< Wahebrania 11 >

1 Sasa imani ni hakika aliyo nayo mtu wakati atarajiapo kitu fulani kwa ujasiri. Ni hakika ya kitu ambacho bado hakijaonekana.
Now faith is a realization of things being hoped for, an evidence of things not seen.
2 Kwa sababu hii mababu zetu walithibitika kwa imani yao.
By it the ancients were approved.
3 Kwa imani tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa amri ya Mungu, ili kwamba kile kinachoonekana hakikutengenezwa kutokana na vitu ambavyo vilikuwa vinaonekana. (aiōn g165)
By faith we understand that the ages were created by a word from God, so that the things that are seen were made out of things invisible. (aiōn g165)
4 Ilikuwa kwa sababu ya imani kwamba Habili alimtolea Mungu sadaka ya kufaa kuliko alivyofanya Kaini. Ilikuwa ni kwa sababu hii kwamba alisifiwa kuwa mwenye haki. Mungu alimsifu kwa sababu ya zawadi alizoleta. Kwa sababu hiyo, Habili bado ananena, ingawa amekufa.
By faith Abel offered to God a better sacrifice than did Cain, through which he obtained witness that he was righteous, God testifying concerning his gifts; and by means of it he still speaks, even though being dead.
5 Ilikuwa kwa imani kwamba Enoko alichukuliwa juu na hakuona mauti. “Hakuonekana, kwa sababu Mungu alimchukua” kwa vile ilinenwa juu yake kuwa alimpendeza Mungu kabla ya kuchukuliwa juu.
By faith Enoch was transferred so as not to see death, and could not be found because God had translated him; before his translation he had obtained witness that he was pleasing to God.
6 Pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu, kwa kuwa ajaye kwa Mungu lazima aamini kwamba Mungu anaishi na kwamba huwapatia zawadi wale wamtafutao.
Now without faith it is impossible to please Him, because the one approaching God must believe that He exists and that He becomes a rewarder of those who earnestly seek Him.
7 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Nuhu, akiwa ameonywa na Mungu kuhusiana na mambo ambayo hayakuwa yameonekana, kwa heshima ya ki Mungu alitengeneza safina kwa ajili ya kuiokoa familia yake. Kwa kufanya hivi, aliuhukumu ulimwengu na akawa mrithi wa haki ambayo huja kupitia imani.
By faith Noah, being divinely warned of things not yet seen, moved with godly fear, prepared an ark for the salvation of his household, by which he condemned the world and became an heir of the righteousness that is according to faith.
8 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Ibrahimu, alipoitwa alitii na kwenda mahali ambapo alipaswa kupokea kama urithi. Alitoka bila kujua mahali gani alikuwa anakwenda.
By faith Abraham, upon being called to go forth to the place that he would receive as an inheritance, obeyed and went, though not being acquainted with where he was going.
9 Ilikuwa ni kwa imani kwamba aliishi katika nchi ya ahadi kama mgeni. Aliishi katika mahema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi wenzake wa ahadi ile ile.
By faith he migrated into the land of promise as into a foreign country, dwelling in tents, along with Isaac and Jacob, the fellow heirs of the same promise;
10 Hii ni kwa sababu alitarajia kuupata mji ambao mwenye kuubuni na mjenzi wake angelikuwa ni Mungu.
for he was waiting expectantly for the city with the real foundations, whose designer and builder is God.
11 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Ibrahimu, na Sara mwenyewe, walipokea nguvu ya kutunga mimba ingawa walikuwa wazee sana, kwa kuwa walimuona Mungu kuwa mwaminifu, ambaye aliwaahidia mtoto wa kiume.
By faith Sarah herself also received power to conceive seed, and she bore a child when she was past the normal age, since she judged Him faithful who had promised.
12 Kwa hiyo pia kutoka kwa mtu huyu mmoja ambaye alikuwa amekaribia kufa wakazaliwa watoto wasiohesabika. Walikuwa wengi kama nyota za angani na wengi kama mbegu za mchanga katika ufukwe wa bahari.
And so from one man, actually an impotent, were begotten descendants as numerous as the stars in the sky, and as countless as the sand on the seashore.
13 Hawa wote walikufa katika imani pasipo kupokea ahadi. Isipokuwa, wakiwa wameziona na kuzikaribisha kwa mbali, walikiri kwamba walikuwa wageni na wapitaji juu ya nchi.
These all died believing—not having received the promises, but having seen and welcomed them from a distance, thus confessing that they were aliens and sojourners on the earth.
14 Kwa wale wasemao mambo kama haya wanaweka bayana kuwa wanatafuta nchi yao wenyewe.
Now those who say such things make it clear that they are seeking a homeland.
15 Kwa kweli, kama wangekuwa wakiifikiria nchi ambayo kwayo walitoka, wangelikuwa na nafasi ya kurejea.
If they were actually remembering that land from which they had departed, they would have had opportunity to return.
16 Lakini kama ilivyo, wanatamani nchi iliyo bora, ambayo, ni ya kimbingu. Kwa hiyo Mungu haoni aibu kuitwa Mungu wao, kwa kuwa ametayarisha mji kwa ajili yao.
Instead they are aspiring to a better home—a heavenly one. Therefore God is not ashamed to be called their God; in fact He has prepared a city for them.
17 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Ibrahimu baada ya kujaribiwa, alimtoa Isaka. Ndiyo, yeye ambaye alipokea kwa furaha ahadi, alimtoa mwanawe wa pekee,
By faith Abraham, upon being tested, offered up Isaac; yes, he who had received the promises was about to sacrifice his only begotten,
18 ambaye juu yake ilinenwa, “Kutoka kwa Isaka uzao wako utaitwa.”
of whom it had been said, “Through Isaac will your seed be reckoned,”
19 IbrahImU alijua kwamba Mungu alikuwa na uwezo wa kumfufua Isaka kutoka katika wafu, na kwa kuzungumza kwa lugha ya maumbo, alimpokea.
calculating that God was indeed able to raise him from the dead; from whence in fact he did receive him, figuratively speaking.
20 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Isaka alimbariki Yakobo na Esau kuhusu mambo yajayo.
By faith Isaac blessed Jacob and Esau concerning things to come.
21 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Yakobo alipokuwa katika hali ya kufa, alimbariki kila mmoja wa watoto wa Yusufu. Yakobo akaabudu, akiegemea juu ya fimbo yake.
By faith Jacob, when he was dying, blessed each of Joseph's sons and worshiped, leaning on the top of his staff.
22 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Yusufu wakati wake wa mwisho ulipokaribia, alinena juu ya kutoka kwa wana wa Israel Misri na akawaagiza kuchukua pamoja nao mifupa yake.
By faith Joseph, near the end, thought of the exodus of the sons of Israel and gave orders concerning his bones.
23 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Musa, alipozaliwa, alifichwa kwa miezi mitatu na wazazi wake kwa sababu walimuona kuwa ni mtoto mchanga aliyekuwa mzuri, na hawakutishwa na amri ya mfalme.
By faith Moses was hidden for three months by his parents, after he was born, because they saw he was a fine child, and they were not afraid of the king's edict.
24 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Musa, alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mtoto wa binti Farao.
By faith Moses, when he had grown up, refused to be called the son of Pharaoh's daughter,
25 Badala yake, alichagua kushiriki mateso pamoja na watu wa Mungu badala ya kufurahia anasa za dhambi kwa kitambo.
choosing rather to be maltreated along with God's people than to have the temporary pleasure of sin,
26 Alifikiri aibu ya kumfuata Kristo kuwa ni utajiri mkuu kuliko hazina za Misri kwa kuwa alikaza macho yake katika zawadi ya wakati wake ujao.
considering the reproach of Christ to be greater riches than the treasures of Egypt; because he was looking ahead to the reward.
27 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Musa alitoka Misri. Hakuhofia hasira ya Mfalme, kwa kuwa alivumilia kwa kutazama kwa asiyeonekana.
By faith he left Egypt behind, not fearing the king's rage, because he persevered as though seeing Him who is invisible.
28 Ilikuwa ni kwa imani kwamba aliishika pasaka na kunyunyiza damu, ili kwamba mharibu wa mzaliwa wa kwanza asiweze kuwagusa wazaliwa wa kwanza wa kiume wa waisrael.
By faith he kept the Passover and the sprinkling of the blood, so that the destroyer of the firstborn would not touch them.
29 Ilikuwa ni kwa imani kwamba walipita katika bahari ya shamu kama katika nchi kavu. Wakati wamisri walipojaribu kupita, walimezwa.
By faith they passed through the Red Sea as on dry ground, whereas the Egyptians, attempting to do so, were swallowed up.
30 Ilikuwa ni kwa imani kwamba ukuta wa Yeriko ulianguka chini, baada ya kuuzunguka kwa siku saba.
By faith the walls of Jericho fell down, having been encircled for seven days.
31 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Rahabu yule kahaba hakuangamia pamoja na wale ambao hawakuwa watiifu, kwa sababu alikuwa amewapokea wapelelezi na kuwahifadhi salama.
By faith the prostitute Rahab, having received the spies in peace, did not perish with the disobedient.
32 Na niseme nini zaidi? Maana muda hautoshi kusimulia ya Gideoni, Barak, Samsoni, Yeftha, Daudi, Samwel na za manabii,
And what more shall I say? For the time would fail me to tell about Gideon, about Barak and Samson and Jephtha, about David and Samuel and the prophets,
33 ambao kupitia imani walizishinda falme, walitenda haki, na wakapokea ahadi. Walizuia vinywa vya simba,
who through faith subdued kingdoms, administered justice, obtained promises, closed lions' mouths,
34 walizima nguvu za moto, walikwepa ncha ya upanga, waliponywa kutoka katika magonjwa, walikuwa mashujaa vitani, na walisababisha majeshi wageni kukimbia.
quenched the power of fire, escaped the edge of the sword, out of weakness were made strong, became mighty in battle, put to flight foreign armies.
35 Wanawake walipokea wafu wao kwa njia ya ufufuo. Wengine waliteswa, bila kukubali kuachwa huru ili kwamba waweze kupata uzoefu wa ufufuo ulio bora zaidi.
Women received their dead back by resurrection; while others were tortured, not accepting their deliverance, so that they might obtain a better resurrection.
36 Wengine waliteswa kwa dhihaka na kwa vichapo, naam, hata kwa vifungo na kwa kutiwa gerezani.
Still others were tried by mockings and scourgings, and even by chains and imprisonment.
37 Walipondwa mawe. Walikatwa vipande kwa misumeno. Waliuawa kwa upanga. Walikwenda kwa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi walikuwa wahitaji, wakiendelea katika maumivu na wakitendewa mabaya
They were stoned, they were sawed in two, they were tempted, they were murdered by sword. They went about in sheepskins and goatskins; being destitute, afflicted, mistreated
38 (ambayo ulimwengu haukustahili kuwa nao), wakitangatanga nyikani, milimani, katika mapango na katika mashimo ya ardhini.
—of whom the world was not worthy—wandering in deserts and mountains and caves and holes in the ground.
39 Ingawa watu wote hawa walikubaliwa na Mungu kwa sababu ya imani yao, hawakupokea alichoahidi.
Now all these did not receive the promise, though having been approved through faith,
40 Mungu alitangulia kutupatia kitu kilichobora, ili kwamba bila sisi wasingeweza kukamilishwa.
God having planned something better for us, so that they should not be perfected without us.

< Wahebrania 11 >