< Wahebrania 3 >

1 Kwa hiyo, ndugu watakatifu, washiriki wa wito wa mbinguni, mumfikiri Yesu, Mtume na Kuhani Mkuu wa ukiri wetu.
WHEREFORE, holy brethren, partakers of the heavenly calling, contemplate the apostle and high-priest whom ye confess, Jesus Christ;
2 Alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemteua, kama Musa alivyokuwa mwaminifu pia katika nyumba yote ya Mungu.
who was faithful to him who appointed him, as Moses also was in all his house.
3 Kwa kuwa Yesu amehesabiwa kuwa na heshima kubwa kuliko aliyokuwa nayo Musa, kwa sababu yule anayejenga nyumba anahesabiwa kuwa na heshima kubwa kuliko nyumba yenyewe.
For this personage hath been counted worthy of higher glory than Moses, inasmuch as he who built it, hath greater honour than the house.
4 Kwa kuwa kila nyumba hujengwa na mtu fulani, lakini yule anayejenga kila kitu ni Mungu.
For every house is built by some person; but he who is the architect of all things is God.
5 Hakika Musa alikuwa mwaminifu kama mtumishi katika nyumba yote ya Mungu, akitoa ushuhuda kuhusu mambo yatakayosemwa wakati ujao.
And Moses indeed was faithful in all that house of his as a servant, to bear testimony of the things which should be after spoken;
6 Lakini Kristo ni Mwana katika usimamizi wa nyumba ya Mungu. Sisi ni nyumba yake kama tutashikilia haraka katika kujiamini na fahari ya kujiamini.
but Christ as a son over his own house: whose house are we, if we hold firmly the confidence and glorying of hope stedfast unto the end.
7 Kwa hiyo, ni kama Roho Mtakatifu asemavyo, “Leo, kama utasikia sauti yake,
Wherefore, as the Holy Ghost saith, To day if ye will hear his voice,
8 Usiufanye moyo wako kuwa mgumu kama Waisraeli walivyofanya katika uasi, katika wakati wa kujaribiwa nyikani.
harden not your hearts, as in that bitter provocation, at the day of the temptation in the wilderness;
9 Huu ulikuwa wakati ambao baba zenu waliniasi kwa kunijaribu, na wakati, kwa miaka arobaini, waliona matendo yangu.
when your fathers tempted me, proved me, and saw my works during forty years.
10 Kwa hiyo sikufurahishwa na kizazi hicho. Nilisema, 'Wanapotea kila mara katika mioyo yao, na hawajui njia zangu.
Wherefore I was provoked against that generation, and said, They are always deluded in heart, and they have not known my ways:
11 Ni kama vile nilivyoapa katika hasira yangu: hawataiingia raha yangu.”
so I swore in my wrath that they shall not enter into my rest.
12 Muwe waangalifu, ndugu, ili kwamba usije ukawepo moyo mwovu wa kutokuamini kwa mmoja wenu, moyo ambao utakwenda mbali na Mungu aliye hai.
Take heed, brethren, that there be not in any one of you a wicked heart of infidelity, evident in departure from the living God:
13 Badala yake, mhamasishane kila siku kila mmoja na mwenzie, ili kila iitwapo leo mtamani, ili kwamba mmoja kati yenu asifanywe kuwa mgumu kwa udanganyifu wa dhambi.
but exhort one another daily, whilst to-day remains, that no one of you be hardened by the deceitfulness of sin.
14 Kwa maana tumekuwa washiriki wa Kristo ikiwa tutashikamana na uthabiti wetu kwa nguvu katika yeye kutoka mwanzo hadi mwisho.
For we are partakers with Christ, if we hold the beginning of our confidence firm unto the end;
15 Kuhusu hili imekwisha kusemwa, “Leo kama mtaisikiliza sauti yake, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu, kama Waisraeli walivyofanya wakati wa uasi.”
while it is said, To-day if ye will hear his voice, harden not your hearts as in the provocation.
16 Ni akina nani hao waliomsikia Mungu na kuasi? Hawakuwa wale wote ambao Musa alikuwa amewaongoza kutoka Misri?
For some, though they had heard, provoked him; yet not all who came out of Egypt by Moses.
17 Na kina nani ambao Mungu aliwakasirikia kwa miaka arobaini? Siyo pamoja na wale waliotenda dhambi, ambao miili yao iliyokufa ililala jangwani?
But against whom was he incensed forty years? Was it not against those who had sinned, whose corpses fell in the wilderness?
18 Ni akina nani aliowaapia Mungu kwamba hawataingia katika raha yake, kama siyo wale ambao hawakumtii yeye?
And to whom did he swear that they should not enter into his rest, but to those who did not believe?
19 Tunaona kwamba hawakuweza kuingia katika raha yake kwa sababu ya kutokuamini.
So we see that they could not enter in because of unbelief.

< Wahebrania 3 >