< Mwanzo 9 >
1 Kisha Mungu akambariki Nuhu na wanawe, na kuwaambia, “Zaeni, mkaongezeke, na muijaze nchi.
Then God blessed Noah and his sons, saying to them, “I want you to have many children who will live all over the earth.
2 Hofu na utisho wenu vitakuwa juu ya kila mnyama aliye hai juu ya nchi, juu ya kila ndege wa angani, juu ya kila kitu kiendacho chini juu ya ardhi, na juu ya samaki wote wa baharini. Vimetolewa katika mikono yenu.
All the wild animals on the earth and all the birds, all the creatures that scurry across the ground, and all the fish, will be very afraid [DOU] of you. I have put them under your control.
3 Kila kitu kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula kwa ajili yenu. Kama nilivyo wapa mimea, sasa nawapa kila kitu.
Just as I previously said you could eat green plants for food, now I am saying you can eat everything that lives and moves.
4 Lakini msile nyama pamoja na uhai wake - yaani damu yake - ndani yake.
[It is blood that causes creatures to be alive], therefore you must not eat meat that still has blood in it after the animal is killed. [After you have drained the blood out, you may cook it and eat it].
5 Lakini kwa ajili ya damu yenu, uhai uliomo katika damu yenu nitataka malipo. Kutoka katika mkono wa kila mnyama nitaitaka. Kutoka katika mkono wa kila mtu, yaani, kutoka katika mkono wa yule ambaye amemuua ndugu yake, nitataka fidia kwa ajili ya uhai wa mtu huyo.
I insist that murderers must be executed. Animals that kill people must also be executed. The reason that everyone who murders someone else must be executed is that
6 Yeyote amwagaye damu ya mtu, kwa njia ya mtu damu yake itamwagwa, kwa sababu ilikuwa ni katika mfano wa Mungu kwamba Mungu alimuumba mtu.
I made people to be like myself [in many ways]. So someone who murders another human being must be executed by others, [because he killed someone who is like me].
7 Na hivyo nanyi zaeni na kuongezeka, sambaeni katika inchi yote na muongezeke juu yake.”
As for you, I want you to produce many children, in order that they and their descendants may live all over the earth.”
8 Kisha Mungu akazungumza na Nuhu na wanae pamoja naye, akisema,
God also said to Noah and his sons,
9 “Kwa ajili yangu, sikiliza! Ninakwenda kulithibitisha agano langu pamoja nawe na uzao wenu baada yenu,
“Listen carefully. I am now making a solemn promise to you and with your descendants,
10 na kwa kila kiumbe hai kilicho pamoja nawe, pamoja na ndege, mnyama wa kufugwa, na kila kiumbe cha nchi pamoja nawe, kuanzia kwa wote waliotoka kwenye safina, mpaka kwa kila kiumbe hai juu ya nchi.
and with all the living creatures that are with you—including the birds, the livestock, and the wild animals—every living creature on the earth that came out of the boat with you.
11 Kwa sababu hii ninalithibitisha agano langu pamoja nanyi, kwamba hapatatokea kuangamizwa kwa mwenye mwili kwa njia ya maji ya gharika. Tena hapatatokea gharika ya kuangamiza nchi.”
This is the promise that I am making to you: I will never again destroy all living creatures by a flood, or destroy everything else on the earth by a flood.”
12 Mungu akasema, “na hii ndiyo ishara ya agano ambalo ninafanya kati yangu na ninyi pamoja na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, kwa vizazi vyote vya baadaye:
Then God said to him, “This is the sign to guarantee that I will keep the promise that I am making to you and to all living creatures, a promise that I will keep forever:
13 Nimeweka upinde wangu wa mvua katika wingu, na itakuwa ndiyo ishara ya agano kati yangu na nchi.
[From time to time] I will put a rainbow in the sky. It will remind me of my promise that I have made to you and everything on the earth.
14 Hata itakuwa nitakapoleta wingu juu ya nchi na upinde wa mvua ukaonekana katika wingu,
When I cause rain to fall from the clouds, and a rainbow appears in the sky,
15 ndipo nitakumbuka agano langu, ambalo ni kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai cha wote mwenye mwili. Maji hayatafanyika tena gharika kuharibu wote wenye mwili.
it will remind me about the promise that I have made to you and all living creatures, my promise that there will never again be a flood that will destroy all living creatures.
16 Upinde wa mvua utakuwa katika mawingu na nitauona, ili kukumbuka agano la milele kati ya Mungu na kila kiumbe hai cha wote wenye mwili ambacho kiko juu ya nchi.”
Whenever there is a rainbow in the sky, I will see it, and I will think about the promise that I have made to every living creature that is upon the earth, a promise that I will keep forever.”
17 Kisha Mungu akamwambia Nuhu, “Hii ni ishara ya agano ambalo nimelithibitisha kati yangu na wenye mwili wote ambao wako juu ya nchi.”
Then God said to Noah, “The rainbow will be the sign of the promise that I have made to all the creatures that live on the earth.”
18 Wana wa Nuhu ambao walitoka katika safina walikuwa ni Shemu, Hamu, na Yafethi. Na Hamu akamzaa kanaani.
The sons of Noah who came out of the boat were Shem, Ham, and Japheth. Ham later became the father of Canaan.
19 Watatu hawa walikuwa ndio wana wa Nuhu, na kutokea kwa hawa nchi yote ikajaa watu.
All the people on the earth are descended from those three sons of Noah.
20 Nuhu akaanza kuwa mkulima, na akapanda mizabibu.
Noah was a farmer. He planted grapevines.
21 Akanywa sehemu ya divai na akalewa. Akawa amelala hemeani uchi.
[When they later produced grapes, he made wine from the grapes]. One day, when he drank too much of the wine, he became drunk, and he lay naked in his tent.
22 Kisha Hamu, baba yake na Kanaani, akaona uchi wa baba yake na akawaambia ndugu zake wawili waliokuwa nje.
Ham, the father of Canaan, saw his father lying naked in the tent. So he went outside and told his two older brothers what he had seen.
23 Kwa hiyo Shemu na Yafethi wakachukua kanzu wakaitanda juu ya mabega yao, na wakatembea kinyumenyume na wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zikiwa zimegeuka nyuma upande mwingine, kwa hiyo hawakuona uchi wa baba yao.
Then Shem and Japheth took a large cloth and placed it across their backs, and walked backwards into the tent. They covered their father’s naked body with the cloth. Their faces were turned away from their father, so they did not see him naked.
24 Nuhu alipozinduka kutoka katika ulevi wake, alijua ni jambo gani mtoto wake mdogo amemfanyia.
When Noah woke up [and was sober again], he found out how wrongfully Ham, his youngest son, had behaved toward him.
25 Hivyo akasema, “Alaaniwe Kanaani. Na awe mtumishi kwa watumishi wa ndugu zake.”
He said, “I am cursing Ham’s youngest son, Canaan, and his descendants. They will be like slaves to their uncles.
26 Akasema pia, Yahwe, Mungu wa Shemu, abarikiwe, Kanaani na awe mtumwa wake.
I will ask God to enlarge the territory that belongs to Japheth, and allow his descendants to live peacefully among the descendants of Shem [MTY].
27 Mungu na apanuwe mipaka ya Yafethi, na afanye makazi yake katika hema za Shemu. Kanaani na awe mtumwa wake.”
And I desire that Canaan’s descendants will be like slaves of Japheth’s descendants.”
28 Baada ya gharika, Nuhu aliishi miaka miatatu na hamsini.
Noah lived 350 more years after the flood.
29 Siku zote za Nuhu zilikuwa ni miaka mia tisa na hamsini, na kisha alikufa.
He died when he was 950 years old.