< Wahebrania 10 >
1 Kwa vile sheria ni kivuli cha mambo mema yajayo, si yale yaliyo halisi. Sheria kamwe haiwezi kuwakamilisha wale ambao wanaomkaribia Mungu kwa njia ya dhabihu zilezile ambazo makuhani waliendelea kutoa mwaka baada ya mwaka.
For the law is only a shadow of the good things to come, not the real forms of those things themselves. Those who approach God can never be made perfect by the same sacrifices that the priests continually bring year after year.
2 Au vinginevyo dhabihu hizo zisingeweza kukoma kutolewa? Kwa kigezo hicho waabuduo, wakiwa wamesafishwa mara moja, wasingelikuwa na utambuzi zaidi wa dhambi.
Otherwise, would the sacrifices not have ceased to be offered? For the worshipers would have been cleansed one time and would no longer have any consciousness of sin.
3 Bali katika dhabihu hizo kuna ukumbusho wa dhambi zilizotendwa mwaka baada ya mwaka.
But with those sacrifices there is a reminder of sins year after year.
4 Kwa kuwa haiwezekani kwa damu ya mafahari na mbuzi kuziondoa dhambi.
For it is impossible for the blood of bulls and goats to take away sins.
5 Wakati Kristo alipokuja duniani, alisema, “Hamkutamani matoleo au dhabihu, badala yake, mliandaa mwili kwa ajili yangu.
When Christ came into the world, he said, “Sacrifices and offerings you did not desire, but a body you have prepared for me;
6 Hamkuwa na thamani katika matoleo yote ya kuteketezwa au dhabihu kwa ajili ya dhambi.
with burnt offerings and sin offerings you did not take pleasure.
7 Kisha nilisema, “Ona, hapa ninayafanya mapenzi yako, Mungu, kama ilivyoandikwa kunihusu mimi katika gombo”.
Then I said, 'See, here I am— as it is written about me in the scroll— to do your will.'”
8 Alisema kama ilivyo semwa hapo juu: “Hamkutamani dhabihu, matoleo, au sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya dhambi, wala hukuona furaha ndani yake” dhabihu ambazo zinatolewa kulingana na sheria.
First he said, “It was neither sacrifices, nor offerings, nor whole burnt offerings, nor sacrifices for sin that you desired. Nor did you take pleasure in them.” These are sacrifices that are offered according to the law.
9 Kisha alisema, “Ona, niko hapa kufanya mapenzi yako”. Ameweka pembeni taratibu zilizo za awali ili kuimarisha zile za pili.
Then he said, “See, here I am to do your will.” He takes away the first practice in order to establish the second practice.
10 Katika taratibu za pili, tumekwisha tengwa kwa Mungu kwa mapenzi yake kupitia kujitoa kwa mwili wa Yesu Kristo mara moja kwa nyakati zote.
By that will, we have been sanctified through the offering of the body of Jesus Christ once for all.
11 Ni kweli, kila kuhani husimama kwa huduma siku kwa siku, akitoa dhabihu ile ile, ambayo, kwa vyovyote, kamwe isingeweza kuziondoa dhambi.
Day after day every priest stands and performs his service to God. He offers the same sacrifices again and again—sacrifices that can never take away sins.
12 Lakini baada ya Kristo kutoa dhabihu mara moja kwa dhambi milele yote, aliketi mkono wa kuume wa Mungu,
But when Christ offered for all time one sacrifice for sins, he sat down at the right hand of God.
13 akisubiri mpaka maadui zake watiwe chini na kufanywa kiti kwa ajili ya miguu yake.
He is waiting until his enemies are made a stool for his feet.
14 Kwa kuwa kwa njia ya toleo moja amewakamilisha milele wale ambao wametengwa kwa Mungu.
For by one offering he has perfected forever those who are being sanctified.
15 Na Roho Mtakatifu pia ashuhudia kwetu. Kwa kuwa kwanza alisema,
The Holy Spirit also testifies to us. First he said,
16 “Hili ni agano nitakalofanya pamoja nao baada ya siku hizo; asema Bwana: nitaweka sheria zangu ndani ya mioyo yao, na nitaziandika katika akili zao”.
“This is the covenant that I will make with them after those days, says the Lord. I will put my laws in their hearts, and I will write them on their minds.
17 Kisha alisema, “Hawatazikumbuka tena dhambi na matendo yao mafu”.
Their sins and lawless deeds I will remember no longer.”
18 Sasa mahali palipo na msamaha kwa hawa, hakuna tena dhabihu yoyote kwa ajili ya dhambi.
Now where there is forgiveness for these, there is no longer any sacrifice for sin.
19 Kwa hiyo, ndugu, tunao ujasiri wa kuingia mahali patakatifu zaidi kwa damu ya Yesu.
Therefore, brothers, we have confidence to enter into the most holy place by the blood of Jesus.
20 Hiyo ni njia ambayo ameifungua kwa ajili yetu kwa njia ya mwili wake, mpya na hai inayopitia kwenye pazia.
That is the new and living way that he has opened for us through the curtain, that is, by means of his flesh.
21 Na kwa sababu tunaye kuhani mkuu juu ya nyumba ya Mungu,
Because we have a great priest over the house of God,
22 na tumkaribie na moyo wa kweli katika utimilifu wa uhakika wa imani tukiwa na mioyo iliyonyunyiziwa safi kutoka uovu wa dhamiri na kuwa na miili yetu iliyooshwa kwa maji safi.
let us approach with true hearts in the full assurance of faith, having our hearts sprinkled clean from an evil conscience and having our bodies washed with pure water.
23 Basi na tushikilie kwa uthabiti katika ungamo la ujasiri wa tumaini letu, bila ya kugeuka, kwa sababu Mungu aliyeahidi ni mwaminifu.
Let us also hold tightly to the confession of our hope without wavering, because God, who has promised, is faithful.
24 Na tuzidi kutafakari namna ya kumtia moyo kila mmoja kupenda na matendo mema.
Let us consider how to motivate one another to love and good deeds.
25 Na tusiache kukusanyika pamoja, kama wafanyavyo wengine. Badala yake, kutiana moyo kila mmoja zaidi na zaidi, kama muonavyo siku inakaribia.
Let us not stop meeting together, as some have done. Instead, encourage one another more and more, and all the more as you see the day coming closer.
26 Kama tukifanya makusudi kuendelea kutenda dhambi baada ya kuwa tumepokea elimu ya ukweli, Dhabihu nyingine ya dhambi haisalii tena.
For if we deliberately go on sinning after we have received the knowledge of the truth, a sacrifice for sins no longer exists.
27 Badala yake, kuna tarajio pekee la hukumu ya kutisha, na ukali wa moto ambao utawateketeza maadui wa Mungu.
Instead, there is only a certain fearful expectation of judgment, and a fury of fire that will consume God's enemies.
28 Yeyote ambaye ameikataa sheria ya Musa hufa bila rehema mbele ya ushuhuda wa mashahidi wawili au watatu.
Anyone who has rejected the law of Moses dies without mercy at the testimony of two or three witnesses.
29 kiwango gani zaidi cha adhabu unafikiri kinamstahiri kilammoja ambaye amemdharau mwana wa Mungu, yeyote aliyeitendea damu ya agano kama kitu kisicho kitakatifu, damu ambayo kwayo aliiweka wakfu kwa Mungu - yeyote ambaye amemtukana Roho wa neema?
How much worse punishment do you think one deserves who has trampled underfoot the Son of God, who treated the blood of the covenant as unholy—the blood by which he was sanctified—and insulted the Spirit of grace?
30 Kwakuwa tunajua mmoja ambaye aliyesema, “Kisasi ni changu, nitalipa”. Na tena, “Bwana atawahukumu watu wake”.
For we know the one who said, “Vengeance belongs to me; I will pay back.” And again, “The Lord will judge his people.”
31 Ni jambo la kuogofya mtu kuangukia katika mikono ya Mungu aliye hai!
It is a fearful thing to fall into the hands of the living God!
32 Lakini kumbuka siku zilizopita, baada ya kutiwa kwenu nuru, ni jinsi gani mliweza kuvumilia maumivu makali.
But remember the former days, after you were enlightened, how you endured a great struggle in suffering.
33 Mlikuwa mmewekwa wazi katika dhihaka ya matukano na mateso, na mlikuwa washiriki pamoja na wale waliopitia mateso kama hayo.
You were exposed to public ridicule by insults and persecution, and you were sharing with those who went through such suffering.
34 Kwa kuwa mlikuwa na moyo wa huruma kwa hao waliokuwa wafungwa, na mlipokea kwa furaha adhabu ya urithi wenu, mkijua kwamba ninyi wenyewe mlikuwa na urithi bora na wa kudumu milele.
For you had compassion on those who were prisoners, and you accepted with joy the seizure of your possessions. You knew that you yourselves had a better and everlasting possession.
35 Kwa hiyo msiutupe ujasiri wenu, ulio na zawadi kuu.
So do not throw away your confidence, which has a great reward.
36 Kwa kuwa mnahitaji uvumilivu, ili kwamba mpate kupokea ambacho Mungu amekiahidi, baada ya kuwa mmekwisha yatenda mapenzi yake.
For you need patience, so that you may receive what God has promised, after you have done his will.
37 Kwa kuwa baada ya kitambo kidogo, mmoja anayekuja, atakuja hakika na hatakawia.
“For in a very little while, the one who is coming will indeed come and not delay.
38 Mwenye haki wangu ataishi kwa imani. Kama atarudi nyuma, sitapendezwa naye.”
My righteous one will live by faith. If he shrinks back, I will not be pleased with him.”
39 Lakini sisi si kama wale warudio nyuma kwa kuangamia. Badala yake, sisi ni baadhi ya wale tulio na imani ya kuzilinda roho zetu.
But we are not any of those who turn back to destruction. Instead, we are some of those who have faith for keeping our soul.