< Mwanzo 7 >

1 Yahwe akamwambia Nuhu, “Njoo, wewe na nyumba yako wote, katika safina, kwa kuwa nimeona kuwa wewe ni mwenye haki mbele yangu katika kizazi hiki.
Yahvé dit à Noé: « Entre dans le navire avec toute ta famille, car j'ai vu ta justice devant moi, dans cette génération.
2 Kwa kila mnyama aliye safi utakuja nao saba wa kiume na saba wa kike. Na kwa wanyama wasio safi, lete wawili wawili, wakiume na wakike.
Tu prendras avec toi sept couples de chaque animal pur, le mâle et sa femelle. Des animaux qui ne sont pas purs, tu en prendras deux, le mâle et sa femelle.
3 Pia na kwa ndege wa angani, lete saba wa kiume na saba wa kike, ili kuhifadhi kizazi chao juu ya uso wa nchi yote.
Et aussi des oiseaux du ciel, sept et sept, mâle et femelle, pour faire vivre la semence sur la surface de toute la terre.
4 Kwa kuwa ndani ya siku saba nitasababisha mvua kunyesha juu ya nchi muda wa siku arobaini mchana na usiku. Nitaharibu kila kiumbe hai nilichokiumba juu ya uso wa ardhi.”
En sept jours, je ferai pleuvoir sur la terre pendant quarante jours et quarante nuits. Je détruirai tout être vivant que j'ai créé à la surface de la terre. »
5 Nuhu alifanya yote ambayo Yahwe alimuagiza.
Noé fit tout ce que Yahvé lui avait ordonné.
6 Nuhu alikuwa na umri wa miaka mia sita wakati gharika ilipokuja juu ya nchi.
Noé avait six cents ans lorsque le déluge d'eaux vint sur la terre.
7 Nuhu, watoto wake wa kiume, mke wake, na wake za watoto wake waliingia katika safina pamoja kwa sababu ya maji ya gharika.
Noé monta dans le bateau avec ses fils, sa femme et les femmes de ses fils, à cause du déluge.
8 Wanyama ambao ni safi na wanyama ambao si safi, ndege, na kila kitambaacho juu ya ardhi,
Les animaux purs, les animaux impurs, les oiseaux et tout ce qui rampe sur le sol
9 wawili wawili mume na mke wakaja kwa Nuhu na wakaingia katika safina, kama vile Mungu alivyokuwa amemwagiza Nuhu.
allèrent par paires vers Noé dans le bateau, mâle et femelle, comme Dieu l'avait ordonné à Noé.
10 Ikawa kwamba baada ya siku saba, maji ya gharika yakaja juu ya nchi.
Après les sept jours, les eaux du déluge arrivèrent sur la terre.
11 Katika mwaka wa mia sita wa maisha yake Nuhu, katika mwezi wa pili, katika siku ya kumi na saba ya mwezi, katika siku iyo hiyo, chemchemi zote za vilindi vikuu zilipasuka na kufunguka, na madirisha ya mbinguni yakafunguka.
La six centième année de la vie de Noé, au deuxième mois, le dix-septième jour du mois, en ce jour, toutes les sources du grand abîme éclatèrent, et les fenêtres du ciel s'ouvrirent.
12 Mvua ikaanza kunyesha juu ya nchi kwa siku arobaini mchana na usiku.
Il pleuvait sur la terre quarante jours et quarante nuits.
13 Katika siku iyo hiyo Nuhu pamoja na watoto wake, Shem, Ham, na Yafethi na mke wa Nuhu, na wale wake watatu wa wana wa Nuhu pamoja waliingia katika safina.
Ce même jour, Noé, Sem, Cham et Japhet, les fils de Noé, ainsi que la femme de Noé et les trois femmes de ses fils avec eux, montèrent dans le navire,
14 Waliingia pamoja na kila mnyama wa mwitu kwa jinsi yake, na kila mnyama wa kufugwa kwa jinsi yake, na kila kitambaacho juu ya ardhi kwa jinsi yake, na kila aina ya ndege kwa jinsi yake, kila aina ya kiumbe chenye mabawa.
eux et tous les animaux selon leur espèce, tout le bétail selon son espèce, tous les reptiles qui rampent sur la terre selon leur espèce, et tous les oiseaux selon leur espèce, tous les oiseaux de toute espèce.
15 Viwili viwili katika kila chenye mwili ambacho kilikuwa na pumzi ya uhai kilikuja kwa Nuhu na kuingia katika safina.
Des couples de toute chair ayant en eux une haleine de vie montèrent dans le bateau vers Noé.
16 Wanyama walioingia ndani walikuwa wakiume na kike katika wote wenye mwili; wakaingia kama vile Mungu alivyokuwa amemwagiza. Kisha Yahwe akawafungia mlango.
Ceux qui entrèrent, entrèrent mâle et femelle de toute chair, comme Dieu l'avait ordonné; puis Yahvé l'enferma.
17 Kisha gharika ikaja juu ya nchi kwa siku arobaini, na maji yakaongezeka na kuinua safina juu ya nchi.
Le déluge fut quarante jours sur la terre. Les eaux grossirent et soulevèrent le navire, qui s'éleva au-dessus de la terre.
18 Maji yakafunika kabisa nchi, na safina ikaelea juu ya uso wa maji.
Les eaux montèrent et s'élevèrent très haut sur la terre, et le navire flotta à la surface des eaux.
19 Maji yakaongezeka zaidi juu ya nchi kiasi kwamba milima yote mirefu ambayo ilikuwa chini ya anga ikafunikwa.
Les eaux s'élevèrent très haut sur la terre. Toutes les hautes montagnes qui étaient sous tout le ciel furent couvertes.
20 Maji yakaongezeka dhiraa kumi na tano juu ya vilele vya milima.
Les eaux s'élevèrent de quinze coudées, et les montagnes furent couvertes.
21 Vitu vyote vyenye uhai ambavyo vilitembea juu ya nchi vilikufa: ndege, mifugo, wanyama wa mwituni, viumbe hai vyote kwa wingi vilivyoishi juu ya nchi, pamoja na watu.
Toute chair qui se mouvait sur la terre mourut, les oiseaux, le bétail, les animaux, tous les reptiles qui rampent sur la terre, et tous les hommes.
22 Viumbe hai vyote ambavyo vilikaa juu ya ardhi, vilivyo pumua pumzi ya uhai kwa njia ya pua, vilikufa.
Tout ce qui était sur la terre ferme, dans les narines duquel se trouvait le souffle de l'esprit de vie, mourut.
23 Hivyo kila kilichokuwa hai ambacho kilikuwa juu ya uso wa mchi kilifutwa, kuanzia watu mpaka wanyama wakubwa, mpaka vitambaavyo, na mpaka ndege wa angani. Vyote viliangamizwa kutoka kwenye nchi. Nuhu tu pamoja na wale waliokuwa naye kwenye safina ndio walisalia.
Tout être vivant qui était à la surface de la terre fut détruit, y compris l'homme, le bétail, les reptiles et les oiseaux du ciel. Ils furent détruits de la terre. Il ne resta que Noé et ceux qui étaient avec lui dans le bateau.
24 Maji haya kuzama chini ya nchi kwa muda wa siku miamoja na hamsini.
Les eaux inondèrent la terre pendant cent cinquante jours.

< Mwanzo 7 >

The Great Flood
The Great Flood