< Wahebrania 5 >
1 Kwani kila kuhani mkuu, aliyechaguliwa kutoka miongoni mwa watu, amechaguliwa kusimama badala yao katika vitu vinavyohusiana na Mungu, ili aweze kutoa kwa pamoja zawadi na dhabihu kwa ajili ya dhambi.
For every high priest taken from among men, is ordained for men in the things that appertain to God, that he may offer up gifts and sacrifices for sins:
2 Anaweza kujishughulisha kwa upole na wajinga na wabishi kwa kuwa yeye mwenyewe pia amezungukwa na udhaifu.
Who can have compassion on them that are ignorant and that err: because he himself also is compassed with infirmity.
3 Kwa sababu ya hili, ana wajibu wa kutoa sadaka kwa ajili ya dhambi zake kama afanyavyo kwa dhambi za watu.
And therefore he ought, as for the people, so also for himself, to offer for sins.
4 Na hakuna mtu achukuaye heshima hii kwa ajili yake mwenyewe, lakini badala yake, lazima aitwe na Mungu, kama alivyokuwa Haruni.
Neither doth any man take the honour to himself, but he that is called by God, as Aaron was.
5 Hata Kristo hakujipa heshimu mwenyewe kwa kujifanya mwenyewe kuwa kuhani mkuu. Badala yake, Mungu alisema kwake, “Wewe ni mwanangu, leo nimekuwa Baba yako.”
So Christ also did not glorify himself, that he might be made a high priest: but he that said unto him: Thou art my Son, this day have I begotten thee.
6 Ni kama asemavyo pia sehemu nyingine, “Wewe ni kuhani milele baada ya mfumo wa Melkizedeki.” (aiōn )
As he saith also in another place: Thou art a priest for ever, according to the order of Melchisedech. (aiōn )
7 Wakati wa kipindi chake katika mwili, aliomba na kuombea, alimwomba Mungu kwa machozi, kwa yeye awezaye kumwokoa kutoka kwenye kifo. Kwa sababu ya unyenyekevu wake kwa Mungu, alisikiwa.
Who in the days of his flesh, with a strong cry and tears, offering up prayers and supplications to him that was able to save him from death, was heard for his reverence.
8 Ijapokuwa alikua mwana, alijifunza kutii kwa mambo yaliyomtesa.
And whereas indeed he was the Son of God, he learned obedience by the things which he suffered:
9 Alikamilishwa na kwa njia hii alifanyika kwa kila mtu amwaminiye kuwa sababu ya wokovu wa milele, (aiōnios )
And being consummated, he became, to all that obey him, the cause of eternal salvation. (aiōnios )
10 kwa kutengwa na Mungu kama kuhani Mkuu baada ya zamu ya Melkizedeki.
Called by God a high priest according to the order of Melchisedech.
11 Tuna mengi ya kusema kuhusu Yesu, lakini ni vigumu kuwaelezea kwa kuwa ninyi ni wavivu wa kusikia.
Of whom we have much to say, and hard to be intelligibly uttered: because you are become weak to hear.
12 Ijapokuwa kwa kipindi hiki mlipaswa kuwa walimu, bado kuna umuhimu wa mtu kuwafundisha mafundisho ya awali ya kanuni za neno la Mungu. Mnahitaji maziwa na si chakula kigumu.
For whereas for the time you ought to be masters, you have need to be taught again what are the first elements of the words of God: and you are become such as have need of milk, and not of strong meat.
13 Kwa kuwa yeyote anywaye maziwa tu hana uzoefu katika ujumbe wa haki, kwa kuwa bado ni mtoto.
For every one that is a partaker of milk, is unskillful in the word of justice: for he is a little child.
14 Kwa upande mwingine, chakula kigumu ni cha watu wazima, wale ambao kwa sababu ya uzoefu wao katika kutofautisha haki na ubaya wamefundishwa kutambua jema na ovu.
But strong meat is for the perfect; for them who by custom have their senses exercised to the discerning of good and evil.