< Mwanzo 6 >

1 Ikawa wakati watu walipoanza kuongezeka juu ya uso wa nchi na wana wa kike wakazaliwa kwao,
When people began to become very numerous all over the earth, and many daughters were born to them,
2 wana wa Mungu walipoona kuwa mabinti wa wanadamu ni wenye kuvutia. waliwachukua kuwa wake zao, kila waliye mchagua.
some of the men who (belonged to/believed in) God saw that some of the women who did not (belong to/believe in) God were very beautiful. So they took whichever ones they chose to become their wives.
3 Yahwe akaema, “roho yangu haitasalia kwa mwanadamu milele, kwa kuwa wao ni nyama. Wataishi miaka 120.”
Then Yahweh said, “[I will] not [allow] my Spirit to keep people alive forever (OR, the breath of life will not remain in people forever). They will die eventually. They will live not more than 120 years before they die (OR, there will be only 120 more years before they die).”
4 Majitu makubwa yalikuwa juu ya uso wa nchi nyakati hizo, na hata baada ya hapo. Hii ilitokea wakati wana wa Mungu walipowaoa binti za wanadamu, na kupata watoto pamoja nao. Hawa walikuwa watu hodari zamani, watu wenye sifa.
There were [giants called] Nephils who lived on the earth at that time and later. During that time [some of the Nephil] men who (belonged to/believed in) God had sex [EUP] with women who did not (belong to/believe in) God, and they gave birth to children. The Nephils were considered to be heroic fighters, and they became famous.
5 Yahwe akaona kwamba uovu wa watu umezidi katika nchi, na kwamba mawazo ya mioyo yao daima inaelekea tu katika uovu.
Yahweh saw that people on the earth had become very wicked, and that everything they thought about evil things continually.
6 Yahwe akajuta kuwa amemuumba mwanadamu juu ya nchi, na ikamuhuzunisha moyo wake.
Yahweh was sorry that he had made people.
7 Kwa hiyo Yahwe akasema, “Nitamfutilia mbali mwanadamu ambaye nimemuumba katika uso wa nchi; mwanadamu na wanyama wakubwa, na vitambaavyo na ndege wa angani, kwa kuwa nimehuzunika kuwa nimeviumba.”
So he said, “I will completely destroy the people I made. I will also destroy all the animals and the creatures that scurry across the ground and the birds. None of them will remain on the earth, because I regret that I made them.”
8 Lakini Nuhu akapata neema ya upendeleo machoni pa Yahwe.
But Yahweh was pleased with Noah.
9 Kulikuwa na matukio kumuhusu Nuhu. Nuhu alikuwa mtu mwenye haki, na asiye na lawama miongoni mwa watu wa kipindi chake. Nuhu alitembea na Mungu.
This is why: Noah was a man who always acted in a righteous way. No one who lived at that time could criticize him about anything. Noah lived in close fellowship with God.
10 Nuhu akafanyika baba wa wana watatu wa kiume: Shem, Ham na Yafeti.
Noah became the father of three sons: Shem, Ham, and Japheth.
11 Nchi iliharibika mbele za Mungu, na ikajaa ghasia.
At that time God considered that everyone else on earth was very wicked, and everywhere on the earth, people [MTY] were acting cruelly and violently toward each other.
12 Mungu akaiona nchi; tazama, ilikuwa imeharibika, kwa kuwa wote wenye mwili walikuwa wameharibu njia zao juu ya nchi.
God was dismayed when he saw how evil people [MTY] were, because everyone (OR, all living creatures) had begun to behave in an evil way.
13 Mungu akamwambia Nuhu, “Nimeona kuwa sasa niwakati wa mwisho kwa wote wenye mwili, kwa kuwa inchi imejaa ghasia kutokana na wao. Hakika, nitawaharibu wao pamoja na nchi.
So God said to Noah, “I have decided to destroy everyone, because all over the earth people are acting violently toward each other. So I am about to get rid of them as well as everything else on the earth.
14 Tengeneza safina ya mti wa mvinje kwa ajili yako. Tengeneza vyumba katika safina, na vifunike kwa lami ndani na nje.
[I want you to] make for yourself a large boat from cypress wood. Make rooms inside it. Cover the outside and the inside with tar [to make it (waterproof/so that water cannot get in and sink the boat]).
15 Hivi ndivyo utakavyofanya: urefu wa safina dhiraa miatatu, upana wake dhiraa hamsini, kwenda juu kwake dhiraa thelathini.
This is the size you must make it: It shall be (150 yards/135 meters) long, (25 yards/22.5 meters) wide, and (15 yards/13.5 meters) high.
16 Tengeneza paa la safina, na ulimalize kwa kipimo cha dhiraa kutoka juu ubavuni. Weka mlango katika ubavu wa safina na utengeneze dari ya chini, ya pili na ya tatu.
Make a roof for the boat. Leave a space of about (18 in./.5 meter) between the sides and the roof to let air and light enter (OR, the middle of the roof should be 18 inches higher than the sides). Build the boat with three decks inside, and put a door in one side.
17 Sikiliza, nimekaribia kuleta gharika ya maji juu ya nchi, kuharibu wenye mwili wote wakaao ndani ya nchi wenye pumzi ya uhai chini ya mbingu. Kila kitu kilichopo juu ya nchi kitakufa.
Listen carefully! I am about to cause a flood to occur that will destroy every creature that lives beneath the sky. Everything on the earth will die.
18 Lakini nitalifanya thabiti agano langu na wewe. Utaingia ndani ya safina, wewe, na wana wako wa kiume, na mke wako, pamoja na wake za wanao.
But I will make an agreement with you(sg): You and your wife, your sons and their wives will enter the boat.
19 Kwa kila kiumbe hai chenye mwili, viwili vya kila aina utavileta ndani ya safina, ili visalie hai pamoja nawe, vya kike na vya kiume.
And I want to save some of all kinds of creatures. So you must also bring two of all living creatures, a male and a female, into the boat with you, so that their species also may remain alive.
20 Katika ndege kwa jinsi yake, na wanyama wakubwa kwa jinsi yake, kila kitambaacho ardhini kwa jinsi yake, viwili viwili vya kila aina vitakuja kwako ili viwe salama.
Two of every kind of creature will come to [in order that by your putting them in the boat] you will keep them alive. They will include two of each kind of bird and each kind of animal and each kind of creature that scurries across the ground.
21 Kusanya kila aina ya chakula kinacholiwa kwa ajili yako na ukitunze, ili kwamba viwe chakula chako na chao.”
You must also take some of every kind of food that you and all these animals will need, and store it in the boat.”
22 Kwa hiyo Nuhu akafanya hivi. kulingana na yote ambayo Mungu alimuagiza, ndivyo alifanya.
So Noah did everything that God told him to do.

< Mwanzo 6 >

The World is Destroyed by Water
The World is Destroyed by Water