< Habakuki 2 >

1 Nitasimama kwenye nguzo yangu ya ulinzi na kujiweka mwenyewe juu ya mnara wa mlinzi, na nitatazama kwa makini kuona yeye atasema nini kwangu na namna gani nitageuka kutoka kwenye lawama yangu.
On my charge I stand, and I station myself on a bulwark, and I watch to see what He speaks against me, and what I reply to my reproof.
2 Yahwe alinijibu na alisema, “Rekodi maono haya, na uandike dhahiri juu ya kibao ili kwamba anayesoma anaweza kukimbia.
And YHWH answers me and says: “Write a vision, and explain on the tablets, That he may run who is reading it.
3 Sababu maono haya bado ni kwa wakati ujao na hatimaye atazungumza bila kuanguka. Ingawa inachelewa, isubiri. Sababu kwa hakika itatakuja na haitachelewa.
For yet the vision [is] for a season, And it breathes for the end, and does not lie, If it lingers, wait for it, For surely it comes, it is not late.
4 Tazama! yule ambae hamu yake siyo sawa ndani yake anapumua kwa nguvu. Lakini mwenye haki ataishi kwa imani.
Behold, a presumptuous one! His soul is not upright within him, And the righteous lives by his faith.
5 Sababu mvinyo ni msaliti wa kijana mwenye kiburi ili kwamba asistahimili, lakini hukuza tamaa yake kama kaburi na, kama kifo, haitaweza kuridhishwa. Yeye anajikusanyia kila taifa na anakusanya kwaajili yake watu wote. (Sheol h7585)
And also, because the wine [is] treacherous, A man is haughty, and does not remain at home, Who has enlarged his soul as Sheol, And is as death that is not satisfied, And gathers to itself all the nations, And assembles to itself all the peoples, (Sheol h7585)
6 Haya yote hayatatengeneza usemi kumdhihaki na wimbo wa dhihaka unaomhusu, 'ole wake yule aongezaye visivyo vya kwake! kwa muda gani utaongeza uzito wa dhamana uliyochukua?'
Are these not—all of them—an allegory taken up against him, And a moral of acute sayings for him, And say, Woe [to] him who is multiplying [what is] not his? Until when also is he multiplying to himself heavy pledges?
7 Wale wanao ngojea kwako hawatainuka ghafla? na wale wanaokutetemesha kuamka? Utakuwa mwathirika kwaajili yao.
Do your usurers not instantly rise up, And those shaking you awake, And you have been a spoil to them?
8 Kwasababu umeteka nyara watu wengi, mabaki yote ya watu, yatakuteka nyara wewe. Sababu umemwaga damu nyingi za watu na umetenda kwa uasi kinyume cha nchi, miji, na wote wanaokaa ndani yake.
Because you have spoiled many nations, All the remnant of the peoples spoil you, Because of man’s blood, and of violence [to] the land, [To] the city, and [to] all dwelling in it.
9 Ole kwa yule anayechonga mapato maovu kwaajili ya nyumba yake, hivyo anaweza kutengeneza kiota chake juu kumweka yeye salama mbali na mikono ya uovu.
Woe [to] him who is gaining evil gain for his house, To set his nest on high, To be delivered from the hand of evil,
10 Umebuni aibu kwa nyumba yako kwa kuwakata watu wengi, na umefanya dhambi dhidi yako mwenyewe.
You have counseled a shameful thing to your house, To cut off many peoples, and your soul [is] sinful.
11 Sababu jiwe litapaza sauti kutoka ukutani, na pao la mbao litawajibu,
For a stone cries out from the wall, And a beam from the wood answers it.
12 'Ole wake yule ajengaye mji kwa damu, na anayeimarisha mji kwa katika uovu.
Woe [to] him who is building a city by blood, And establishing a city by iniquity.
13 Hii haitoki kwa Yahwe wa majeshi kwamba watu wafanye kazi kwa moto na mataifa yote mengine yanachakaa menyewe bila kitu?
Behold, is it not from YHWH of Hosts And peoples are fatigued for fire, And nations for vanity are weary?
14 Bado nchi itajaa maarifa ya utukufu wa Yahwe kama maji yanavyojaza bahari.
For the earth is full of the knowledge of the glory of YHWH, As the waters cover over a sea.
15 'Ole wake yule anayemfanya jirani yake alewe, wewe ambaye unaye ongeza sumu uwafanye walewe ili uweze kutazama uchi wao.
Woe [to] him who is giving drink to his neighbor, Pouring out your bottle, and also making drunk, In order to look on their nakedness.
16 Utavimbiwa na aibu zaidi kuliko utukufu. Kunywa hiyo vilevile, na funua uchi wako mwenyewe. Kikombe cha mkono wa kuume wa Yahwe utakuja katika kukugeukia wewe, na aibu itafunika heshima yako.
You have been filled—shame without honor, Drink also, and be uncircumcised, Turn around to you does the cup of the right hand of YHWH, And shameful spewing [is] on your glory.
17 Vurugu iliyofanywa kwa Lebanoni itakufunika na uharibifu wa wanyama utakuogopesha. Sababu umemwaga damu za watu na umetenda kwa uasi dhidi ya ile nchi, miji, na wote wanaokaa humo.
For violence [done to] Lebanon covers you, And spoil of beasts frightens them, Because of man’s blood, and of violence [to] the land, [To] the city, and [to] all dwelling in it.
18 Sanamu iliyochongwa inakufaidia nini? Sababu yule aliyeichonga hiyo, au ambaye kaisubu kwa kuiyeyusha metali, ni mwalimu wa uongo; Sababu anaiamini kazi ya mikono yake anapotengeneza miungu hii isiyoongea.
What profit has a carved image given That its former has hewn it? A molten image and teacher of falsehood, That the former has trusted on his own formation—to make mute idols?
19 'Ole kwa yule anayeuambia ubao, Amka! Au kwa jiwe lisiloongea, Inuka!' Vitu hivi vinafundisha? Angalia, hiki juu kimefunikwa kwa dhahabu na fedha, lakini ndani yake hakipumui kabisa.
Woe [to] him who is saying to wood, Awake, To a mute stone, Stir up, It [is] a teacher! Behold, it is overlaid—gold and silver, And there is no spirit in its midst.
20 Lakini Yahwe yumo katika hekalu lake takatifu! Nchi yote iwe kimya mbele zake.
And YHWH [is] in His holy temple, Be silent before Him, all the earth!”

< Habakuki 2 >