< Wahebrania 3 >

1 Kwa hiyo, ndugu watakatifu, washiriki wa wito wa mbinguni, mumfikiri Yesu, Mtume na Kuhani Mkuu wa ukiri wetu.
Wherefore, holy brethren, partakers of the heavenly calling, consider the apostle and high priest of our confession, Christ Jesus,
2 Alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemteua, kama Musa alivyokuwa mwaminifu pia katika nyumba yote ya Mungu.
who is faithful to him that appointed him, as Moses also was faithful in all his house.
3 Kwa kuwa Yesu amehesabiwa kuwa na heshima kubwa kuliko aliyokuwa nayo Musa, kwa sababu yule anayejenga nyumba anahesabiwa kuwa na heshima kubwa kuliko nyumba yenyewe.
For this man is counted worthy of more glory than Moses, inasmuch as he who has builded the house, has more honor than the house.
4 Kwa kuwa kila nyumba hujengwa na mtu fulani, lakini yule anayejenga kila kitu ni Mungu.
For every house is builded by some one; but he that built all things is God.
5 Hakika Musa alikuwa mwaminifu kama mtumishi katika nyumba yote ya Mungu, akitoa ushuhuda kuhusu mambo yatakayosemwa wakati ujao.
And Moses indeed was faithful in all his house as a servant, to bear testimony to those things which were to be spoken afterward;
6 Lakini Kristo ni Mwana katika usimamizi wa nyumba ya Mungu. Sisi ni nyumba yake kama tutashikilia haraka katika kujiamini na fahari ya kujiamini.
but Christ, as a Son over his own house; whose house we are, if we hold the confidence and the joy of our hope firm to the end.
7 Kwa hiyo, ni kama Roho Mtakatifu asemavyo, “Leo, kama utasikia sauti yake,
Wherefore, as the Holy Spirit says: To-day, if you will hear his voice,
8 Usiufanye moyo wako kuwa mgumu kama Waisraeli walivyofanya katika uasi, katika wakati wa kujaribiwa nyikani.
harden not your hearts, as in the bitter provocation, in the day of trial in the wilderness,
9 Huu ulikuwa wakati ambao baba zenu waliniasi kwa kunijaribu, na wakati, kwa miaka arobaini, waliona matendo yangu.
where your fathers tried me, proved me, and saw my works forty years.
10 Kwa hiyo sikufurahishwa na kizazi hicho. Nilisema, 'Wanapotea kila mara katika mioyo yao, na hawajui njia zangu.
Where fore, I was angry with that generation, and said, They do always err in their heart, and they have not known my ways:
11 Ni kama vile nilivyoapa katika hasira yangu: hawataiingia raha yangu.”
so that I swore in my anger, They shall not enter into my rest.
12 Muwe waangalifu, ndugu, ili kwamba usije ukawepo moyo mwovu wa kutokuamini kwa mmoja wenu, moyo ambao utakwenda mbali na Mungu aliye hai.
Take heed, brethren, lest there be in any of you an evil heart of unbelief in apostatizing from the living God.
13 Badala yake, mhamasishane kila siku kila mmoja na mwenzie, ili kila iitwapo leo mtamani, ili kwamba mmoja kati yenu asifanywe kuwa mgumu kwa udanganyifu wa dhambi.
But exhort one another daily, while it is called To-day, lest any of you be hardened by the deceitfulness of sin.
14 Kwa maana tumekuwa washiriki wa Kristo ikiwa tutashikamana na uthabiti wetu kwa nguvu katika yeye kutoka mwanzo hadi mwisho.
For we are partakers of the Christ, if we hold our begun confidence firm to the end;
15 Kuhusu hili imekwisha kusemwa, “Leo kama mtaisikiliza sauti yake, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu, kama Waisraeli walivyofanya wakati wa uasi.”
while it is said, To-day, if you will hear his voice, harden not your hearts, as in the bitter provocation.
16 Ni akina nani hao waliomsikia Mungu na kuasi? Hawakuwa wale wote ambao Musa alikuwa amewaongoza kutoka Misri?
For some, when they had heard, did bitterly provoke; yet, not all that came out of Egypt by Moses.
17 Na kina nani ambao Mungu aliwakasirikia kwa miaka arobaini? Siyo pamoja na wale waliotenda dhambi, ambao miili yao iliyokufa ililala jangwani?
But with whom was he angry forty years? Was it not with those who sinned, whose carcasses fell in the wilderness?
18 Ni akina nani aliowaapia Mungu kwamba hawataingia katika raha yake, kama siyo wale ambao hawakumtii yeye?
But to whom did he swear that they should not enter into his rest, but to those who believed not?
19 Tunaona kwamba hawakuweza kuingia katika raha yake kwa sababu ya kutokuamini.
And so we see that they could not enter in because of unbelief.

< Wahebrania 3 >