< Mwanzo 9 >
1 Kisha Mungu akambariki Nuhu na wanawe, na kuwaambia, “Zaeni, mkaongezeke, na muijaze nchi.
And God blessed Noah and his sons. And he said to them: “Increase, and multiply, and fill the earth.
2 Hofu na utisho wenu vitakuwa juu ya kila mnyama aliye hai juu ya nchi, juu ya kila ndege wa angani, juu ya kila kitu kiendacho chini juu ya ardhi, na juu ya samaki wote wa baharini. Vimetolewa katika mikono yenu.
And let the fear and trembling of you be upon all the animals of the earth, and upon all the birds of the air, along with all that moves across the earth. All the fish of the sea have been delivered into your hand.
3 Kila kitu kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula kwa ajili yenu. Kama nilivyo wapa mimea, sasa nawapa kila kitu.
And everything that moves and lives will be food for you. Just as with the edible plants, I have delivered them all to you,
4 Lakini msile nyama pamoja na uhai wake - yaani damu yake - ndani yake.
except that flesh with blood you shall not eat.
5 Lakini kwa ajili ya damu yenu, uhai uliomo katika damu yenu nitataka malipo. Kutoka katika mkono wa kila mnyama nitaitaka. Kutoka katika mkono wa kila mtu, yaani, kutoka katika mkono wa yule ambaye amemuua ndugu yake, nitataka fidia kwa ajili ya uhai wa mtu huyo.
For I will examine the blood of your lives at the hand of every beast. So also, at the hand of mankind, at the hand of each man and his brother, I will examine the life of mankind.
6 Yeyote amwagaye damu ya mtu, kwa njia ya mtu damu yake itamwagwa, kwa sababu ilikuwa ni katika mfano wa Mungu kwamba Mungu alimuumba mtu.
Whoever will shed human blood, his blood will be poured out. For man was indeed made to the image of God.
7 Na hivyo nanyi zaeni na kuongezeka, sambaeni katika inchi yote na muongezeke juu yake.”
But as for you: increase and multiply, and go forth upon the earth and fulfill it.”
8 Kisha Mungu akazungumza na Nuhu na wanae pamoja naye, akisema,
To Noah and to his sons with him, God also said this:
9 “Kwa ajili yangu, sikiliza! Ninakwenda kulithibitisha agano langu pamoja nawe na uzao wenu baada yenu,
“Behold, I will establish my covenant with you, and with your offspring after you,
10 na kwa kila kiumbe hai kilicho pamoja nawe, pamoja na ndege, mnyama wa kufugwa, na kila kiumbe cha nchi pamoja nawe, kuanzia kwa wote waliotoka kwenye safina, mpaka kwa kila kiumbe hai juu ya nchi.
and with every living soul that is with you: as much with the birds as with the cattle and all the animals of the earth that have gone forth from the ark, and with all the wild beasts of the earth.
11 Kwa sababu hii ninalithibitisha agano langu pamoja nanyi, kwamba hapatatokea kuangamizwa kwa mwenye mwili kwa njia ya maji ya gharika. Tena hapatatokea gharika ya kuangamiza nchi.”
I will establish my covenant with you, and no longer will all that is flesh be put to death by the waters of a great flood, and, henceforth, there will not be a great flood to utterly destroy the earth.”
12 Mungu akasema, “na hii ndiyo ishara ya agano ambalo ninafanya kati yangu na ninyi pamoja na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, kwa vizazi vyote vya baadaye:
And God said: “This is the sign of the pact that I grant between me and you, and to every living soul that is with you, for perpetual generations.
13 Nimeweka upinde wangu wa mvua katika wingu, na itakuwa ndiyo ishara ya agano kati yangu na nchi.
I will place my arc in the clouds, and it will be the sign of the pact between myself and the earth.
14 Hata itakuwa nitakapoleta wingu juu ya nchi na upinde wa mvua ukaonekana katika wingu,
And when I obscure the sky with clouds, my arc will appear in the clouds.
15 ndipo nitakumbuka agano langu, ambalo ni kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai cha wote mwenye mwili. Maji hayatafanyika tena gharika kuharibu wote wenye mwili.
And I will remember my covenant with you, and with every living soul that enlivens flesh. And there will no longer be waters from a great flood to wipe away all that is flesh.
16 Upinde wa mvua utakuwa katika mawingu na nitauona, ili kukumbuka agano la milele kati ya Mungu na kila kiumbe hai cha wote wenye mwili ambacho kiko juu ya nchi.”
And the arc will be in the clouds, and I will see it, and I will remember the everlasting covenant that was enacted between God and every living soul of all that is flesh upon the earth.”
17 Kisha Mungu akamwambia Nuhu, “Hii ni ishara ya agano ambalo nimelithibitisha kati yangu na wenye mwili wote ambao wako juu ya nchi.”
And God said to Noah, “This will be the sign of the covenant that I have established between myself and all that is flesh upon the earth.”
18 Wana wa Nuhu ambao walitoka katika safina walikuwa ni Shemu, Hamu, na Yafethi. Na Hamu akamzaa kanaani.
And so the sons of Noah, who came out of the ark, were Shem, Ham, and Japheth. Now Ham himself is the father of Canaan.
19 Watatu hawa walikuwa ndio wana wa Nuhu, na kutokea kwa hawa nchi yote ikajaa watu.
These three are the sons of Noah. And from these all the family of mankind was spread over the whole earth.
20 Nuhu akaanza kuwa mkulima, na akapanda mizabibu.
And Noah, a good farmer, began to cultivate the land, and he planted a vineyard.
21 Akanywa sehemu ya divai na akalewa. Akawa amelala hemeani uchi.
And by drinking its wine, he became inebriated and was naked in his tent.
22 Kisha Hamu, baba yake na Kanaani, akaona uchi wa baba yake na akawaambia ndugu zake wawili waliokuwa nje.
Because of this, when Ham, the father of Canaan, had indeed seen the privates of his father to be naked, he reported it to his two brothers outside.
23 Kwa hiyo Shemu na Yafethi wakachukua kanzu wakaitanda juu ya mabega yao, na wakatembea kinyumenyume na wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zikiwa zimegeuka nyuma upande mwingine, kwa hiyo hawakuona uchi wa baba yao.
And truly, Shem and Japheth put a cloak upon their arms, and, advancing backwards, covered the privates of their father. And their faces were turned away, so that they did not see their father’s manhood.
24 Nuhu alipozinduka kutoka katika ulevi wake, alijua ni jambo gani mtoto wake mdogo amemfanyia.
Then Noah, awaking from the wine, when he had learned what his younger son had done to him,
25 Hivyo akasema, “Alaaniwe Kanaani. Na awe mtumishi kwa watumishi wa ndugu zake.”
he said, “Cursed be Canaan, a servant of servants will he be to his brothers.”
26 Akasema pia, Yahwe, Mungu wa Shemu, abarikiwe, Kanaani na awe mtumwa wake.
And he said: “Blessed be the Lord God of Shem, let Canaan be his servant.
27 Mungu na apanuwe mipaka ya Yafethi, na afanye makazi yake katika hema za Shemu. Kanaani na awe mtumwa wake.”
May God enlarge Japheth, and may he live in the tents of Shem, and let Canaan be his servant.”
28 Baada ya gharika, Nuhu aliishi miaka miatatu na hamsini.
And after the great flood, Noah lived for three hundred and fifty years.
29 Siku zote za Nuhu zilikuwa ni miaka mia tisa na hamsini, na kisha alikufa.
And all his days were completed in nine hundred and fifty years, and then he died.