< Mwanzo 9 >
1 Kisha Mungu akambariki Nuhu na wanawe, na kuwaambia, “Zaeni, mkaongezeke, na muijaze nchi.
And God blessed Noe and his sonnes and sayd vnto them: Increase and multiplye and fyll the erth.
2 Hofu na utisho wenu vitakuwa juu ya kila mnyama aliye hai juu ya nchi, juu ya kila ndege wa angani, juu ya kila kitu kiendacho chini juu ya ardhi, na juu ya samaki wote wa baharini. Vimetolewa katika mikono yenu.
The feare also and drede of yow be vppon all beastes of the erth and vppon all foules of the ayre ad vppon all that crepeth on the erth and vppon all fyshes of the see which are geven vnto youre handes
3 Kila kitu kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula kwa ajili yenu. Kama nilivyo wapa mimea, sasa nawapa kila kitu.
And all that moveth vppon the erth havynge lyfe shall be youre meate: Euen as ye grene herbes so geue I yow all thynge.
4 Lakini msile nyama pamoja na uhai wake - yaani damu yake - ndani yake.
Only the flesh with his life which is his bloud se that ye eate not.
5 Lakini kwa ajili ya damu yenu, uhai uliomo katika damu yenu nitataka malipo. Kutoka katika mkono wa kila mnyama nitaitaka. Kutoka katika mkono wa kila mtu, yaani, kutoka katika mkono wa yule ambaye amemuua ndugu yake, nitataka fidia kwa ajili ya uhai wa mtu huyo.
For verely the bloude of yow wherein youre lyves are wyll I requyre: Eue of the hande of all beastes wyll I requyre it And of the hande of man and of the hand off euery mannes brother wyll I requyre the lyfe of man:
6 Yeyote amwagaye damu ya mtu, kwa njia ya mtu damu yake itamwagwa, kwa sababu ilikuwa ni katika mfano wa Mungu kwamba Mungu alimuumba mtu.
so yt he which shedeth mannes bloude shall haue hys bloud shed by man agayne: for God made man after his awne lycknesse.
7 Na hivyo nanyi zaeni na kuongezeka, sambaeni katika inchi yote na muongezeke juu yake.”
See that ye encrease and waxe and be occupyde vppon the erth and multiplye therein.
8 Kisha Mungu akazungumza na Nuhu na wanae pamoja naye, akisema,
Farthermore God spake vnto Noe and to hys sonnes wyth hym saynge:
9 “Kwa ajili yangu, sikiliza! Ninakwenda kulithibitisha agano langu pamoja nawe na uzao wenu baada yenu,
see I make my bod wyth you and youre seed after you
10 na kwa kila kiumbe hai kilicho pamoja nawe, pamoja na ndege, mnyama wa kufugwa, na kila kiumbe cha nchi pamoja nawe, kuanzia kwa wote waliotoka kwenye safina, mpaka kwa kila kiumbe hai juu ya nchi.
and wyth all lyvynge thinge that is wyth you: both foule and catell and all maner beste of the erth that is wyth yow of all that commeth out of the arke what soeuer beste of the erth it be.
11 Kwa sababu hii ninalithibitisha agano langu pamoja nanyi, kwamba hapatatokea kuangamizwa kwa mwenye mwili kwa njia ya maji ya gharika. Tena hapatatokea gharika ya kuangamiza nchi.”
I make my bonde wyth yow that hence forth all flesh shall not be destroyed wyth yt waters of any floud ad yt hence forth there shall not be a floud to destroy the erth.
12 Mungu akasema, “na hii ndiyo ishara ya agano ambalo ninafanya kati yangu na ninyi pamoja na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, kwa vizazi vyote vya baadaye:
And God sayd. This is the token of my bode which I make betwene me and yow ad betwene all lyvynge thyng that is with yow for ever:
13 Nimeweka upinde wangu wa mvua katika wingu, na itakuwa ndiyo ishara ya agano kati yangu na nchi.
I wyll sette my bowe in the cloudes and it shall be a sygne of the appoyntment made betwene me and the erth:
14 Hata itakuwa nitakapoleta wingu juu ya nchi na upinde wa mvua ukaonekana katika wingu,
So that when I brynge in cloudes vpo ye erth the bowe shall appere in ye cloudes.
15 ndipo nitakumbuka agano langu, ambalo ni kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai cha wote mwenye mwili. Maji hayatafanyika tena gharika kuharibu wote wenye mwili.
And than wyll I thynke vppon my testament which I haue made betwene me and yow and all that lyveth what soeuer flesh it be. So that henceforth there shall be no more waters to make a floud to destroy all flesh.
16 Upinde wa mvua utakuwa katika mawingu na nitauona, ili kukumbuka agano la milele kati ya Mungu na kila kiumbe hai cha wote wenye mwili ambacho kiko juu ya nchi.”
The bowe shalbe in the cloudes and I wyll loke vpon it to remembre the euerlastynge testament betwene God and all that lyveth vppon the erth what soeuer flesh it be.
17 Kisha Mungu akamwambia Nuhu, “Hii ni ishara ya agano ambalo nimelithibitisha kati yangu na wenye mwili wote ambao wako juu ya nchi.”
And God sayd vnto Noe: This is the sygne of the testament which I have made betwene me and all flesh yt is on the erth.
18 Wana wa Nuhu ambao walitoka katika safina walikuwa ni Shemu, Hamu, na Yafethi. Na Hamu akamzaa kanaani.
The sonnes of Noe that came out of the arke were: Sem Ham and Iapheth. And Ham he is the father of Canaa.
19 Watatu hawa walikuwa ndio wana wa Nuhu, na kutokea kwa hawa nchi yote ikajaa watu.
These are the. iij. sonnes of Noe and of these was all the world overspred.
20 Nuhu akaanza kuwa mkulima, na akapanda mizabibu.
And Noe beynge an husbad man went furth and planted a vyneyarde
21 Akanywa sehemu ya divai na akalewa. Akawa amelala hemeani uchi.
and drancke of the wyne and was droncke and laye vncouered in the myddest of his tet.
22 Kisha Hamu, baba yake na Kanaani, akaona uchi wa baba yake na akawaambia ndugu zake wawili waliokuwa nje.
And Ham the father of Canaan sawe his fathers prevytees and tolde his ij. brethren that were wythout.
23 Kwa hiyo Shemu na Yafethi wakachukua kanzu wakaitanda juu ya mabega yao, na wakatembea kinyumenyume na wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zikiwa zimegeuka nyuma upande mwingine, kwa hiyo hawakuona uchi wa baba yao.
And Sem and Iapheth toke a mantell and put it on both there shulders ad went backward ad covered there fathers secrets but there faces were backward So that they sawe not there fathers nakydnes.
24 Nuhu alipozinduka kutoka katika ulevi wake, alijua ni jambo gani mtoto wake mdogo amemfanyia.
As soone as Noe was awaked fro his wyne and wyst what his yongest sonne had done vnto hym
25 Hivyo akasema, “Alaaniwe Kanaani. Na awe mtumishi kwa watumishi wa ndugu zake.”
he sayd: cursed be Canaan ad a seruante, of all seruantes be he to his brethren.
26 Akasema pia, Yahwe, Mungu wa Shemu, abarikiwe, Kanaani na awe mtumwa wake.
And he sayd: Blessed be the LORde God of Se and Canaan be his seruante.
27 Mungu na apanuwe mipaka ya Yafethi, na afanye makazi yake katika hema za Shemu. Kanaani na awe mtumwa wake.”
God increase Iapheth that he may dwelle in the tentes of Sem. And Canaan be their seruante.
28 Baada ya gharika, Nuhu aliishi miaka miatatu na hamsini.
And Noe lyved after the floude. iij. hundred and. l. yere:
29 Siku zote za Nuhu zilikuwa ni miaka mia tisa na hamsini, na kisha alikufa.
So that all the dayes of Noe were ix. hundred and. l. yere ad than he dyed.