< Mwanzo 48 >

1 Ikawa baada ya mambo haya, mmojawapo akamwambia Yusufu, “Tazama, baba yako ni mgonjwa.” Hivyo akaondoka pamoja na wanawe wawili, Manase na Efrahimu.
Some time later, someone told Joseph, “[Hey, ] your father is ill.” When Joseph heard that, he took his two sons, Manasseh and Ephraim, to see his father.
2 Yakobo alipoambiwa, “Tazama, mwanao Yusufu amekuja kukuona,” Israeli akakusanya nguvu na kukaa juu ya kitanda.
When someone told Jacob, “Look, your son Joseph has come to see you!” Jacob sat up on the bed, even though it was difficult for him to do that.
3 Yakobo akamwambia Yusufu, Mungu Mwenyezi alinitokea huko Luzu katika nchi ya Kanaani. Akanibariki na
He said to Joseph, “When I was at Luz in Canaan, God Almighty appeared to me. He blessed me
4 kuniambia, 'Tazama, nitakupa uzao mwingi, na kukuzidisha. Nitakufanya kuwa kusanyiko la mataifa. Nitakupa nchi hii wewe na uzao wako kuwa milki ya milele.'
and said to me, ‘I am going to enable you to become the father of many children. You will have many descendants, and they will become [the ancestors of] many people-groups. And I will give this land to your descendants to possess forever.’
5 Na sasa wanao wawili, waliozaliwa kwako katika nchi ya Misri kabla sijaja Misri, ni wangu. Efrahimu na Manase watakuwa wangu, kama walivyo Rubeni na Simioni.
“And now I will consider that your two sons, who were born to you here in Egypt before I came here, will (belong to me/be as though they are my sons). Ephraim and Manasseh will be [as though they were] my sons, and they will inherit my possessions, just like my sons Reuben and Simeon [and the others] will.
6 Watoto utakaowapata baada ya hapo ni wako; watahesabiwa katika majina ya ndugu zao katika urithi wao.
If you later become the father of any more children, they will not be considered to be my children, but as my grandchildren, and [in Canaan] they will receive as part of what they inherit some of the same land that is in the territory that their brothers [Ephraim and Manasseh] will inherit.
7 Lakini kwangu mimi, nilipokuja kutoka Padani, kwa uzuni yangu Raheli alikufa njiani katika nchi ya Kanaani, wakati kungalipo kitambo kwenda Efrathi. Nilimzika pale katika njia iendayo Efrathi” (ndio, Bethlehemu).
Many years ago, as I was returning from Paddan-Aram/Mesopotamia, your mother Rachel died in the Canaan region, while we were still traveling, not far from Ephrath [town]. So I buried her body there alongside the road to Ephrath [which is now called Bethlehem].”
8 Israeli alipowaona wana wa Yusufu, akasema, “Ni nani hawa?”
When Jacob saw Joseph’s sons, he asked, “Who are these boys?”
9 Yusufu akamwambia baba yake, “Hawa ni wanangu, Mungu alionipa hapa:” Israeli akasema, “Walete kwangu, kwamba niwabariki.”
Joseph replied, “They are the sons that God has given to me here in Egypt.” Jacob said, “Bring them close to me so that I can bless them.”
10 Basi macho ya Israeli yalikuwa yanashindwa kwa ajili ya umri wake, hivyo hakuweza kuona. Hivyo Yusufu akawasogeza karibu yake, na akawabusu na kuwakumbatia.
Jacob was almost blind because he was very old. He could not recognize the boys. So Joseph brought his sons close to his father, and Jacob kissed them and hugged them.
11 Israeli akamwambia Yusufu, “Sikutazamia kuuona uso wako tena, Lakini Mungu ameniruhusu kuwaona hata wanao.”
Jacob said to Joseph, “I did not expect to see you again, but look at this! God has allowed me to see not only you, but he has allowed me to see your children, too!”
12 Yusufu akawaondoa kati ya magoti ya Israeli, na kisha akainama na uso wake juu ya nchi.
Joseph took the boys from alongside Jacob’s knees. Then he bowed down with his face to the ground.
13 Yusufu akawachukua wote wawili, Efrahimu katika mkono wake wa kulia kuelekea mkono wa kushoto wa Israeli, na Manase katika mkono wake wa kulia kuelekea mkono wa kulia wa Israeli, na akawasogeza kwake.
Then Joseph took both of the boys, putting Ephraim on his right side toward Jacob’s left hand, and putting Manasseh on his left side toward Jacob’s right hand, and brought them close to Jacob.
14 Israeli akainua mkono wake wa kulia na kuuweka juu ya kichwa cha Efrahimu, aliyekuwa mdogo, na mkono wake wa kushoto juu ya kichwa cha Manase. Akaipishanisha mikono yake, kwani Manase ndiye alikuwa mzaliwa wa kwanza.
But Jacob [did not do what Joseph wanted him to do. Instead], he reached out his right hand and put it on Ephraim’s head, even though he was the younger son. He crossed his arms and put his left hand on Manasseh’s head, even though Manasseh was the older son.
15 Israeli akambariki Yusufu, akisema, Mungu ambaye mbele zake baba zangu Ibrahimu na Isaka walitembea, Mungu aliyenilinda hata leo,
Then he (blessed/asked God to bless) Joseph and his sons, saying, “My grandfather Abraham and my father Isaac conducted their lives as God desired, and to this very day God has led me and taken care of me as a shepherd leads and cares for his sheep [MET].
16 malaika walionilinda na madhara yote, awabariki vijana hawa. Jina langu na litajwe kwao, na majina ya baba zangu Ibrahimu na Isaka. Na wawe makutano ya watu juu ya nchi.”
The angel whom he sent has kept me from being harmed in any way. I pray that God will bless these boys. I pray that people will never forget about me and about Abraham and Isaac because of what God does for these boys. I pray that they will have many descendants who will live all over the earth.”
17 Yusufu alipoona baba yake ameweka mkono wake wa kulia juu ya kichwa cha Efrahimu, haikumpendeza. Akauchukuwa mkono wa baba yake auweke katika kichwa cha Manase.
When Joseph saw that his father had placed his right hand on Ephraim’s head and not on Manasseh’s head, he was distressed/displeased. So he took his father’s hand to move it from Ephraim’s head to Manasseh’s head.
18 Yusufu akamwambia baba yake, “Sivyo babangu; kwani huyu ndiye mzaliwa wa kwanza. Uweke mkono wako juu ya kichwa chake.”
Joseph said to him, “My father, that is not right! The one on whom you put your left hand is my older son. Put your right hand on his head.”
19 Baba yake akakataa na kusema, “Ninafahamu, mwanangu, nafahamu. Yeye naye atakuwa watu, naye pia atakuwa mkuu. Lakini mdogo wake atakuwa mkuu kuliko yeye, na uzao wake utakuwa wingi wa mataifa.”
But his father refused, saying, “I know that, my son, I know what I am doing. Manasseh’s descendants will also become a people-group, and they will become important. But his younger brother’s descendants will become greater than his will. His descendants will become several nations.”
20 Israeli akawabariki siku hiyo kwa maneno haya, “Watu wa Israeli watatamka baraka kwa majina yenu wakisema, Mungu na akufanye kama Efrahimu na kama Manase'. “Kwa njia hii, Israeli akamweka Efrahimu mbele ya Manase.
So he blessed them both on that day, saying, “The people in Israel will use your names when they bless people. They will say, ‘We pray that God will help you as he helped Ephraim and Manasseh.’” In that way, Jacob said that Ephraim would become more important than Manasseh.
21 Israeli akamwambia Yusufu, “Tazama, ninakaribia kufa, lakini Mungu atakuwa nanyi, na atawarudisha katika nchi ya baba zenu.
Then Jacob said to Joseph, “I am about to die. But I know that God will help/protect you. And some day he will take your descendants back to the land of their ancestors.
22 Kwako wewe, kwa kuwa uko juu ya ndugu zako, ninakupa mtelemko wa mlima niliouchukuwa kutoka kwa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.”
And it is to you, not to your brothers, that I will give the fertile hill in the Shechem area. I captured that land from the Amor people-group, fighting them with my sword and my bow and arrows.”

< Mwanzo 48 >