< Mwanzo 9 >
1 Kisha Mungu akambariki Nuhu na wanawe, na kuwaambia, “Zaeni, mkaongezeke, na muijaze nchi.
God blessed Noah and his sons, and told them, “Reproduce, increase, and spread throughout the earth!
2 Hofu na utisho wenu vitakuwa juu ya kila mnyama aliye hai juu ya nchi, juu ya kila ndege wa angani, juu ya kila kitu kiendacho chini juu ya ardhi, na juu ya samaki wote wa baharini. Vimetolewa katika mikono yenu.
All animals will be very afraid of you—this includes all the birds, all the creatures that run along the ground, and all the fish in the sea. You are in charge of them.
3 Kila kitu kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula kwa ajili yenu. Kama nilivyo wapa mimea, sasa nawapa kila kitu.
Every living creature that moves will be food for you, as well as all the green plants.
4 Lakini msile nyama pamoja na uhai wake - yaani damu yake - ndani yake.
But do not eat meat with the lifeblood still in it.
5 Lakini kwa ajili ya damu yenu, uhai uliomo katika damu yenu nitataka malipo. Kutoka katika mkono wa kila mnyama nitaitaka. Kutoka katika mkono wa kila mtu, yaani, kutoka katika mkono wa yule ambaye amemuua ndugu yake, nitataka fidia kwa ajili ya uhai wa mtu huyo.
If your blood is shed by any animal, I will call it to account; and if your blood is shed by any person, I will call that person to account.
6 Yeyote amwagaye damu ya mtu, kwa njia ya mtu damu yake itamwagwa, kwa sababu ilikuwa ni katika mfano wa Mungu kwamba Mungu alimuumba mtu.
Whoever sheds the blood of a human being will have their blood shed by human beings. For God made human beings in his image.
7 Na hivyo nanyi zaeni na kuongezeka, sambaeni katika inchi yote na muongezeke juu yake.”
Reproduce, increase, and spread throughout the earth—have many descendants!”
8 Kisha Mungu akazungumza na Nuhu na wanae pamoja naye, akisema,
Then God told Noah and his sons who were there with him,
9 “Kwa ajili yangu, sikiliza! Ninakwenda kulithibitisha agano langu pamoja nawe na uzao wenu baada yenu,
“Listen, I'm making my agreement with you and your descendants,
10 na kwa kila kiumbe hai kilicho pamoja nawe, pamoja na ndege, mnyama wa kufugwa, na kila kiumbe cha nchi pamoja nawe, kuanzia kwa wote waliotoka kwenye safina, mpaka kwa kila kiumbe hai juu ya nchi.
and with all the animals around you—the birds, the livestock, and all the wild animals of the earth—every animal that accompanied you on the ark.
11 Kwa sababu hii ninalithibitisha agano langu pamoja nanyi, kwamba hapatatokea kuangamizwa kwa mwenye mwili kwa njia ya maji ya gharika. Tena hapatatokea gharika ya kuangamiza nchi.”
In my agreement I'm promising you that I won't ever again destroy all life by means of a flood—there won't be a destructive flood like this again.”
12 Mungu akasema, “na hii ndiyo ishara ya agano ambalo ninafanya kati yangu na ninyi pamoja na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, kwa vizazi vyote vya baadaye:
Then God said, “I'm going to give you a sign to confirm the agreement I'm making between me and you and all living creatures, an agreement that will last for all generations.
13 Nimeweka upinde wangu wa mvua katika wingu, na itakuwa ndiyo ishara ya agano kati yangu na nchi.
I've placed my rainbow in the clouds, and this will be the sign of my agreement with you and with all life on earth.
14 Hata itakuwa nitakapoleta wingu juu ya nchi na upinde wa mvua ukaonekana katika wingu,
Whenever I make clouds form over the earth and the rainbow appears,
15 ndipo nitakumbuka agano langu, ambalo ni kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai cha wote mwenye mwili. Maji hayatafanyika tena gharika kuharibu wote wenye mwili.
it will remind me of my agreement between me and you and every kind of living creature that floodwaters won't ever again destroy all life.
16 Upinde wa mvua utakuwa katika mawingu na nitauona, ili kukumbuka agano la milele kati ya Mungu na kila kiumbe hai cha wote wenye mwili ambacho kiko juu ya nchi.”
I will see the rainbow in the clouds and it will remind me of the eternal agreement between God and every kind of living creature that lives on the earth.”
17 Kisha Mungu akamwambia Nuhu, “Hii ni ishara ya agano ambalo nimelithibitisha kati yangu na wenye mwili wote ambao wako juu ya nchi.”
Then God told Noah, “This is the sign of the agreement I'm making between me and every creature on earth.”
18 Wana wa Nuhu ambao walitoka katika safina walikuwa ni Shemu, Hamu, na Yafethi. Na Hamu akamzaa kanaani.
Noah's sons who left the ark were Shem, Ham, and Japheth. (Ham was the father of the Canaanites.)
19 Watatu hawa walikuwa ndio wana wa Nuhu, na kutokea kwa hawa nchi yote ikajaa watu.
All the people who are spread over the world are descended from these three sons of Noah.
20 Nuhu akaanza kuwa mkulima, na akapanda mizabibu.
Noah started to cultivate the ground as a farmer, and he planted a vineyard.
21 Akanywa sehemu ya divai na akalewa. Akawa amelala hemeani uchi.
He drank some of the wine he'd produced, got drunk, and fell asleep in his tent, naked.
22 Kisha Hamu, baba yake na Kanaani, akaona uchi wa baba yake na akawaambia ndugu zake wawili waliokuwa nje.
Ham, the father of Canaan, saw his father's private parts and went and told his two brothers who were outside.
23 Kwa hiyo Shemu na Yafethi wakachukua kanzu wakaitanda juu ya mabega yao, na wakatembea kinyumenyume na wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zikiwa zimegeuka nyuma upande mwingine, kwa hiyo hawakuona uchi wa baba yao.
Shem and Japheth picked up a cloak and, holding it over their shoulders, walked in backwards and covered up their father's privates. They made sure to look the other way so they wouldn't see their father's privates.
24 Nuhu alipozinduka kutoka katika ulevi wake, alijua ni jambo gani mtoto wake mdogo amemfanyia.
When Noah woke up from his drunken sleep, he discovered what his youngest son had done,
25 Hivyo akasema, “Alaaniwe Kanaani. Na awe mtumishi kwa watumishi wa ndugu zake.”
and said, “May Canaan be cursed! He will be the lowest kind of slave and will serve his brothers!”
26 Akasema pia, Yahwe, Mungu wa Shemu, abarikiwe, Kanaani na awe mtumwa wake.
Then Noah continued, “May the Lord be blessed, the God of Shem, and may Canaan be his slave.
27 Mungu na apanuwe mipaka ya Yafethi, na afanye makazi yake katika hema za Shemu. Kanaani na awe mtumwa wake.”
May God give Japtheth plenty of space to accommodate his many descendants, and may they live at peace among Shem's people, and may Canaan also be his slave.”
28 Baada ya gharika, Nuhu aliishi miaka miatatu na hamsini.
Noah lived for another 350 years after the flood.
29 Siku zote za Nuhu zilikuwa ni miaka mia tisa na hamsini, na kisha alikufa.
Noah lived a total of 950 years, and then he died.