< Mwanzo 9 >
1 Kisha Mungu akambariki Nuhu na wanawe, na kuwaambia, “Zaeni, mkaongezeke, na muijaze nchi.
Dios bendijo a Noé y a sus hijos y les dijo: “Sed fecundos, multiplicaos y llenad la tierra.
2 Hofu na utisho wenu vitakuwa juu ya kila mnyama aliye hai juu ya nchi, juu ya kila ndege wa angani, juu ya kila kitu kiendacho chini juu ya ardhi, na juu ya samaki wote wa baharini. Vimetolewa katika mikono yenu.
El temor y el miedo a vosotros recaerán sobre todos los animales de la tierra y sobre todas las aves del cielo. Todo lo que se mueve por la tierra, y todos los peces del mar, serán entregados en tu mano.
3 Kila kitu kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula kwa ajili yenu. Kama nilivyo wapa mimea, sasa nawapa kila kitu.
Todo lo que se mueve y vive será alimento para ti. Así como te di la hierba verde, te he dado todo.
4 Lakini msile nyama pamoja na uhai wake - yaani damu yake - ndani yake.
Pero la carne con vida, es decir, su sangre, no la comeréis.
5 Lakini kwa ajili ya damu yenu, uhai uliomo katika damu yenu nitataka malipo. Kutoka katika mkono wa kila mnyama nitaitaka. Kutoka katika mkono wa kila mtu, yaani, kutoka katika mkono wa yule ambaye amemuua ndugu yake, nitataka fidia kwa ajili ya uhai wa mtu huyo.
Ciertamente pediré cuentas por la sangre de tu vida. A la mano de todo animal se la exigiré. A la mano del hombre, incluso a la mano del hermano de todo hombre, le exigiré la vida del hombre.
6 Yeyote amwagaye damu ya mtu, kwa njia ya mtu damu yake itamwagwa, kwa sababu ilikuwa ni katika mfano wa Mungu kwamba Mungu alimuumba mtu.
El que derrame sangre de hombre, su sangre será derramada por el hombre, porque Dios hizo al hombre a su imagen y semejanza.
7 Na hivyo nanyi zaeni na kuongezeka, sambaeni katika inchi yote na muongezeke juu yake.”
Sed fecundos y multiplicaos. Creced en abundancia en la tierra y multiplicaos en ella”.
8 Kisha Mungu akazungumza na Nuhu na wanae pamoja naye, akisema,
Dios habló a Noé y a sus hijos con él, diciendo:
9 “Kwa ajili yangu, sikiliza! Ninakwenda kulithibitisha agano langu pamoja nawe na uzao wenu baada yenu,
“En cuanto a mí, he aquí que yo establezco mi pacto con vosotros, y con vuestra descendencia después de vosotros,
10 na kwa kila kiumbe hai kilicho pamoja nawe, pamoja na ndege, mnyama wa kufugwa, na kila kiumbe cha nchi pamoja nawe, kuanzia kwa wote waliotoka kwenye safina, mpaka kwa kila kiumbe hai juu ya nchi.
y con toda criatura viviente que está con vosotros: las aves, el ganado y todo animal de la tierra con vosotros, de todos los que salen de la nave, todo animal de la tierra.
11 Kwa sababu hii ninalithibitisha agano langu pamoja nanyi, kwamba hapatatokea kuangamizwa kwa mwenye mwili kwa njia ya maji ya gharika. Tena hapatatokea gharika ya kuangamiza nchi.”
Estableceré mi pacto con vosotros: Toda la carne no volverá a ser eliminada por las aguas del diluvio. Nunca más habrá un diluvio que destruya la tierra”.
12 Mungu akasema, “na hii ndiyo ishara ya agano ambalo ninafanya kati yangu na ninyi pamoja na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, kwa vizazi vyote vya baadaye:
Dios dijo: “Esta es la señal de la alianza que hago entre ustedes y yo, y toda criatura viviente que está con ustedes, por generaciones perpetuas:
13 Nimeweka upinde wangu wa mvua katika wingu, na itakuwa ndiyo ishara ya agano kati yangu na nchi.
Yo pongo mi arco iris en la nube, y será una señal de alianza entre la tierra y yo.
14 Hata itakuwa nitakapoleta wingu juu ya nchi na upinde wa mvua ukaonekana katika wingu,
Cuando traiga una nube sobre la tierra, para que el arco iris se vea en la nube,
15 ndipo nitakumbuka agano langu, ambalo ni kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai cha wote mwenye mwili. Maji hayatafanyika tena gharika kuharibu wote wenye mwili.
me acordaré de mi pacto, que es entre yo y vosotros y toda criatura viviente de toda carne, y las aguas no se convertirán más en un diluvio para destruir toda carne.
16 Upinde wa mvua utakuwa katika mawingu na nitauona, ili kukumbuka agano la milele kati ya Mungu na kila kiumbe hai cha wote wenye mwili ambacho kiko juu ya nchi.”
El arco iris estará en la nube. Lo miraré para acordarme del pacto eterno entre Dios y toda criatura viviente de toda carne que está en la tierra.”
17 Kisha Mungu akamwambia Nuhu, “Hii ni ishara ya agano ambalo nimelithibitisha kati yangu na wenye mwili wote ambao wako juu ya nchi.”
Dios dijo a Noé: “Esta es la señal de la alianza que he establecido entre yo y toda la carne que está sobre la tierra.”
18 Wana wa Nuhu ambao walitoka katika safina walikuwa ni Shemu, Hamu, na Yafethi. Na Hamu akamzaa kanaani.
Los hijos de Noé que salieron de la nave fueron Sem, Cam y Jafet. Cam es el padre de Canaán.
19 Watatu hawa walikuwa ndio wana wa Nuhu, na kutokea kwa hawa nchi yote ikajaa watu.
Estos tres fueron los hijos de Noé, y de ellos se pobló toda la tierra.
20 Nuhu akaanza kuwa mkulima, na akapanda mizabibu.
Noé comenzó a ser agricultor y plantó una viña.
21 Akanywa sehemu ya divai na akalewa. Akawa amelala hemeani uchi.
Bebió del vino y se emborrachó. Se descubrió dentro de su tienda.
22 Kisha Hamu, baba yake na Kanaani, akaona uchi wa baba yake na akawaambia ndugu zake wawili waliokuwa nje.
Cam, el padre de Canaán, vio la desnudez de su padre y se lo dijo a sus dos hermanos que estaban fuera.
23 Kwa hiyo Shemu na Yafethi wakachukua kanzu wakaitanda juu ya mabega yao, na wakatembea kinyumenyume na wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zikiwa zimegeuka nyuma upande mwingine, kwa hiyo hawakuona uchi wa baba yao.
Sem y Jafet tomaron una prenda de vestir, se la pusieron sobre los hombros de ambos, entraron de espaldas y cubrieron la desnudez de su padre. Sus rostros estaban al revés, y no vieron la desnudez de su padre.
24 Nuhu alipozinduka kutoka katika ulevi wake, alijua ni jambo gani mtoto wake mdogo amemfanyia.
Noé despertó de su vino y supo lo que su hijo menor le había hecho.
25 Hivyo akasema, “Alaaniwe Kanaani. Na awe mtumishi kwa watumishi wa ndugu zake.”
Dijo, “Canaán está maldito. Será siervo de los siervos de sus hermanos”.
26 Akasema pia, Yahwe, Mungu wa Shemu, abarikiwe, Kanaani na awe mtumwa wake.
Él dijo, “Bendito sea Yahvé, el Dios de Sem. Que Canaán sea su siervo.
27 Mungu na apanuwe mipaka ya Yafethi, na afanye makazi yake katika hema za Shemu. Kanaani na awe mtumwa wake.”
Que Dios engrandezca a Jafet. Que habite en las tiendas de Sem. Que Canaán sea su siervo”.
28 Baada ya gharika, Nuhu aliishi miaka miatatu na hamsini.
Noé vivió trescientos cincuenta años después del diluvio.
29 Siku zote za Nuhu zilikuwa ni miaka mia tisa na hamsini, na kisha alikufa.
Todos los días de Noé fueron novecientos cincuenta años, y luego murió.