< Wahebrania 10 >

1 Kwa vile sheria ni kivuli cha mambo mema yajayo, si yale yaliyo halisi. Sheria kamwe haiwezi kuwakamilisha wale ambao wanaomkaribia Mungu kwa njia ya dhabihu zilezile ambazo makuhani waliendelea kutoa mwaka baada ya mwaka.
En effet, la loi, n'ayant que l'ombre des biens à venir, et non la forme réelle des choses, ne peut jamais, par les mêmes sacrifices qu'on offre chaque année à perpétuité, amener à la perfection ceux qui s'approchent ainsi de Dieu.
2 Au vinginevyo dhabihu hizo zisingeweza kukoma kutolewa? Kwa kigezo hicho waabuduo, wakiwa wamesafishwa mara moja, wasingelikuwa na utambuzi zaidi wa dhambi.
Autrement, n'aurait-on pas cessé de les offrir, puisque ceux qui rendent ce culte, une fois purifiés, n'auraient plus eu leur conscience chargée de péchés?
3 Bali katika dhabihu hizo kuna ukumbusho wa dhambi zilizotendwa mwaka baada ya mwaka.
Au contraire, le souvenir des péchés est renouvelé chaque année par ces sacrifices.
4 Kwa kuwa haiwezekani kwa damu ya mafahari na mbuzi kuziondoa dhambi.
Car il est impossible que le sang des taureaux et des boucs ôte les péchés.
5 Wakati Kristo alipokuja duniani, alisema, “Hamkutamani matoleo au dhabihu, badala yake, mliandaa mwili kwa ajili yangu.
C'est pourquoi le Christ, entrant dans le monde, dit: «Tu n'as voulu ni sacrifice, ni offrande, mais tu m'as formé un corps.
6 Hamkuwa na thamani katika matoleo yote ya kuteketezwa au dhabihu kwa ajili ya dhambi.
Tu n'as agréé ni les holocaustes, ni les offrandes pour le péché.
7 Kisha nilisema, “Ona, hapa ninayafanya mapenzi yako, Mungu, kama ilivyoandikwa kunihusu mimi katika gombo”.
Alors j'ai dit: Je viens — il est parlé de moi dans le Livre — oui, je viens, ô Dieu, pour faire ta volonté.»
8 Alisema kama ilivyo semwa hapo juu: “Hamkutamani dhabihu, matoleo, au sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya dhambi, wala hukuona furaha ndani yake” dhabihu ambazo zinatolewa kulingana na sheria.
Après avoir dit d'abord: «Tu n'as voulu, tu n'as agréé ni sacrifices, ni offrandes, ni holocaustes, ni oblations pour le péché», — ce qui pourtant est prescrit par la loi, —
9 Kisha alisema, “Ona, niko hapa kufanya mapenzi yako”. Ameweka pembeni taratibu zilizo za awali ili kuimarisha zile za pili.
il ajoute: «Me voici: Je viens pour faire ta volonté.» Il abolit ainsi le premier ordre de sacrifices pour établir le second.
10 Katika taratibu za pili, tumekwisha tengwa kwa Mungu kwa mapenzi yake kupitia kujitoa kwa mwili wa Yesu Kristo mara moja kwa nyakati zote.
C'est en vertu de cette volonté que nous avons été sanctifiés, par le sacrifice que Jésus-Christ a fait, une fois pour toutes, de son propre corps.
11 Ni kweli, kila kuhani husimama kwa huduma siku kwa siku, akitoa dhabihu ile ile, ambayo, kwa vyovyote, kamwe isingeweza kuziondoa dhambi.
De plus, tandis que tout sacrificateur se présente, chaque jour, pour faire le service et offrir plusieurs fois les mêmes sacrifices qui ne peuvent jamais ôter les péchés,
12 Lakini baada ya Kristo kutoa dhabihu mara moja kwa dhambi milele yote, aliketi mkono wa kuume wa Mungu,
celui-ci, après avoir offert un seul sacrifice pour les péchés, s'est assis pour toujours à la droite de Dieu,
13 akisubiri mpaka maadui zake watiwe chini na kufanywa kiti kwa ajili ya miguu yake.
attendant désormais que ses ennemis soient mis sous ses pieds, pour lui servir de marchepied.
14 Kwa kuwa kwa njia ya toleo moja amewakamilisha milele wale ambao wametengwa kwa Mungu.
En effet, par une seule oblation, il a amené pour toujours à la perfection ceux qui sont sanctifiés.
15 Na Roho Mtakatifu pia ashuhudia kwetu. Kwa kuwa kwanza alisema,
Et c'est aussi ce que nous atteste le Saint-Esprit; car, après avoir dit:
16 “Hili ni agano nitakalofanya pamoja nao baada ya siku hizo; asema Bwana: nitaweka sheria zangu ndani ya mioyo yao, na nitaziandika katika akili zao”.
«Voici l'alliance que je traiterai avec eux après ces jours-là, dit le Seigneur: Je mettrai mes lois dans leurs coeurs, et je les graverai dans leur esprit», — il ajoute:
17 Kisha alisema, “Hawatazikumbuka tena dhambi na matendo yao mafu”.
«Et je ne me souviendrai plus de leurs péchés ni de leurs iniquités.»
18 Sasa mahali palipo na msamaha kwa hawa, hakuna tena dhabihu yoyote kwa ajili ya dhambi.
Or, là où il y a pardon, il n'est plus besoin d'oblation pour le péché.
19 Kwa hiyo, ndugu, tunao ujasiri wa kuingia mahali patakatifu zaidi kwa damu ya Yesu.
Ainsi donc, frères, puisque nous avons un libre accès dans le lieu très saint, grâce au sang de Jésus,
20 Hiyo ni njia ambayo ameifungua kwa ajili yetu kwa njia ya mwili wake, mpya na hai inayopitia kwenye pazia.
par le chemin nouveau et vivant qu'il nous a frayé à travers le voile, c'est-à-dire à travers sa propre chair,
21 Na kwa sababu tunaye kuhani mkuu juu ya nyumba ya Mungu,
et puisque nous avons un grand sacrificateur établi sur la maison de Dieu,
22 na tumkaribie na moyo wa kweli katika utimilifu wa uhakika wa imani tukiwa na mioyo iliyonyunyiziwa safi kutoka uovu wa dhamiri na kuwa na miili yetu iliyooshwa kwa maji safi.
approchons-nous avec un coeur sincère, avec une foi pleine et entière, le coeur purifié des souillures d'une mauvaise conscience, et le corps lavé d'une eau pure.
23 Basi na tushikilie kwa uthabiti katika ungamo la ujasiri wa tumaini letu, bila ya kugeuka, kwa sababu Mungu aliyeahidi ni mwaminifu.
Retenons fermement la profession de notre espérance, car Celui qui a fait les promesses est fidèle.
24 Na tuzidi kutafakari namna ya kumtia moyo kila mmoja kupenda na matendo mema.
Veillons les uns sur les autres pour nous exciter à la charité et aux bonnes oeuvres,
25 Na tusiache kukusanyika pamoja, kama wafanyavyo wengine. Badala yake, kutiana moyo kila mmoja zaidi na zaidi, kama muonavyo siku inakaribia.
et n'abandonnons pas nos assemblées, comme quelques-uns ont coutume de faire, mais exhortons-nous les uns les autres, et cela d'autant plus que vous voyez approcher le grand jour.
26 Kama tukifanya makusudi kuendelea kutenda dhambi baada ya kuwa tumepokea elimu ya ukweli, Dhabihu nyingine ya dhambi haisalii tena.
En effet, si nous péchons volontairement, après avoir reçu la connaissance de la vérité, il ne reste plus de sacrifice pour les péchés,
27 Badala yake, kuna tarajio pekee la hukumu ya kutisha, na ukali wa moto ambao utawateketeza maadui wa Mungu.
mais seulement la terrible attente du jugement et le feu ardent, qui doit dévorer les rebelles.
28 Yeyote ambaye ameikataa sheria ya Musa hufa bila rehema mbele ya ushuhuda wa mashahidi wawili au watatu.
Celui qui a violé la loi de Moïse, meurt sans miséricorde, sur la déposition de deux ou trois témoins.
29 kiwango gani zaidi cha adhabu unafikiri kinamstahiri kilammoja ambaye amemdharau mwana wa Mungu, yeyote aliyeitendea damu ya agano kama kitu kisicho kitakatifu, damu ambayo kwayo aliiweka wakfu kwa Mungu - yeyote ambaye amemtukana Roho wa neema?
Ne pensez-vous pas qu'il sera jugé digne d'un châtiment bien plus sévère, celui qui aura foulé aux pieds le Fils de Dieu, qui aura tenu pour vil le sang de l'alliance par lequel il a été sanctifié, et qui aura outragé l'Esprit de la grâce?
30 Kwakuwa tunajua mmoja ambaye aliyesema, “Kisasi ni changu, nitalipa”. Na tena, “Bwana atawahukumu watu wake”.
Car nous connaissons celui qui a dit: «C'est à moi qu'appartient la vengeance; c'est moi qui rétribuerai», — dit le Seigneur.
31 Ni jambo la kuogofya mtu kuangukia katika mikono ya Mungu aliye hai!
Et ailleurs: «Le Seigneur jugera son peuple.» C'est une chose terrible que de tomber entre les mains du Dieu vivant!
32 Lakini kumbuka siku zilizopita, baada ya kutiwa kwenu nuru, ni jinsi gani mliweza kuvumilia maumivu makali.
Rappelez-vous ces premiers temps, où, après avoir été éclairés, vous avez soutenu un grand combat de souffrances:
33 Mlikuwa mmewekwa wazi katika dhihaka ya matukano na mateso, na mlikuwa washiriki pamoja na wale waliopitia mateso kama hayo.
d'un côté, vous avez été exposés comme en spectacle aux opprobres et aux afflictions, de l'autre, vous avez pris part aux maux de ceux qui subissaient les mêmes traitements.
34 Kwa kuwa mlikuwa na moyo wa huruma kwa hao waliokuwa wafungwa, na mlipokea kwa furaha adhabu ya urithi wenu, mkijua kwamba ninyi wenyewe mlikuwa na urithi bora na wa kudumu milele.
Car vous avez eu compassion des prisonniers, et vous avez accepté avec joie qu'on vous ravît vos biens, sachant que vous en avez de meilleurs et qui durent toujours.
35 Kwa hiyo msiutupe ujasiri wenu, ulio na zawadi kuu.
N'abandonnez donc pas votre confiance, à laquelle une grande récompense est réservée.
36 Kwa kuwa mnahitaji uvumilivu, ili kwamba mpate kupokea ambacho Mungu amekiahidi, baada ya kuwa mmekwisha yatenda mapenzi yake.
Car vous avez besoin de persévérance, afin qu'après avoir fait la volonté de Dieu, vous obteniez ce qui vous a été promis.
37 Kwa kuwa baada ya kitambo kidogo, mmoja anayekuja, atakuja hakika na hatakawia.
Encore un peu, bien peu de temps, et celui qui doit venir, viendra; il ne tardera point.
38 Mwenye haki wangu ataishi kwa imani. Kama atarudi nyuma, sitapendezwa naye.”
«Et mon juste vivra par la foi; mais s'il se retire, mon âme ne prend point plaisir en lui.»
39 Lakini sisi si kama wale warudio nyuma kwa kuangamia. Badala yake, sisi ni baadhi ya wale tulio na imani ya kuzilinda roho zetu.
Pour nous, nous ne sommes pas de ceux qui se retirent pour leur perte, mais de ceux qui gardent la foi pour sauver leur âme.

< Wahebrania 10 >