< Habakuki 1 >
1 Ujumbe ambao habakuki nabii alipokea,
The burden which Habakkuk the prophet did see.
2 Yahwe, kwa muda gani nitalilia msaada, na hutasikia? Nimekulilia wewe katika kitisho, 'vurugu' lakini hutaniokoa.
O LORD, how long shall I cry, and thou wilt not hear? I cry out unto thee of violence, and thou wilt not save.
3 Kwanini unanifanya nione mabaya na kuangalia matendo mabaya. Uharibifu na vurugu uko mbele yangu; kuna mapambano, na ushindani unainuka.
Why dost thou shew me iniquity, and look upon perverseness? for spoiling and violence are before me: and there is strife, and contention riseth up.
4 Walakini sheria ni dhaifu, na haki haiishi kwa wakati wowote. Sababu uovu umezunguka haki; walakini haki ya uongo inatoweka. “Yahwe” anamjibu habakuki
Therefore the law is slacked, and judgment doth never go forth: for the wicked doth compass about the righteous; therefore judgment goeth forth perverted.
5 “Angalia mataifa na uwajaribu; stajaabishwa na shangazwa! Sababu nina uhakika kuhusu kufanya kitu katika siku zako kwamba hutaamini itakapotaarifiwa kwenu.
Behold ye among the nations, and regard, and wonder marvelously: for I work a work in your days, which ye will not believe though it be told you.
6 Sababu angalia! nakaribia kuwainua Wakaldayo - taifa katili na lenye kishindo - wanatembea kupitia upana wa nchi kuteka nyumba zisizo za kwao.
For, lo, I raise up the Chaldeans, that bitter and hasty nation; which march through the breadth of the earth, to possess dwelling places that are not theirs.
7 Wanahofu na kuogopa; hukumu yao na uzuri kutoka kwao unaendelea.
They are terrible and dreadful: their judgment and their dignity proceed from themselves.
8 Farasi wao pia wanambio sana kuliko chui, wepesi sana kuliko mbwa mwitu wa jioni. Farasi wao huwaseta, na wapanda farasi wao wanakuja kutoka mbali - wanapaa kama tai anayewahi kula.
Their horses also are swifter than leopards, and are more fierce than the evening wolves; and their horsemen spread themselves: yea, their horsemen come from far; they fly as an eagle that hasteth to devour.
9 Wote wanakuja kwa vurugu; makundi yao yanakwenda kama upepo wa jangwani, na wanakusanya mateka kama mchanga.
They come all of them for violence; their faces are set eagerly as the east wind; and they gather captives as the sand.
10 Wanawadhihaki wafalme, na viongozi ni dhihaka kwaajili yao. Huicheka kila ngome, maana hurundika mavumbi na kuyaondoa.
Yea, he scoffeth at kings, and princes are a derision unto him: he derideth every strong hold; for he heapeth up dust, and taketh it.
11 Ndipo upepo utapita; itaendelea kupita - watu wenye hatia, ambao uwezo wao ni katika mungu.” Habakuki anamuuliza Yahwe swali lingine
Then shall he sweep by [as] a wind, and shall pass over, and be guilty: [even] he whose might is his god.
12 “Wewe si wa tangu nyakati za zamani, Yahwe Mungu wangu, uliye Mtakatifu? Sisi hatutakufa. Yahwe aliwatenga kwaajili ya hukumu, na ninyi, Mwamba, mmeimarisha kwaajili ya kusahihisha.
Art not thou from everlasting, O LORD my God, mine Holy One? we shall not die. O LORD, thou hast ordained him for judgment; and thou, O Rock, hast established him for correction.
13 Macho yenu ni safi kuangaza juu ya uovu, lakini hamuwezi kuangalia matendo mabaya kwa fadhila; kwa nini mnaangalia kwa upendeleo hivyo juu ambao wanasaliti? Kwanini kunyamaza wakati uovu unameza sana wenye haki zaidi yao?
Thou that art of purer eyes than to behold evil, and that canst not look on perverseness, wherefore lookest thou upon them that deal treacherously, and holdest thy peace when the wicked swalloweth up the man that is more righteous than he;
14 unawafanya watu kama samaki baharini, kama vitu vitambaavyo bila kiongozi juu yao.
and makest men as the fishes of the sea, as the creeping things, that have no ruler over them?
15 Wao wanawaleta wote kwa ndoano; wanawakokota watu kutoka kwenye nyavu za samaki na kuwakusanya kwenye wavu wao. Hii ndiyo sababu wanafurahi na kupiga kelele kwa uchangamfu sana.
He taketh up all of them with the angle, he catcheth them in his net, and gathereth them in his drag: therefore he rejoiceth and is glad.
16 Walakini wanatoa sadaka kwenye nyavu zao za kuvulia na kuchoma ubani kwenye nyavu zao, sababu wanyama wanene ni sehemu yao, na nyama iliyonona ni chakula chao.
Therefore he sacrificeth unto his net, and burneth incense unto his drag; because by them his portion is fat, and his meat plenteous.
17 Kwa sababu hiyo watamaliza nyavu zao za kuvulia na kuendelea kuchicha mataifa, bila kuhisi huruma”?
Shall he therefore empty his net, and not spare to slay the nations continually?