he is a baby.
14 Kwa upande mwingine, chakula kigumu ni cha watu wazima, wale ambao kwa sababu ya uzoefu wao katika kutofautisha haki na ubaya wamefundishwa kutambua jema na ovu.
But solid food is for those who are full grown, who by reason of use have their senses exercised to discern good and evil.