< Habakuki 3 >
1 Maombi ya Habakuki nabii:
A PRAYER OF THE PROPHET AMBACUM, WITH A SONG.
2 Yahwe, nimesikia taarifa zako, na mimi naogopa. Yahwe, fufua kazi yako katikati wakati; katikati ya muda huu; fanya hiyo ijulikane; kumbuka kuwa na rehema katika ghadhabu yako.
O Lord, I have heard your report, and was afraid: I considered your works, and was amazed: you shall be known between the two living creatures, you shall be acknowledged when the years draw near; you shall be manifested when the time is come; when my soul is troubled, you will in wrath remember mercy.
3 Mungu alikuja kutoka Temani, na yule Mtakatifu kutoka Parani. (Sela) Utukufu wake umezifunika mbingu, na dunia ilikuwa imejaa utukufu wake.
God shall come from Thaeman, and the Holy One from the dark shady mount Pharan. (Pause)
4 Miali miwili ya mikono yake ilikuwa iking'aa kama mwanga, ambapo uweza wake ulifichwa.
His excellence covered the heavens, and the earth was full of his praise. And his brightness shall be as light; [there were] horns in his hands, and he caused a mighty love of his strength.
5 Ugonjwa wa kuua ulitangulia mbele yake, na adha iliifuta miguu yake.
Before his face shall go a report, and it shall go forth into the plains,
6 Yeye alisimama na akaipima nchi; aliangalia na aliyatikisa mataifa. Hata milima ya milele iliharibiwa kabisa, na vilima vya milele vilianguka chini. Njia yake ni ya milele.
the earth stood at his feet and trembled: he saw, and the nations melted away: the mountains were violently burst through, the everlasting hills melted at his everlasting going forth.
7 Niliona mahema ya Wakushi katika mateso, na vitambaa vya mahema katika Midiani vinatetema.
Because of troubles I looked upon the tents of the Ethiopians: the tabernacles also of the land of Madiam shall be dismayed.
8 Yahwe alikuwa na hasira pale mtoni? Ghadhabu yako ilikuwa dhidi ya mito, au hasira yako dhidi ya bahari, unapopanda juu ya farasi wenye mikokoteni na wa ushindi wako?
Was you angry, O Lord, with the rivers? or [was] your wrath against the rivers, or your anger against the sea? for you will mount on your horses, and your chariots are salvation.
9 Umeleta upinde wako bila mfuniko; unaweka mishale kwenye upinde wako! (Sela) uliigawa nchi na mito.
Surely you did bend they bow at sceptres, says the Lord. (Pause) The land of rivers shall be torn asunder.
10 Milima ilikuona wewe na kugeuka kwa huzuni. Maji yaliyomwagwa chini yalipita juu yao; kina cha bahari kilipaza sauti. Mawimbi yake yakainuka juu.
The nations shall see you and be in pain, [as you do] divide the moving waters: the deep uttered her voice, and raised her form on high.
11 Jua na mwezi vilisimama imara juu mahali pake katika mwanga wa mishale yako na ilipaa, pale katika uangavu wa mwanga wa mikuki yako.
The sun was exalted, and the moon stood still in her course: your darts shall go forth at the light, at the brightness of the gleaming of your arms.
12 Umetembea juu ya nchi kwa uchungu. Katika ghadhabu umepukuchua mataifa.
You will bring low the land with threatening, and in wrath you will break down the nations.
13 Ulikwenda nje kwaajili ya wokovu wa watu wako, Kwaajili ya wokovu wa mteule wako. Wewe pondaponda kichwa cha nyumba ya mwovu kuweka wazi msingi wa shingo. (Sela)
You went forth for the salvation of your people, to save your anointed: you shall bring death on the heads of transgressors; you has brought bands upon [their] neck. (Pause)
14 Umekichoma kichwa cha wapiganaji wake kwa mshale wake mwenyewe sababu walikuja kama upepo kututawanya sisi, wivu wao ulikuwa kama mtu ambaye anamteketeza masikini katika mahali pamaficho.
You did cut asunder the heads of princes with amazement, they shall tremble in it; they shall burst their bridles, [they shall be] as a poor man devouring in secret.
15 Umesafiri juu ya bahari kwa farasi wako, na kuyapita maji makuu.
And you do cause your horses to enter the sea, disturbing much water.
16 Nilisikia, na ndani yangu nilitetemeka! midomo yangu ilitetemesha sauti. Uozo unakuja katika mifupa yangu, na chini yangu mwenyewe nilitetemeka kama nasubiri kwaajili ya siku ya kuhuzunisha ifike juu ya watu waliotushambulia sisi.
I watched, and my belly trembled at the sound of the prayer of my lips, and trembling entered into my bones, and my frame was troubled within me; I will rest in the day of affliction, from going up to the people of my sojourning.
17 Ingawa mtini hauchipui na hauzai kutokana na mzababibu; na ingawa kuzaa kwa mti wa mzaituni hakuridhishi na mashamba hayatoi chakula; na ingawa kundi mifugo limetoweka na hakuna ng'ombe katika zizi, hiki ndicho nitakacho kifanya.
For [though] the fig tree shall bear no fruit, and there shall be no produce on the vines; the labour of the olive shall fail, and the fields shall produce no food: the sheep have failed from the pasture, and there are no oxen at the cribs;
18 Bado, nitafurahia katika Yahwe. Nitakuwa nafuraha kwa sababu ya Mungu wa wokovu wangu.
yet I will exult in the Lord, I will joy in God my Saviour.
19 Bwana Yahwe ni nguvu yangu na anaifanya miguu yangu kama ya kulungu. Ananifanya mimi niende mbele mahali pangu pa juu. - kufuata maelekezo ya muziki, katika vyombo vyangu vya nyuzi.
The Lord God is my strength, and he will perfectly strengthen my feet; he mounts me upon high places, that I may conquer by his song.