< Mwanzo 7 >
1 Yahwe akamwambia Nuhu, “Njoo, wewe na nyumba yako wote, katika safina, kwa kuwa nimeona kuwa wewe ni mwenye haki mbele yangu katika kizazi hiki.
Or le Seigneur dit à Noé: Entre, toi et toute ta maison, dans l’arche; car je t’ai trouvé juste devant moi au milieu de cette génération.
2 Kwa kila mnyama aliye safi utakuja nao saba wa kiume na saba wa kike. Na kwa wanyama wasio safi, lete wawili wawili, wakiume na wakike.
De tous les animaux purs prends sept couples, mâles et femelles; mais des animaux impurs, deux couples, mâles et femelles.
3 Pia na kwa ndege wa angani, lete saba wa kiume na saba wa kike, ili kuhifadhi kizazi chao juu ya uso wa nchi yote.
Et des volatiles du ciel pareillement sept couples, mâles et femelles, afin qu’en soit conservée la race sur la face de toute la terre.
4 Kwa kuwa ndani ya siku saba nitasababisha mvua kunyesha juu ya nchi muda wa siku arobaini mchana na usiku. Nitaharibu kila kiumbe hai nilichokiumba juu ya uso wa ardhi.”
Car encore sept jours, et après je ferai pleuvoir sur la terre durant quarante jours et quarante nuits, et j’exterminerai toutes les créatures que j’ai faites, de la surface de la terre.
5 Nuhu alifanya yote ambayo Yahwe alimuagiza.
Noé fit donc tout ce que lui avait ordonné le Seigneur.
6 Nuhu alikuwa na umri wa miaka mia sita wakati gharika ilipokuja juu ya nchi.
Or, il avait six cents ans, lorsque les eaux du déluge inondèrent la terre.
7 Nuhu, watoto wake wa kiume, mke wake, na wake za watoto wake waliingia katika safina pamoja kwa sababu ya maji ya gharika.
Ainsi Noé et ses fils, sa femme et les femmes de ses fils entrèrent avec lui dans l’arche, à cause des eaux du déluge.
8 Wanyama ambao ni safi na wanyama ambao si safi, ndege, na kila kitambaacho juu ya ardhi,
Les animaux aussi, purs et impurs, les oiseaux et tout ce qui se meut sur la terre,
9 wawili wawili mume na mke wakaja kwa Nuhu na wakaingia katika safina, kama vile Mungu alivyokuwa amemwagiza Nuhu.
Entrèrent deux à deux auprès de Noé dans l’arche, mâle et femelle, comme avait ordonné le Seigneur à Noé.
10 Ikawa kwamba baada ya siku saba, maji ya gharika yakaja juu ya nchi.
Et lorsque les sept jours furent passés, les eaux du déluge inondèrent la terre.
11 Katika mwaka wa mia sita wa maisha yake Nuhu, katika mwezi wa pili, katika siku ya kumi na saba ya mwezi, katika siku iyo hiyo, chemchemi zote za vilindi vikuu zilipasuka na kufunguka, na madirisha ya mbinguni yakafunguka.
L’an six cent de la vie de Noé, au second mois, le dix-septième jour du mois, toutes les sources du grand abîme furent rompues, et les cataractes du ciel furent ouvertes;
12 Mvua ikaanza kunyesha juu ya nchi kwa siku arobaini mchana na usiku.
Et la pluie tomba sur la terre durant quarante jours et quarante nuits.
13 Katika siku iyo hiyo Nuhu pamoja na watoto wake, Shem, Ham, na Yafethi na mke wa Nuhu, na wale wake watatu wa wana wa Nuhu pamoja waliingia katika safina.
Ce jour-là même, Noé, Sem, Cham et Japhet, ses fils, sa femme et les trois femmes de ses fils entrèrent dans l’arche;
14 Waliingia pamoja na kila mnyama wa mwitu kwa jinsi yake, na kila mnyama wa kufugwa kwa jinsi yake, na kila kitambaacho juu ya ardhi kwa jinsi yake, na kila aina ya ndege kwa jinsi yake, kila aina ya kiumbe chenye mabawa.
Ainsi, eux et tout animal selon son espèce, tous les animaux domestiques selon leur espèce, et tout ce qui se meut sur la terre dans son genre et tout volatile selon son genre, tous les oiseaux et tout ce qui s’élève dans l’air,
15 Viwili viwili katika kila chenye mwili ambacho kilikuwa na pumzi ya uhai kilikuja kwa Nuhu na kuingia katika safina.
Entrèrent auprès de Noé dans l’arche, deux à deux, de toute chair en laquelle est l’esprit de vie.
16 Wanyama walioingia ndani walikuwa wakiume na kike katika wote wenye mwili; wakaingia kama vile Mungu alivyokuwa amemwagiza. Kisha Yahwe akawafungia mlango.
Et ceux qui y entrèrent, entrèrent mâles et femelles de toute chair, comme Dieu lui avait ordonné: et le Seigneur l’enferma par dehors.
17 Kisha gharika ikaja juu ya nchi kwa siku arobaini, na maji yakaongezeka na kuinua safina juu ya nchi.
Et il y eut un déluge durant quarante jours sur la terre: et les eaux s’accrurent et élevèrent l’arche de la terre dans les airs.
18 Maji yakafunika kabisa nchi, na safina ikaelea juu ya uso wa maji.
Car elles se répandirent impétueusement, et remplirent tout sur la surface de la terre: mais l’arche était portée sur les eaux.
19 Maji yakaongezeka zaidi juu ya nchi kiasi kwamba milima yote mirefu ambayo ilikuwa chini ya anga ikafunikwa.
Et les eaux crûrent prodigieusement sur la terre, et toutes les hautes montagnes furent couvertes sous le ciel entier.
20 Maji yakaongezeka dhiraa kumi na tano juu ya vilele vya milima.
L’eau s’éleva de quinze coudées au-dessus des montagnes qu’elle avait couvertes.
21 Vitu vyote vyenye uhai ambavyo vilitembea juu ya nchi vilikufa: ndege, mifugo, wanyama wa mwituni, viumbe hai vyote kwa wingi vilivyoishi juu ya nchi, pamoja na watu.
Ainsi périt entièrement toute chair qui se mouvait sur la terre, d’oiseaux, d’animaux domestiques, de bêtes sauvages, et de tout reptile qui rampe sur la terre: tous les hommes,
22 Viumbe hai vyote ambavyo vilikaa juu ya ardhi, vilivyo pumua pumzi ya uhai kwa njia ya pua, vilikufa.
Et tout ce qui a un souffle de vie sur la terre, moururent.
23 Hivyo kila kilichokuwa hai ambacho kilikuwa juu ya uso wa mchi kilifutwa, kuanzia watu mpaka wanyama wakubwa, mpaka vitambaavyo, na mpaka ndege wa angani. Vyote viliangamizwa kutoka kwenye nchi. Nuhu tu pamoja na wale waliokuwa naye kwenye safina ndio walisalia.
C’est ainsi que Dieu détruisit toute créature qui était sur la terre, depuis l’homme jusqu’à la bête, tant le reptile que les oiseaux du ciel: tout disparut de la terre; il ne resta que Noé et ceux qui étaient avec lui dans l’arche.
24 Maji haya kuzama chini ya nchi kwa muda wa siku miamoja na hamsini.
Et les eaux couvrirent la terre durant cent cinquante jours.