< Mwanzo 7 >
1 Yahwe akamwambia Nuhu, “Njoo, wewe na nyumba yako wote, katika safina, kwa kuwa nimeona kuwa wewe ni mwenye haki mbele yangu katika kizazi hiki.
И рече Господь Бог к Ною: вниди ты и весь дом твой в ковчег, яко тя видех праведна предо Мною в роде сем:
2 Kwa kila mnyama aliye safi utakuja nao saba wa kiume na saba wa kike. Na kwa wanyama wasio safi, lete wawili wawili, wakiume na wakike.
от скотов же чистых введи к себе седмь седмь, мужеский пол и женский: от скотов же нечистых два два, мужеский пол и женский:
3 Pia na kwa ndege wa angani, lete saba wa kiume na saba wa kike, ili kuhifadhi kizazi chao juu ya uso wa nchi yote.
и от птиц небесных чистых седмь седмь, мужеский пол и женский: и от всех птиц нечистых две две, мужеский пол и женский, препитати семя по всей земли:
4 Kwa kuwa ndani ya siku saba nitasababisha mvua kunyesha juu ya nchi muda wa siku arobaini mchana na usiku. Nitaharibu kila kiumbe hai nilichokiumba juu ya uso wa ardhi.”
еще бо дний седмь, Аз наведу дождь на землю четыредесять дний и четыредесять нощей: и потреблю всякое востание, еже сотворих, от лица всея земли.
5 Nuhu alifanya yote ambayo Yahwe alimuagiza.
И сотвори Ное вся, елика заповеда ему Господь Бог.
6 Nuhu alikuwa na umri wa miaka mia sita wakati gharika ilipokuja juu ya nchi.
Ное же бе лет шести сот, и потоп водный бысть на земли.
7 Nuhu, watoto wake wa kiume, mke wake, na wake za watoto wake waliingia katika safina pamoja kwa sababu ya maji ya gharika.
Вниде же Ное и сынове его, и жена его и жены сынов его с ним в ковчег, воды ради потопа.
8 Wanyama ambao ni safi na wanyama ambao si safi, ndege, na kila kitambaacho juu ya ardhi,
И от птиц чистых и от птиц нечистых, и от скот чистых и от скот нечистых, (и от зверей, ) и от всех гадов пресмыкающихся по земли,
9 wawili wawili mume na mke wakaja kwa Nuhu na wakaingia katika safina, kama vile Mungu alivyokuwa amemwagiza Nuhu.
два два внидоша к Ною в ковчег, мужеский пол и женский, якоже заповеда (Господь) Бог Ною.
10 Ikawa kwamba baada ya siku saba, maji ya gharika yakaja juu ya nchi.
И бысть по седми днех, и вода потопная бысть на земли.
11 Katika mwaka wa mia sita wa maisha yake Nuhu, katika mwezi wa pili, katika siku ya kumi na saba ya mwezi, katika siku iyo hiyo, chemchemi zote za vilindi vikuu zilipasuka na kufunguka, na madirisha ya mbinguni yakafunguka.
В шестьсотное лето в житии Ноеве, втораго месяца, в двадесять седмый день месяца, в день той разверзошася вси источницы бездны, и хляби небесныя отверзошася:
12 Mvua ikaanza kunyesha juu ya nchi kwa siku arobaini mchana na usiku.
и бысть дождь на землю четыредесять дний и четыредесять нощей.
13 Katika siku iyo hiyo Nuhu pamoja na watoto wake, Shem, Ham, na Yafethi na mke wa Nuhu, na wale wake watatu wa wana wa Nuhu pamoja waliingia katika safina.
В день той вниде Ное, Сим, Хам, Иафеф, сынове Ноевы, и жена Ноева, и три жены сынов его с ним в ковчег.
14 Waliingia pamoja na kila mnyama wa mwitu kwa jinsi yake, na kila mnyama wa kufugwa kwa jinsi yake, na kila kitambaacho juu ya ardhi kwa jinsi yake, na kila aina ya ndege kwa jinsi yake, kila aina ya kiumbe chenye mabawa.
И вси зверие земнии по роду, и вси скоти по роду, и всякий гад движущийся на земли по роду, и всякая птица пернатая по роду своему,
15 Viwili viwili katika kila chenye mwili ambacho kilikuwa na pumzi ya uhai kilikuja kwa Nuhu na kuingia katika safina.
внидоша к Ною в ковчег два два, мужеский пол и женский, от всякия плоти, в нейже есть дух животный:
16 Wanyama walioingia ndani walikuwa wakiume na kike katika wote wenye mwili; wakaingia kama vile Mungu alivyokuwa amemwagiza. Kisha Yahwe akawafungia mlango.
и входящая мужеский пол и женский от всякия плоти, внидоша к Ною в ковчег, якоже заповеда Господь Бог Ною: и затвори Господь Бог ковчег отвне его.
17 Kisha gharika ikaja juu ya nchi kwa siku arobaini, na maji yakaongezeka na kuinua safina juu ya nchi.
И бысть потоп четыредесять дний и четыредесять нощей на земли, и умножися вода и взя ковчег, и возвысися от земли:
18 Maji yakafunika kabisa nchi, na safina ikaelea juu ya uso wa maji.
и возмогаше вода, и умножашеся зело на земли, и ношашеся ковчег верху воды.
19 Maji yakaongezeka zaidi juu ya nchi kiasi kwamba milima yote mirefu ambayo ilikuwa chini ya anga ikafunikwa.
Вода же возмогаше зело зело на земли: и покры вся горы высокия, яже бяху под небесем:
20 Maji yakaongezeka dhiraa kumi na tano juu ya vilele vya milima.
пятьнадесять лактей горе возвысися вода, и покры вся горы высокия.
21 Vitu vyote vyenye uhai ambavyo vilitembea juu ya nchi vilikufa: ndege, mifugo, wanyama wa mwituni, viumbe hai vyote kwa wingi vilivyoishi juu ya nchi, pamoja na watu.
И умре всякая плоть движущаяся по земли птиц и скотов и зверей, и всякий гад движущийся на земли, и всякий человек,
22 Viumbe hai vyote ambavyo vilikaa juu ya ardhi, vilivyo pumua pumzi ya uhai kwa njia ya pua, vilikufa.
и вся елика имут дыхание жизни, и все еже бе на суши умре.
23 Hivyo kila kilichokuwa hai ambacho kilikuwa juu ya uso wa mchi kilifutwa, kuanzia watu mpaka wanyama wakubwa, mpaka vitambaavyo, na mpaka ndege wa angani. Vyote viliangamizwa kutoka kwenye nchi. Nuhu tu pamoja na wale waliokuwa naye kwenye safina ndio walisalia.
И потребися всякое востание, еже бяше на лицы всея земли, от человека даже до скота и гадов и птиц небесных, и потребишася от земли: и оста Ное един, и иже с ним в ковчезе.
24 Maji haya kuzama chini ya nchi kwa muda wa siku miamoja na hamsini.
И возвысися вода над землею дний сто пятьдесят.