< Mwanzo 9 >
1 Kisha Mungu akambariki Nuhu na wanawe, na kuwaambia, “Zaeni, mkaongezeke, na muijaze nchi.
and to bless God [obj] Noah and [obj] son: child his and to say to/for them be fruitful and to multiply and to fill [obj] [the] land: country/planet
2 Hofu na utisho wenu vitakuwa juu ya kila mnyama aliye hai juu ya nchi, juu ya kila ndege wa angani, juu ya kila kitu kiendacho chini juu ya ardhi, na juu ya samaki wote wa baharini. Vimetolewa katika mikono yenu.
and fear your and terror your to be upon all living thing [the] land: country/planet and upon all bird [the] heaven in/on/with all which to creep [the] land: soil and in/on/with all fish [the] sea in/on/with hand your to give: give
3 Kila kitu kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula kwa ajili yenu. Kama nilivyo wapa mimea, sasa nawapa kila kitu.
all creeping which he/she/it alive to/for you to be to/for food like/as green vegetation to give: give to/for you [obj] all
4 Lakini msile nyama pamoja na uhai wake - yaani damu yake - ndani yake.
surely flesh in/on/with soul: life his blood his not to eat
5 Lakini kwa ajili ya damu yenu, uhai uliomo katika damu yenu nitataka malipo. Kutoka katika mkono wa kila mnyama nitaitaka. Kutoka katika mkono wa kila mtu, yaani, kutoka katika mkono wa yule ambaye amemuua ndugu yake, nitataka fidia kwa ajili ya uhai wa mtu huyo.
and surely [obj] blood your to/for soul: life your to seek from hand: to all living thing to seek him and from hand: to [the] man from hand: to man: anyone brother: compatriot his to seek [obj] soul: life [the] man
6 Yeyote amwagaye damu ya mtu, kwa njia ya mtu damu yake itamwagwa, kwa sababu ilikuwa ni katika mfano wa Mungu kwamba Mungu alimuumba mtu.
to pour: kill blood [the] man in/on/with man blood his to pour: kill for in/on/with image God to make [obj] [the] man
7 Na hivyo nanyi zaeni na kuongezeka, sambaeni katika inchi yote na muongezeke juu yake.”
and you(m. p.) be fruitful and to multiply to swarm in/on/with land: country/planet and to multiply in/on/with her
8 Kisha Mungu akazungumza na Nuhu na wanae pamoja naye, akisema,
and to say God to(wards) Noah and to(wards) son: child his with him to/for to say
9 “Kwa ajili yangu, sikiliza! Ninakwenda kulithibitisha agano langu pamoja nawe na uzao wenu baada yenu,
and I look! I to arise: establish [obj] covenant my with you and with seed: children your after you
10 na kwa kila kiumbe hai kilicho pamoja nawe, pamoja na ndege, mnyama wa kufugwa, na kila kiumbe cha nchi pamoja nawe, kuanzia kwa wote waliotoka kwenye safina, mpaka kwa kila kiumbe hai juu ya nchi.
and with all soul: animal [the] alive which with you in/on/with bird in/on/with animal and in/on/with all living thing [the] land: country/planet with you from all to come out: come [the] ark to/for all living thing [the] land: country/planet
11 Kwa sababu hii ninalithibitisha agano langu pamoja nanyi, kwamba hapatatokea kuangamizwa kwa mwenye mwili kwa njia ya maji ya gharika. Tena hapatatokea gharika ya kuangamiza nchi.”
and to arise: establish [obj] covenant my with you and not to cut: eliminate all flesh still from water [the] flood and not to be still flood to/for to ruin [the] land: country/planet
12 Mungu akasema, “na hii ndiyo ishara ya agano ambalo ninafanya kati yangu na ninyi pamoja na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, kwa vizazi vyote vya baadaye:
and to say God this sign: indicator [the] covenant which I to give: make between me and between you and between all soul: animal alive which with you to/for generation forever: enduring
13 Nimeweka upinde wangu wa mvua katika wingu, na itakuwa ndiyo ishara ya agano kati yangu na nchi.
[obj] bow my to give: put in/on/with cloud and to be to/for sign: indicator covenant between me and between [the] land: country/planet
14 Hata itakuwa nitakapoleta wingu juu ya nchi na upinde wa mvua ukaonekana katika wingu,
and to be in/on/with to cloud I cloud upon [the] land: country/planet and to see: see [the] bow in/on/with cloud
15 ndipo nitakumbuka agano langu, ambalo ni kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai cha wote mwenye mwili. Maji hayatafanyika tena gharika kuharibu wote wenye mwili.
and to remember [obj] covenant my which between me and between you and between all soul: animal alive in/on/with all flesh and not to be still [the] water to/for flood to/for to ruin all flesh
16 Upinde wa mvua utakuwa katika mawingu na nitauona, ili kukumbuka agano la milele kati ya Mungu na kila kiumbe hai cha wote wenye mwili ambacho kiko juu ya nchi.”
and to be [the] bow in/on/with cloud and to see: see her to/for to remember covenant forever: enduring between God and between all soul: animal alive in/on/with all flesh which upon [the] land: country/planet
17 Kisha Mungu akamwambia Nuhu, “Hii ni ishara ya agano ambalo nimelithibitisha kati yangu na wenye mwili wote ambao wako juu ya nchi.”
and to say God to(wards) Noah this sign: indicator [the] covenant which to arise: establish between me and between all flesh which upon [the] land: country/planet
18 Wana wa Nuhu ambao walitoka katika safina walikuwa ni Shemu, Hamu, na Yafethi. Na Hamu akamzaa kanaani.
and to be son: child Noah [the] to come out: come from [the] ark Shem and Ham and Japheth and Ham he/she/it father Canaan
19 Watatu hawa walikuwa ndio wana wa Nuhu, na kutokea kwa hawa nchi yote ikajaa watu.
three these son: child Noah and from these to disperse all [the] land: country/planet
20 Nuhu akaanza kuwa mkulima, na akapanda mizabibu.
and to profane/begin: begin Noah man [the] land: soil and to plant vineyard
21 Akanywa sehemu ya divai na akalewa. Akawa amelala hemeani uchi.
and to drink from [the] wine and be drunk and to reveal: uncover in/on/with midst (tent his *Q(K)*)
22 Kisha Hamu, baba yake na Kanaani, akaona uchi wa baba yake na akawaambia ndugu zake wawili waliokuwa nje.
and to see: see Ham father Canaan [obj] nakedness father his and to tell to/for two brother: male-sibling his in/on/with outside
23 Kwa hiyo Shemu na Yafethi wakachukua kanzu wakaitanda juu ya mabega yao, na wakatembea kinyumenyume na wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zikiwa zimegeuka nyuma upande mwingine, kwa hiyo hawakuona uchi wa baba yao.
and to take: take Shem and Japheth [obj] [the] mantle and to set: put upon shoulder two their and to go: walk backwards and to cover [obj] nakedness father their and face their backwards and nakedness father their not to see: see
24 Nuhu alipozinduka kutoka katika ulevi wake, alijua ni jambo gani mtoto wake mdogo amemfanyia.
and to awake Noah from wine his and to know [obj] which to make: do to/for him son: child his [the] small
25 Hivyo akasema, “Alaaniwe Kanaani. Na awe mtumishi kwa watumishi wa ndugu zake.”
and to say to curse Canaan servant/slave servant/slave to be to/for brother: male-sibling his
26 Akasema pia, Yahwe, Mungu wa Shemu, abarikiwe, Kanaani na awe mtumwa wake.
and to say to bless LORD God Shem and to be Canaan servant/slave to/for them
27 Mungu na apanuwe mipaka ya Yafethi, na afanye makazi yake katika hema za Shemu. Kanaani na awe mtumwa wake.”
to open wide God to/for Japheth and to dwell in/on/with tent Shem and to be Canaan servant/slave to/for them
28 Baada ya gharika, Nuhu aliishi miaka miatatu na hamsini.
and to live Noah after [the] flood three hundred year and fifty year
29 Siku zote za Nuhu zilikuwa ni miaka mia tisa na hamsini, na kisha alikufa.
and to be all day Noah nine hundred year and fifty year and to die