< Hagai 2 >

1 Katika Mwezi wa saba siku ya ishirini na moja ya mwezi, Neno la Bwana lilikuja kwa mkono wa Nabii Hagai, na kusema,
In the seventh [month], on the one and twentieth day of the month, came the word of the Lord by means of Haggai the prophet, saying,
2 “Ongea na mkuu wa mkoa wa Yudah, Zerubabeli mwana wa Sheltieli, na kwa kuhani mkuu Yehozadaki; na kwa masalia ya watu. Waambie,
Do say to Zerubbabel the son of Shealthiel, the governor of Judah, and to Joshua the son of Jehozadak, the high priest, and to the residue of the people, saying,
3 Ni nani amebaki kati yenu aliuona utukufu wa nyumba ya kwanza? Na mnauonaje huu wa sasa? Je si kama si chochote machoni penu?
Who is there yet left among you that hath seen this house in its first glory? and how do ye see it now? is it not in comparison with it as nothing in your eyes?
4 Sasa, muwe hodari, Zerubabeli' -hili ni tamko la Bwana - na uwe hodari, kuhani mkuu Joshua mwana wa Yehozadaki; muwe hodari, enyi watu wa nchi! - hili ni tamko la Bwana - na kazi, kwa kuwa ni pamoja nawe! hili ni tamko la Bwana wa majeshi.
Yet now be strong, O Zerubbabel, saith the Lord, and be strong O Joshua, the son of Jehozadak, the high priest, and be strong, all ye people of the land, saith the Lord, and do; [for I am with you, saith the Lord of hosts, ]
5 Kutegemeana na ahadi ilioko katika agano nililofanya na ninyi mlipotoka Misri na Roho yangu ilisimama katikati yenu, msiogope'
[In accordance with] the word that I covenanted with you when ye came out of Egypt, so [will] my spirit remain among you: fear nought.
6 Kwa kuwa Bwana wa majeshi anasema hivi: 'kitambo kidogo kwa mara nyingine nitatikisa mbingu na dunia, bahari na nchi kavu!
For thus hath said the Lord of hosts, Yet one thing more [will I do], it is but little, when I will cause to quake the heavens, and the earth, and the sea, and the dry land;
7 Na nitatikisa kila taifa, na kila taifa wataleta vitu vya thamani kwangu, na kuijaza nyumba hii na utukufu!' asema Bwana wa Majeshi
And I will cause to quake all the nations, and the precious things of all the nations shall come [hither]: and I will fill this house with glory, saith the Lord of hosts.
8 Dhahabu na fedha ni yangu' - hili ni tamko la Bwana wa majeshi.
Mine is the silver, and mine is the gold, saith the Lord of hosts.
9 Utukufu wa nyumba hii utakuwa mkuu zaidi ya utukufu wa nyumba ya kwanza ', asema Bwana wa majeshi,' na nitawapa amani katika sehemu hii'- hili ni Tamko la Bwana wa majeshi
Greater shall be the glory of this latter house than that of the former, saith the Lord of hosts: and in this place will I give peace, saith the Lord of hosts.
10 Katika siku ya ishirini na nne mwezi wa tisa, mwaka wa pili wa utawala wa Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Hagaina kusema,
On the four and twentieth day of the ninth month, in the second year of Darius, came the word of the Lord by means of Haggai the prophet, saying,
11 “Bwana wa majeshi asema hivi: Muulize kuhani kuhusu sheria, na kusema:
Thus hath said the Lord of hosts, Do ask the priests concerning the law, saying,
12 kama mtu akibeba nyama iliyotolewa kwa Bwana katika pindo la vazi lake, kama upindo utagusa mkate au mchuzi, mvinyo au mafuta, au chakula kingine, je chakula hicho kinafanyika kitakatifu?”Kuhani alijibu akasema, “hapana”
Lo! if one should carry holy flesh in the corner of his garment, and touch with his corner bread, or pottage, or wine, or oil, or any food, shall it become holy? And the priests answered and said, No.
13 Halafu Hagai akasema.”Kama mtu mchafu najisi kwa ajili ya kumgusa maiti na kugusa vitu hivi, wote wanaweza kuwa wachafu?” Kuhani akajibu na kusema, “Ndiyo, watakuwa wachafu.”
Then said Haggai, If one that is unclean by a dead body shall touch any of these, will it become unclean? And the priests answered and said, It will become unclean.
14 Kwa hiyo Haghai akajibu nakusema, “Ni pamoja na hawa watu na pamoja na taifa liliko mbele yangu! - haya anayasema Bwana- na pia kila kitu kimekwisha kwa mkono wake: walichotoa hakikuwa kisafi kilikuwa kichafu.
Then answered Haggai, and said, So is this people, and so is this nation before me, saith the Lord; and so are all works of their hands; and what they offer there is unclean.
15 Kwa hiyo, fikiri kutoka siku hii ya leo na za nyuma, kabla hata jiwe halijawekwa kwenye jiwe lingine katika hekalu la Bwana,
And now direct, I pray you, your heart from this day and upward, before the time that a stone was laid upon a stone in the temple of the Lord:
16 ilikuwaje basi? kila mtu alipokuja kwenye vipimo ishirini vya nafaka, kumbe kulikuwa na vipimo kumi tu, na aliyekuja na aliyekuja kuchota divai ya vipimo hamsini, kumbe kuliwa na vipimo ishirini tu.
Since those days were, when one came to a heap of sheaves of twenty [in number], and there were but ten; when one came to the winepress for to draw off fifty measures out of the vat, and there were but twenty.
17 Niliwataabisha ninyi na kazi za mikono yenu kwa doa na koga, nalikini hamkunirudia'- asema Bwana.
I smote you with blasting and with mildew and with hail in all the labors of your hands: yet ye [turned] not [back] to me, saith the Lord.
18 tafakari siku hii ya leo na kuendelea, kutoka siku ya ishirini na nne katika mwezi mwezi wa tisa, toka siku ile msingi wa hekalu la Bwana kuwekwa. Tafakarini hilo!
Direct, I pray you, your heart from this day and upward, from the four and twentieth day of the ninth month, even from the day that the foundation of the Lord's temple was laid, direct your heart [to this].
19 Je, bado kuna mbegu katika ghala? Mzabibu, mti wa mtini, komamanga, na mti wa mzeituni havikuzaa matunda! lakini kutoka siku hii ya leo nitawabariki!”'
Is the seed yet in the barn? yes, as yet the vine, and the fig-tree, and the pomegranate, and the olive-tree, have not brought forth; [but] from this day will I bless you.
20 Tena neno la Bwana likaja kwa mara ya pili kwa Haghai siku ya ishiri na nne katika mwezi kusema,
And the word of the Lord came the second time unto Haggai on the four and twentieth day of the month, saying,
21 “Sema na mkuu wa mkoa wa Yuda, Zerubabeli umwambie, 'Nitatikisa mbingu na dunia.
Speak to Zerubbabel the governor of Judah, saying, I will cause to quake the heavens and the earth;
22 kwa hiyo nitaanhusha kiti cha falme na kuharibu nguvu ya falme za mataifa! nitaangusha magahari na wapandao; farasi na wapanda farasi wataanguka, kila mmoja kwa sababu ya upanga wa ndugu zake.
And I will overthrow the throne of kingdoms, and I will destroy the strength of the kingdoms of the nations; and I will overthrow chariots, and those that ride in them; and the horses and their riders shall come down, every one by the sword of his brother.
23 Siku hiyo '-hivi ndivyo asema Bwana wa Majeshi- 'Nitakuchukua wewe Zerubabeli mwana wa Sheltieli, kama mtumishi wangu'- hivi ndivyo Bwana anavyosema. “Nitakutuma kama pete ya muhuri wangu, kwa sababu mimi ndiye niliyekuchagua!'- asema Bwana wa majeshi!”
On that day, saith the Lord of hosts, will I take thee, O Zerubbabel, the son of Shealthiel, my servant, saith the Lord, and I will place thee as a signet; for of thee have I made choice, saith the Lord of hosts.

< Hagai 2 >