< Mwanzo 50 >

1 Yusufu akahuzunika sana hata akauangukia uso wa baba yake, akamlilia, na kumbusu.
Yusuf kendini babasının üzerine attı, ağlayarak onu öptü.
2 Yusufu akawaagiza watumishi wake matabibu kumtia dawa babaye. Hivyo matabibu wakampaka dawa Israeli.
Babasının cesedini mumyalamaları için özel hekimlerine buyruk verdi. Hekimler İsrail'i mumyaladılar.
3 Wakatimiza siku arobain, kwani huo ndio uliokuwa muda kamili wa kutia dawa. Wamisri wakamlilia kwa siku sabini
Bu iş kırk gün sürdü. Mumyalama için bu süre gerekliydi. Mısırlılar İsrail için yetmiş gün yas tuttu.
4 Siku za maombolezo zilipotimia, Yusufu akaongea na watumishi wa baraza la kifalme wa Farao kusema, “Ikiwa nimepata kibali machoni penu, tafadharini ongeeni na Farao, kusema,
Yas günleri geçince, Yusuf firavunun ev halkına, “Eğer benden hoşnut kaldınızsa, lütfen firavunla konuşun” dedi,
5 'Baba yangu aliniapisha, kusema, “Tazama, ninakaribia kufa. Unizike katika kaburi nililolichimba kwa ajili yangu mwenyewe katika nchi ya Kanaani. Ndipo utakaponizika.” Basi sasa niruhusu niende nimzike baba yangu, na kisha nitarudi.”
“Babam bana ant içirdi: ‘Ölmek üzereyim. Beni Kenan ülkesinde kendim için kazdırdığım mezara gömeceksin’ dedi. Şimdi lütfen firavuna bildirin, izin versin gideyim, babamı gömüp geleyim.”
6 Farao akajibu, “Nenda na umzika baba yako, kama alivyokuwapisha.”
Firavun, “Git, babanı göm, andını yerine getir” dedi.
7 Yusufu akaenda kumzika baba yake. Maofisa wa Farao wote wakaenda pamoja naye - washauri wa nyumba yake, maofisa waandamizi wote wa nchi ya Misri,
Böylece Yusuf babasını gömmeye gitti. Firavunun bütün görevlileri, sarayın ve Mısır'ın ileri gelenleri ona eşlik etti.
8 pamoja na nyumba yote ya Yusufu na ndugu zake, na nyumba yote ya baba yake. Lakini watoto wao, kondoo wao na makundi ya mbuzi wao yaliachwa katika nchi ya Gosheni.
Yusuf'un bütün ailesi, kardeşleri, babasının ev halkı da onunla birlikteydi. Yalnız çocukları, davarlarla sığırları Goşen'de bıraktılar.
9 Vibandawazi na wapanda farasi pia walikwenda pamoja naye. Lilikuwa kundi kubwa sana la watu.
Arabalarla atlılar da onları izledi. Büyük bir alay oluşturdular.
10 Hata walipokuja katika sakafu ya kupuria ya Atadi upande mwingine wa Yordani, wakaomboleza kwa majonzi ya huzuni kubwa. Yusufu akafanya maombolezo ya siku saba kwa ajili ya babaye pale.
Şeria Irmağı'nın doğusunda Atat Harmanı'na varınca, yüksek sesle, acı acı ağıt yaktılar. Yusuf babası için yedi gün yas tuttu.
11 Wenyeji wa nchi, Wakanaani, walipoona maombolezo katika sakafu ya Atadi, wakasema, “Hili ni tukio la kuhuzunisha sana kwa Wamisri.” Ndiyo maana eneo hilo likaitwa Abeli Mizraimu, lililoko mbele ya Yordani.
O bölgede yaşayan Kenanlılar, Atat Harmanı'ndaki yası görünce, “Mısırlılar ne kadar hüzünlü yas tutuyor!” dediler. Bu yüzden, Şeria Irmağı'nın doğusundaki bu yere Avel-Misrayim adı verildi.
12 Hivyo wanawe wakamfanyia Yakobo kama alivyokuwa amewaagiza.
Yakup'un oğulları, babalarının vermiş olduğu buyruğu tam tamına yerine getirdiler.
13 Wana wake wakampeleka katika nchi ya Kanaani na wakamzika katika pango katika shamba la Makpela, karibu na Mamre. Ibrahimi alikuwa amelinunua pango pamoja na shamba kwa ajili ya eneo la kuzikia. Alikuwa amelinunua kutoka kwa Efroni Mhiti.
Onu Kenan ülkesine götürüp Mamre yakınlarında Makpela Tarlası'ndaki mağaraya gömdüler. O mağarayı mezar yapmak üzere tarlayla birlikte Hititli Efron'dan İbrahim satın almıştı.
14 Baada ya kuwa amemzika babaye, Yusufu akarudi Misri, yeye, pamoja na ndugu zake, na wote waliokuwa wamemsindikiza ili kumzika babaye.
Yusuf babasını gömdükten sonra, kendisi, kardeşleri ve onunla birlikte babasını gömmeye gelenlerin hepsi Mısır'a döndüler.
15 Nduguze Yusufu walipoona kwamba baba yao amekufa, wakasema, “Itakuwaje ikiwa Yusufu atatukasirikia na akataka kutulipa kikamilifu kwa ajili ya uovu tuliomtenda?”
Babalarının ölümünden sonra Yusuf'un kardeşleri, “Belki Yusuf bize kin besliyordur” dediler, “Ya ona yaptığımız kötülüğe karşılık bizden öç almaya kalkarsa?”
16 Hivyo wakamwagiza Yusufu, kusema, “Baba yako alitoa maelekezo kabla hajafa, kusema,
Böylece Yusuf'a haber gönderdiler: “Babamız ölmeden önce Yusuf'a şöyle deyin diye buyurmuştu: ‘Kardeşlerin sana kötülük yaptılar, lütfen onların suçunu, günahını bağışla.’ Ne olur şimdi günahımızı bağışla. Biz babanın Tanrısı'nın kullarıyız.” Yusuf bu haberi alınca ağladı.
17 'Mwambieni hivi Yusufu, “Tafadhari samehe makosa ya ndugu zako na dhambi yao uovu waliokutenda.” Basi wasamehe watumishi wa Mungu wa baba yako.” Yusufu akalia walipomwambia.
18 Ndugu zake pia wakaenda na kuinamisha nyuso zao mbele zake. Wakasema, “Tazama, sisi ni watumishi wako.”
Bunun üzerine kardeşleri gidip onun önünde yere kapanarak, “Senin köleniz” dediler.
19 Lakini Yusufu akawajibu, “Msiogope, Je mimi ni badala ya Mungu?
Yusuf, “Korkmayın” dedi, “Ben Tanrı mıyım?
20 Lakini kwenu, mlikusudia kunidhuru, lakini Mungu alikusudia mema, kuhifadhi maisha ya watu wengi, kama mwonavyo leo.
Siz bana kötülük düşündünüz, ama Tanrı bugün olduğu gibi birçok halkın yaşamını korumak için o kötülüğü iyiliğe çevirdi.
21 Hivyo basi msiogope. Nitawahudumia ninyi na watoto wenu wadogo.” Kwa njia hii aliwatia moyo na kuongea na mioyo yao kwa upole.
Korkmanıza gerek yok, size de çocuklarınıza da bakacağım.” Yüreklerine dokunacak güzel sözlerle onlara güven verdi.
22 Yusufu akakaa Misri, pamoja na familia ya baba yake. Akaishi miaka mia moja na kumi.
Yusuf'la babasının ev halkı Mısır'a yerleştiler. Yusuf yüz on yıl yaşadı.
23 Yusufu akawaona wana wa Efraimu hata kizazi cha tatu. Pia aliwaona wana wa Makiri mwana wa Manase, waliowekwa katika magoti ya Yusufu.
Efrayim'in üç göbek çocuklarını gördü. Manaşşe'nin oğlu Makir'in çocukları onun elinde doğdu.
24 Yusufu akawambia ndugu zake, “Ninakaribia kufa; lakini kwa hakika Mungu atawajilia na kuwaongoza kutoka katika nchi hii na kuwapeleka katika nch aliyoapa kumpa Ibrahimu, kwa Isaka na kwa Yakobo.”
Yusuf yakınlarına, “Ben ölmek üzereyim” dedi, “Ama Tanrı kesinlikle size yardım edecek; sizi İbrahim'e, İshak'a, Yakup'a ant içerek söz verdiği topraklara götürecek.”
25 Kisha Yusufu akawaapisha watu wa Israeli kwa kiapo. Akasema, “Bila shaka Mungu atawajilia. Wakati huo mtachukuwa mifupa yangu kutoka hapa.”
Sonra onlara ant içirerek, “Tanrı kesinlikle size yardım edecek” dedi, “O zaman kemiklerimi buradan götürürsünüz.”
26 Hivyo Yusufu akafa, mwenye miaka 110. Wakampaka dawa na akawekwa katika jeneza huko Misri.
Yusuf yüz on yaşında öldü. Onu mumyalayıp Mısır'da bir tabuta koydular.

< Mwanzo 50 >