< Habakuki 2 >

1 Nitasimama kwenye nguzo yangu ya ulinzi na kujiweka mwenyewe juu ya mnara wa mlinzi, na nitatazama kwa makini kuona yeye atasema nini kwangu na namna gani nitageuka kutoka kwenye lawama yangu.
I will stand upon my watch, and set myself upon the tower, and will look forth to see what he will speak with me, and what I shall answer concerning my complaint.
2 Yahwe alinijibu na alisema, “Rekodi maono haya, na uandike dhahiri juu ya kibao ili kwamba anayesoma anaweza kukimbia.
And Jehovah answered me, and said, Write the vision, and make it plain upon tablets, that he may run who reads it.
3 Sababu maono haya bado ni kwa wakati ujao na hatimaye atazungumza bila kuanguka. Ingawa inachelewa, isubiri. Sababu kwa hakika itatakuja na haitachelewa.
For the vision is yet for the appointed time, and it hastens toward the end, and shall not lie. Though it tarry, wait for it, because it will surely come. It will not delay.
4 Tazama! yule ambae hamu yake siyo sawa ndani yake anapumua kwa nguvu. Lakini mwenye haki ataishi kwa imani.
Behold, his soul is puffed up; it is not upright in him. (But the righteous man shall live by his faith.
5 Sababu mvinyo ni msaliti wa kijana mwenye kiburi ili kwamba asistahimili, lakini hukuza tamaa yake kama kaburi na, kama kifo, haitaweza kuridhishwa. Yeye anajikusanyia kila taifa na anakusanya kwaajili yake watu wote. (Sheol h7585)
Yea, moreover, wine is treacherous.) He is a haughty man, who does not keep at home, who enlarges his desire as Sheol, and he is as death, and cannot be satisfied, but gathers to him all nations, and heaps to him all peoples. (Sheol h7585)
6 Haya yote hayatatengeneza usemi kumdhihaki na wimbo wa dhihaka unaomhusu, 'ole wake yule aongezaye visivyo vya kwake! kwa muda gani utaongeza uzito wa dhamana uliyochukua?'
Shall not all these take up a derision against him, and a taunting proverb against him, and say, Woe to him who increases that which is not his (how long?) and who loads himself with pledges!
7 Wale wanao ngojea kwako hawatainuka ghafla? na wale wanaokutetemesha kuamka? Utakuwa mwathirika kwaajili yao.
Shall they not rise up suddenly that shall bite thee, and awake that shall vex thee. And thou shall be for booty to them?
8 Kwasababu umeteka nyara watu wengi, mabaki yote ya watu, yatakuteka nyara wewe. Sababu umemwaga damu nyingi za watu na umetenda kwa uasi kinyume cha nchi, miji, na wote wanaokaa ndani yake.
Because thou have plundered many nations, all the remnant of the peoples shall plunder thee, because of men's blood, and for the violence done to the land, to the city and to all who dwell therein.
9 Ole kwa yule anayechonga mapato maovu kwaajili ya nyumba yake, hivyo anaweza kutengeneza kiota chake juu kumweka yeye salama mbali na mikono ya uovu.
Woe to him who gets an evil gain for his house, that he may set his nest on high, that he may be delivered from the hand of evil!
10 Umebuni aibu kwa nyumba yako kwa kuwakata watu wengi, na umefanya dhambi dhidi yako mwenyewe.
Thou have devised shame to thy house, by cutting off many peoples, and have sinned against thy soul.
11 Sababu jiwe litapaza sauti kutoka ukutani, na pao la mbao litawajibu,
For the stone shall cry out of the wall, and the beam out of the timber shall answer it.
12 'Ole wake yule ajengaye mji kwa damu, na anayeimarisha mji kwa katika uovu.
Woe to him who builds a town with blood, and establishes a city by iniquity!
13 Hii haitoki kwa Yahwe wa majeshi kwamba watu wafanye kazi kwa moto na mataifa yote mengine yanachakaa menyewe bila kitu?
Behold, is it not of Jehovah of hosts that the peoples labor for the fire, and the nations weary themselves for vanity?
14 Bado nchi itajaa maarifa ya utukufu wa Yahwe kama maji yanavyojaza bahari.
For the earth shall be filled with the knowledge of the glory of Jehovah, as the waters cover the sea.
15 'Ole wake yule anayemfanya jirani yake alewe, wewe ambaye unaye ongeza sumu uwafanye walewe ili uweze kutazama uchi wao.
Woe to him who gives his neighbor drink, who adds thy venom, and also makes him drunken, that thou may look on their nakedness!
16 Utavimbiwa na aibu zaidi kuliko utukufu. Kunywa hiyo vilevile, na funua uchi wako mwenyewe. Kikombe cha mkono wa kuume wa Yahwe utakuja katika kukugeukia wewe, na aibu itafunika heshima yako.
Thou are filled with shame, and not glory. Drink thou also, and be as one uncircumcised. The cup of Jehovah's right hand shall come around to thee, and foul shame shall be upon thy glory.
17 Vurugu iliyofanywa kwa Lebanoni itakufunika na uharibifu wa wanyama utakuogopesha. Sababu umemwaga damu za watu na umetenda kwa uasi dhidi ya ile nchi, miji, na wote wanaokaa humo.
For the violence done to Lebanon shall cover thee and the plunder of the beasts (which made them afraid), because of men's blood, and for the violence done to the land, to the city and to all who dwell therein.
18 Sanamu iliyochongwa inakufaidia nini? Sababu yule aliyeichonga hiyo, au ambaye kaisubu kwa kuiyeyusha metali, ni mwalimu wa uongo; Sababu anaiamini kazi ya mikono yake anapotengeneza miungu hii isiyoongea.
What profits the graven image, that the maker of it has engraved it, the molten image, even the teacher of lies, that he who fashions its form trusts in it, to make dumb idols?
19 'Ole kwa yule anayeuambia ubao, Amka! Au kwa jiwe lisiloongea, Inuka!' Vitu hivi vinafundisha? Angalia, hiki juu kimefunikwa kwa dhahabu na fedha, lakini ndani yake hakipumui kabisa.
Woe to him who says to the wood, Awake, to the dumb stone, Arise! Shall this teach? Behold, it is overlaid with gold and silver, and there is no breath at all in the midst of it.
20 Lakini Yahwe yumo katika hekalu lake takatifu! Nchi yote iwe kimya mbele zake.
But Jehovah is in his holy temple. Let all the earth keep silence before him.

< Habakuki 2 >