< Wahebrania 13 >

1 Basi upendo wa ndugu na uendelee.
Let brotherly love remain;
2 Msisahau kuwakaribisha wageni, maana kwa kufanya hivi, baadhi wamewakaribisha malaika pasipo kujua.
of the hospitality be not forgetful, for through this unawares certain did entertain messengers;
3 Kumbuka wote waliomo gerezani, kana kwamba mulikuwa nao kule pamoja nao, na kama miili yenu ilitendewa kama wao.
be mindful of those in bonds, as having been bound with them, of those maltreated, as also yourselves being in the body;
4 Basi ndoa na iheshimiwe na wote na basi kitanda cha ndoa kifanywe kuwa safi, kwa maana Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi.
honourable [is] the marriage in all, and the bed undefiled, and whoremongers and adulterers God shall judge.
5 Basi njia zenu za maisha ziwe huru katika upendo wa pesa. Muwe wanoridhika na vitu mulivyonavyo, kwani Mungu mwenyewe alisema, “Sitawaacha ninyi kamwe, wala kuwatelekeza ninyi.”
Without covetousness the behaviour, being content with the things present, for He hath said, 'No, I will not leave, no, nor forsake thee,'
6 Basi tulidhikeni ili tusema kwa ujasiri, “Bawa ni msaidizi wangu; Sitaogopa. Mwanadamu aweza kunifanya nini?”
so that we do boldly say, 'The Lord [is] to me a helper, and I will not fear what man shall do to me.'
7 Wafikirieni wale walio waongoza, wale waliongea neno la Mungu kwenu, na kumbukeni matokeo ya mienendo yao; igeni imani zao.
Be mindful of those leading you, who did speak to you the word of God, whose faith — considering the issue of the behaviour — be imitating,
8 Yesu Kristo ni yeye jana, leo, na ata milele. (aiōn g165)
Jesus Christ yesterday and to-day the same, and to the ages; (aiōn g165)
9 Usije ukaongozwa na mafundisho mbalimbali ya kigeni kwani ni vizuri kwamba moyo ujengwe kwa neema, na siyo kwa sheria kuhusu chakula hayo hayatawasaidia wale wanaoishi kwa hayo.
with teachings manifold and strange be not carried about, for [it is] good that by grace the heart be confirmed, not with meats, in which they who were occupied were not profited;
10 Tunayo madhabau ambayo wale wanaotumika ndani ya hekalu hawana haki ya kula.
we have an altar, of which to eat they have no authority who the tabernacle are serving,
11 Kwa kuwa damu za wanyama, zilizotolewa dhabihu kwa ajili ya dhambi, ililetwa na kuhani mkuu ndani ya sehemu takatifu, lakini miili yao ilichomwa nje ya kambi.
for of those beasts whose blood is brought for sin into the holy places through the chief priest — of these the bodies are burned without the camp.
12 Kwa hiyo Yesu naye aliteseka nje ya lango la mji, hili kwamba kuweka wakfu watu kwa Mungu kupitia damu yake.
Wherefore, also Jesus — that he might sanctify through [his] own blood the people — without the gate did suffer;
13 Na kwa hiyo twendeni kwake nje ya kambi, tukizibeba fadheha zake.
now, then, may we go forth unto him without the camp, his reproach bearing;
14 Kwani hatuna makao ya kudumu katika mji huu. Badala yake tutafute mji ambao unakuja.
for we have not here an abiding city, but the coming one we seek;
15 Kupitia Yesu mnapaswa mara kwa mara kujitoa sadaka ya kumtukuza Mungu, kumsifu kwamba tunda la midomo yetu likili jina lake.
through him, then, we may offer up a sacrifice of praise always to God, that is, the fruit of lips, giving thanks to His name;
16 Na usisahau kufanya mazuri na kusadiana ninyi kwa ninyi, kwa kuwa ni kwa sadaka kama hiyo ndiyo Mungu hupendezwa sana.
and of doing good, and of fellowship, be not forgetful, for with such sacrifices God is well-pleased.
17 Tiini na kujishusha kwa viongozi wenu, kwani wanaendelea kuwalinda kwa ajili ya nafsi zenu, kama wale watakaotoa hesabu. Tiini ili kwamba viongozi wenu waweze kuwatunza kwa furaha, na sio kwa huzuni, ambayo haitawasaidia.
Be obedient to those leading you, and be subject, for these do watch for your souls, as about to give account, that with joy they may do this, and not sighing, for this [is] unprofitable to you.
18 Tuombeni, kwani tuna uhakikwa kwamba tuna dhamira njema, tunatamani kuishi maisha ya heshima katika mambo yote.
Pray for us, for we trust that we have a good conscience, in all things willing to behave well,
19 Na nyote ninawatia moyo zaidi mfanye hivi, ili kwamba niweze kurudi kwenu hivi karibuni.
and more abundantly do I call upon [you] to do this, that more quickly I may be restored to you.
20 Sasa Mungu wa amani, ambaye aliwaleta tena kutoka kwa wafu mchungaji mkuu wa kondoo, Bwana wetu Yesu, kwa damu ya agano la milele, (aiōnios g166)
And the God of the peace, who did bring up out of the dead the great shepherd of the sheep — in the blood of an age-during covenant — our Lord Jesus, (aiōnios g166)
21 Atawapa uwezo kwa kila jambo zuri kufanya mapenzi yake, akifanya kazi ndani yetu iliyo njema ya kupendeza machoni pake, kupitia Yesu Kristo, kwake uwe utukufu milele na milele. Amina. (aiōn g165)
make you perfect in every good work to do His will, doing in you that which is well-pleasing before Him, through Jesus Christ, to whom [is] the glory — to the ages of the ages! Amen. (aiōn g165)
22 Sasa ninakutia moyo, ndugu, kuchukualiana na neno la kutia moyo ambalo kwa ufupi nililiandika kwenu.
And I entreat you, brethren, suffer the word of the exhortation, for also through few words I have written to you.
23 Fahamu kwamba ndugu yetu Timotheo ameshaachiwa huru, ambaye pamoja naye nitawaona kama atakuja hivi karibuni.
Know ye that the brother Timotheus is released, with whom, if he may come more shortly, I will see you.
24 Salimia viongozi wako wote na waumini wote. Wale wanaotoka Italia wanakusalimia.
Salute all those leading you, and all the saints; salute you doth those from Italy:
25 Na neema iwe nanyi nyote.
the grace [is] with you all! Amen.

< Wahebrania 13 >