< Mwanzo 48 >

1 Ikawa baada ya mambo haya, mmojawapo akamwambia Yusufu, “Tazama, baba yako ni mgonjwa.” Hivyo akaondoka pamoja na wanawe wawili, Manase na Efrahimu.
Pripetilo se je po teh stvareh, da je Jožefu nekdo povedal: »Poglej, tvoj oče je bolan, « in ta je s seboj vzel svoja dva sinova, Manáseja in Efrájima.
2 Yakobo alipoambiwa, “Tazama, mwanao Yusufu amekuja kukuona,” Israeli akakusanya nguvu na kukaa juu ya kitanda.
In nekdo je Jakobu povedal ter rekel: »Glej, tvoj sin Jožef prihaja k tebi.« Izrael se je okrepil in se usedel na postelji.
3 Yakobo akamwambia Yusufu, Mungu Mwenyezi alinitokea huko Luzu katika nchi ya Kanaani. Akanibariki na
Jakob je Jožefu rekel: »Bog Vsemogočni se mi je prikazal pri Luzu, v kánaanski deželi, me blagoslovil
4 kuniambia, 'Tazama, nitakupa uzao mwingi, na kukuzidisha. Nitakufanya kuwa kusanyiko la mataifa. Nitakupa nchi hii wewe na uzao wako kuwa milki ya milele.'
in mi rekel: ›Glej, jaz te bom naredil rodovitnega in te namnožil in jaz bom iz tebe naredil množico ljudstev in to deželo bom dal tvojemu semenu za teboj za večno posest.‹
5 Na sasa wanao wawili, waliozaliwa kwako katika nchi ya Misri kabla sijaja Misri, ni wangu. Efrahimu na Manase watakuwa wangu, kama walivyo Rubeni na Simioni.
In sedaj, tvoja dva sinova, Efrájim in Manáse, ki sta ti bila rojena v egiptovski deželi, preden sem prišel k tebi v Egipt, sta moja; kakor Ruben in Simeon, bosta moja.
6 Watoto utakaowapata baada ya hapo ni wako; watahesabiwa katika majina ya ndugu zao katika urithi wao.
Tvoji potomci pa, ki jih boš zaplodil za njima, bodo tvoji in imenovani bodo po imenu svojih bratov v svoji dediščini.
7 Lakini kwangu mimi, nilipokuja kutoka Padani, kwa uzuni yangu Raheli alikufa njiani katika nchi ya Kanaani, wakati kungalipo kitambo kwenda Efrathi. Nilimzika pale katika njia iendayo Efrathi” (ndio, Bethlehemu).
Kar pa se mene tiče, ko sem prišel iz Padana, je v kánaanski deželi poleg mene umrla Rahela, na poti, ko je bilo le še malo poti, da pride v Efráto. Pokopal sem jo tam, na poti v Efráto; ta isti je Betlehem.«
8 Israeli alipowaona wana wa Yusufu, akasema, “Ni nani hawa?”
Izrael je zagledal Jožefova sinova in rekel: »Kdo sta ta [dva]?«
9 Yusufu akamwambia baba yake, “Hawa ni wanangu, Mungu alionipa hapa:” Israeli akasema, “Walete kwangu, kwamba niwabariki.”
Jožef je svojemu očetu rekel: »Onadva sta moja sinova, katera mi ju je Bog dal na tem kraju.« Rekel je: »Privedi ju, prosim te, k meni in jaz ju bom blagoslovil.«
10 Basi macho ya Israeli yalikuwa yanashindwa kwa ajili ya umri wake, hivyo hakuweza kuona. Hivyo Yusufu akawasogeza karibu yake, na akawabusu na kuwakumbatia.
Torej, Izraelove oči so bile od starosti zatemnjene, tako da ni mogel videti. In privedel ju je bliže k njemu in on ju je poljubil ter ju objel.
11 Israeli akamwambia Yusufu, “Sikutazamia kuuona uso wako tena, Lakini Mungu ameniruhusu kuwaona hata wanao.”
Izrael je Jožefu rekel: »Nisem si mislil, da bom videl tvoj obraz in, glej, Bog mi je pokazal tudi tvoje seme.«
12 Yusufu akawaondoa kati ya magoti ya Israeli, na kisha akainama na uso wake juu ya nchi.
Jožef ju je prestavil izmed svojih kolen in se sam, s svojim obrazom, priklonil k zemlji.
13 Yusufu akawachukua wote wawili, Efrahimu katika mkono wake wa kulia kuelekea mkono wa kushoto wa Israeli, na Manase katika mkono wake wa kulia kuelekea mkono wa kulia wa Israeli, na akawasogeza kwake.
Jožef je prijel oba, Efrájima na svojo desnico proti Izraelovi levici in Manáseja na svojo levico proti Izraelovi desnici in ju privedel k njemu.
14 Israeli akainua mkono wake wa kulia na kuuweka juu ya kichwa cha Efrahimu, aliyekuwa mdogo, na mkono wake wa kushoto juu ya kichwa cha Manase. Akaipishanisha mikono yake, kwani Manase ndiye alikuwa mzaliwa wa kwanza.
Izrael je iztegnil svojo desnico in jo položil na Efrájimovo glavo, ki je bil mlajši, svojo levico pa na Manásejevo glavo, premišljeno vodeč svoji roki, kajti Manáse je bil prvorojenec.
15 Israeli akambariki Yusufu, akisema, Mungu ambaye mbele zake baba zangu Ibrahimu na Isaka walitembea, Mungu aliyenilinda hata leo,
Blagoslovil je Jožefa in rekel: »Bog, pred katerim sta hodila moja očeta, Abraham in Izak, Bog, ki me je hranil vse moje dolgo življenje do današnjega dne,
16 malaika walionilinda na madhara yote, awabariki vijana hawa. Jina langu na litajwe kwao, na majina ya baba zangu Ibrahimu na Isaka. Na wawe makutano ya watu juu ya nchi.”
angel, ki me je odkupil od vsega zla, naj blagoslovi dečka. Naj bo moje ime imenovano na njiju in ime mojih očetov, Abrahama in Izaka. Naj zrasteta v množico na sredi zemlje.«
17 Yusufu alipoona baba yake ameweka mkono wake wa kulia juu ya kichwa cha Efrahimu, haikumpendeza. Akauchukuwa mkono wa baba yake auweke katika kichwa cha Manase.
Ko je Jožef videl, da je njegov oče svojo desnico položil na Efrájimovo glavo, ga je to razžalilo in prijel je roko svojega očeta, da jo odmakne z Efrájimove glave na Manásejevo glavo.
18 Yusufu akamwambia baba yake, “Sivyo babangu; kwani huyu ndiye mzaliwa wa kwanza. Uweke mkono wako juu ya kichwa chake.”
Jožef je svojemu očetu rekel: »Ne tako, moj oče, kajti ta je prvorojenec, svojo desnico položi na njegovo glavo.«
19 Baba yake akakataa na kusema, “Ninafahamu, mwanangu, nafahamu. Yeye naye atakuwa watu, naye pia atakuwa mkuu. Lakini mdogo wake atakuwa mkuu kuliko yeye, na uzao wake utakuwa wingi wa mataifa.”
Njegov oče pa je odklonil in rekel: »Vem to, moj sin, vem to, tudi on bo postal ljudstvo in tudi on bo velik, toda njegov mlajši brat bo resnično večji kakor on in njegovo seme bo postalo množica narodov.«
20 Israeli akawabariki siku hiyo kwa maneno haya, “Watu wa Israeli watatamka baraka kwa majina yenu wakisema, Mungu na akufanye kama Efrahimu na kama Manase'. “Kwa njia hii, Israeli akamweka Efrahimu mbele ya Manase.
Blagoslovil ju je ta dan, rekoč: »V tebi bo Izrael blagoslovljen, rekoč: ›Bog [naj] te naredi kakor Efrájima in kakor Manáseja‹« in Efrájima je postavil pred Manáseja.
21 Israeli akamwambia Yusufu, “Tazama, ninakaribia kufa, lakini Mungu atakuwa nanyi, na atawarudisha katika nchi ya baba zenu.
Izrael je rekel Jožefu: »Glej, jaz umrem, toda Bog bo z vami in vas bo ponovno privedel v deželo vaših očetov.
22 Kwako wewe, kwa kuwa uko juu ya ndugu zako, ninakupa mtelemko wa mlima niliouchukuwa kutoka kwa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.”
Poleg tega sem ti dal en delež nad tvojimi brati, ki sem ga s svojim mečem in s svojim lokom vzel iz roke Amoréjcev.«

< Mwanzo 48 >