< Wahebrania 12 >

1 Kwahiyo, kwa kuwa tumezungukwa na wingu kubwa la mashaidi, na tutupe kila kitu kinacho tulemea pamoja na dhambi ambayo inatuzingira kwa urahisi. Tupige mbio kwa saburi katika mashindano yaliyowekwa mbele yetu.
Therefore also we ourselves such a great having encompassing us a cloud of witnesses, weight having laid aside every and the easily entangling sin, with endurance may run the lying before us race
2 Tuyaelekeze macho yetu kwa Yesu, aliye mwanzilishi na mwenye kutimiliza imani yetu, ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake alistahmili msalaba, akiidharau aibu yake, na akakaa chini mkono wa kulia wa kiti cha enzi cha Mungu.
looking to the of [our] faith founder and perfecter Jesus, who in view of what is lying before Him joy endured [the] cross [its] shame having despised, at right hand and of the throne of God (has sat down. *N(k)O*)
3 Maana mtafakarini yeye aliye stahimili maneno ya chuki kutoka kwa wenye dhambi, dhidi yake mwenyewe ili kwamba msije mkachoka au kuzimia mioyo yenu.
do consider fully for the [One] such great having endured from sinners against (Himself *N(k)(O)*) hostility, so that not you may grow weary in the souls of you fainting.
4 Hamjataabika au kuteseka mkishindana na dhambi kiasi cha kuishiwa damu.
Not yet unto blood have you resisted against sin struggling
5 Tena mmesahau kule kutiwa moyo ambako kunawaelekeza kama watoto wa kiume: “Mwanangu, usiyachukuwe kwa wepesi marudia ya Bwana, wala usikate tamaa unapo rekebishwa na yeye.”
and you have forgotten the exhortation that you as to sons addresses: Son of Mine, not do regard lightly [the] discipline of [the] Lord, nor do faint by Him being reproved.
6 Kwa kuwa Bwana humrudi yeyote ambaye anampenda, na humwadhibu kila mwana ambaye humpokea.
Whom for He loves [the] Lord disciplines, He scourges now every son whom He receives.
7 Stahimili majaribu kama kurudiwa. Mungu hushughulika nanyi kama anavyoshughulika na watoto, maana ni mtoto yupi ambaye baba yake hawezi kumrudi?
As discipline endure, as sons you is treating God; what for (is *k*) son [is there] whom not disciplines [his] father?
8 Lakini kama hakuna kurudiwa, ambako sisi sote tunashiriki, basi ninyi ni haramu na si watoto wake.
If however without you are of discipline of which partakers they have become all, then illegitimate children and not sons you are.
9 Zaidi ya yote, tulikuwa na baba zetu kidunia wa kuturudi, na tuliwaheshimu. Je haitupasi hata zaidi kumtii Baba wa kiroho na kuishi?
Furthermore indeed of the flesh of us fathers we were having correctors and we were respecting [them]; not (much *N(k)O*) (however *n*) more will we be in subjection to the Father of spirits and will live?
10 Kwa hakika baba zetu walituadhibu kwa miaka michache kama ilivyoonekana sawa kwao, lakini Mungu hutuadhibu kwa faida yetu ili tushiriki utakatifu wake.
Indeed for during a few days according to which is seeming good to them they were disciplining [us], [He] however for which is [our] benefitting in order to share of the holiness of Him.
11 Hakuna adhabu inayofurahisha kwa wakati huo. Huwa na maumivu. Hata hivyo, baadaye huzaa tunda la amani ya utauwa kwa wale waliofundishwa nayo.
All (now *NK(o)*) discipline for indeed those being present not it seems of joy to be but of grief, afterward however [the] fruit peaceable to those through it trained it yields of righteousness.
12 Kwa hiyo inueni mikono yenu iliyolegea na kufanya magoti yenu yaliyo dhaifu kuwa yenye nguvu tena;
Therefore the drooped hands and the enfeebled knees do lift up,
13 nyosheni mapito ya nyayo zenu, ili kwamba yeyote aliye mlemavu hataongozwa upotevuni lakini apate kuponywa.
and paths straight (do make *N(k)O*) for the feet of you, so that not the lame may be disabled, may be healed however rather.
14 Tafuteni amani na watu wote, na pia utakatifu ambao bila huo hakuna atakayemwona Bwana.
Peace do pursue with all and holiness, which without no [one] will behold the Lord;
15 Muwe waangalifu ili kwamba asiwepo atakayetengwa mbali na neema ya Mungu, na kwamba lisije shina la uchungu litakalochipuka na kusababisha shida na kukengeusha wengi.
observing lest any be failing of the grace of God, lest any root of bitterness up springing may trouble [you], and through (this *N(k)O*) may be defiled (*o*) many;
16 Angalieni kuwa hakuna zinaa au mtu asiye mtauwa kama vile Esau, ambaye kwa sababu ya mlo mmoja aliuza haki yake ya kuzaliwa.
lest [there be] any fornicator or profane person as Esau, who for meal one sold the birthright (of himself. *N(k)O*)
17 Kwa kuwa mnajua kwamba baadaye, alipotamani kurithi baraka, alikataliwa, kwa sababu hakupata fursa ya kutubu pamoja na baba yake, hata ingawa alitafuta sana kwa machozi.
You know for that even afterward wishing to inherit the blessing he was rejected; of repentance for place not he found although with tears having earnestly sought it.
18 Kwa kuwa hamkuja katika mlima ambao unaweza kuguswa, Mlima unaowaka moto, giza, kukatisha tamaa na dhoruba.
Not for you have come to [that] being touched (mountain *K*) and kindled with fire and to darkness and (to gloom *N(k)O*) and to storm
19 Hamkuja kwa sauti za tarumbeta, au kwa maneno yatokanayo na sauti ambayo ilisababisha kila wasikiao wasiombe neno lolote kusemwa kwao.
and of a trumpet to [the] sound and to a voice of declaration which those having heard they excused themselves [asking] not to be addressed to them [the] word;
20 Kwa kuwa hawakuweza kuvumilia kile kilichoamuliwa: “Ikiwa hata mnyama agusaye mlima, lazima apigwe kwa mawe.”
not [able] they were bearing for which is being commanded: If even If even a beast shall touch the mountain, it will be stoned (or with arrow will be shot down *K*)
21 Ya kutisha zaidi aliyoyaona Musa alisema, “Nimeogopa sana kiasi cha kutetemeka”.
And thus fearful was the [thing] appearing [that] Moses said; Greatly afraid I am and trembling;
22 Badala yake, mmekuja mlima Sayuni na katika mji wa Mungu aliye hai, Yerualem ya mbinguni, na kwa malaika elfu kumi wanaosherehekea.
But you have come to Zion Mount and to [the] city of God [the] living, to Jerusalem [the] heavenly and to myriads of angels
23 Mmekuja katika kusanyiko la wazaliwa wa kwanza wote waliosajiliwa mbinguni, kwa Mungu hakimu wa wote, na kwa roho za watakatifu ambao wamekamilishwa.
to [the] assembly and to [the] church of [the] firstborn enrolled in [the] heavens and to [the] judge God of all and to [the] spirits of [the] righteous perfected
24 Mmekuja kwa Yesu mpatanishi wa agano jipya, na kwa damu iliyonyunyizwa ambayo hunena mema zaidi kuliko damu ya Habili.
and of a covenant new [the] mediator to Jesus and to [the] blood of sprinkling (better thing *N(K)O*) speaking than that of Abel.
25 Angalia kuwa usije ukamkataa mmoja ambaye anenaye. Kwa kuwa kama hawakuepuka walipomkataa mmoja aliye waonya duniani, kwa hakika hatutaepuka ikiwa tutageuka mbali kutoka kwa yule atuonyaye kutoka mbinguni.
do take heed lest you may refuse the [One] speaking; If for they not (escaped *N(k)O*) on (*k*) earth having refused the [One] divinely instructing [them], (much *N(k)O*) less we ourselves the [One] from [the] heavens turning away from,
26 Kwa wakati huo sauti yake ilitikisa dunia. Lakini sasa ameahidi na kunena, “Bado mara nyingine tena sitatikisa dunia pekee, bali mbingu pia.”
whose voice the earth shook at that time, now however He has promised saying; Yet once [more] I myself (will shake *N(k)O*) not only the earth but also heaven.
27 Maneno haya, “Mara moja tena,” inaonesha kutoweshwa kwa vitu vile vitetemeshwavyo, hivi ni, vitu vile ambavyo vimeumbwa, ili kwamba vile vitu visivyotetemeshwa vibakie.
This now Yet once [more], signifies that of the [things] being shaken removing as created, so that may remain the [things] not being shaken.
28 Kwa hiyo, tupokee ufalme ambao hautetemeshwi, tufurahi katika hali ya kumwabudu Mungu kwa kukubali pamoja na kunyenyekea katika kicho,
Therefore a kingdom not to be shaken receiving we may have grace through which (we may serve *NK(o)*) well pleasingly God with reverence and (fear; *N(k)O*)
29 kwa maana Mungu wetu ni moto ulao.
Also for the God of us [is] a fire consuming.

< Wahebrania 12 >